Nipe Maji
JF-Expert Member
- Mar 25, 2025
- 335
- 190
Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (Rea), Mhandisi Hassan Said ametangaza kukamilika kwa miradi minne mikubwa ya umeme inayolenga kuleta nishati katika vijiji 5,259, ikijumuisha vijiji 4,071 na vitongoji 188, katika awamu ya tatu, mzunguko wa pili.
Miradi hii ni sehemu ya juhudi za Serikali kuhakikisha vijiji na vitongoji vingi vinapata huduma ya umeme kama sehemu ya majukumu yake ya kuunga mkono maendeleo ya maeneo ya vijijini.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi la Rea, Mhandisi Said alieleza kuwa miradi hii ni matokeo ya ombi la viongozi wa serikali kuu linalohimiza kufikishwa kwa huduma ya umeme katika maeneo hayo, ili kuboresha maisha ya wananchi wa vijijini.
"Miradi hii ni hatua kubwa katika kufikia lengo letu la kuhakikisha nishati inafika vijijini na maeneo yaliyokuwa hayafikiki. Tunajivunia mafanikio haya, na tutaendelea kufanya juhudi kuongeza maeneo yanayohudumiwa," alisema Mhandisi Said.
Mbali na miradi hiyo, Rea pia imeanzisha mradi mwingine wa kupeleka umeme katika vitongoji vipatavyo 9,000.
Hatua hii inatarajiwa kuongeza wigo wa umeme na kupunguza changanmoto za upatikanaji wa nishati kwa wananchỉ wa maeneo hayo.
ea ucha
Miradi hii ni sehemu ya juhudi za Serikali kuhakikisha vijiji na vitongoji vingi vinapata huduma ya umeme kama sehemu ya majukumu yake ya kuunga mkono maendeleo ya maeneo ya vijijini.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi la Rea, Mhandisi Said alieleza kuwa miradi hii ni matokeo ya ombi la viongozi wa serikali kuu linalohimiza kufikishwa kwa huduma ya umeme katika maeneo hayo, ili kuboresha maisha ya wananchi wa vijijini.
"Miradi hii ni hatua kubwa katika kufikia lengo letu la kuhakikisha nishati inafika vijijini na maeneo yaliyokuwa hayafikiki. Tunajivunia mafanikio haya, na tutaendelea kufanya juhudi kuongeza maeneo yanayohudumiwa," alisema Mhandisi Said.
Mbali na miradi hiyo, Rea pia imeanzisha mradi mwingine wa kupeleka umeme katika vitongoji vipatavyo 9,000.
Hatua hii inatarajiwa kuongeza wigo wa umeme na kupunguza changanmoto za upatikanaji wa nishati kwa wananchỉ wa maeneo hayo.