Cristiano Ronaldo amefanikiwa kushinda tuzo ya Alfred De Stefano ya mchezaji bora wa Ligi Kuu Hispania LaLiga msimu wa 2015/2016, tuzo ambazo zimeandaliwa na gazeti la Hispania la Marca, Ronaldo kapokea tuzo hiyo siku aliyosaini mkataba wa miaka mitano Real Madrid.Hata hivyo mchezaji mwenzake na Ronaldo wanaecheza nae katika klabu ya Real Madrid Alvaro Morata ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa Hispania wakati kocha wa Atletico Madrid Diego Simeone ameshinda tuzo ya Miguel Munoz ya kocha bora wa mwaka.