RC Paul Makonda: Watu wameandika barua kupinga Tanzania kuingia kwenye Uchumi wa kati

Libya

JF-Expert Member
Nov 11, 2016
783
1,918


------------
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Paulo Makonda amesema kuwa kwa fedha ya kitanzia ni kipato cha mtanzania kuwa na dola milioni mbili mpaka tatu kwenda mpaka milioni tisa mpaka kumi, ameongeza kuwa benki ya dunia imekubali kuwa Tanzania imefika kwenye hivyo vigezo vya uchumi mdogo wa kati.

Mh. Makonda amesema kuwa zipo faida nyingi kwa kufikia hatua hiyo, nazo ni:
  • Taifa linaondoka kwenye kuwekewa vikwazo linapotaka kujipangia mambo yake ya kiuchumi.
  • Taifa linakuwa na uwezo wa kujitegemea kutoka kwenye maisha ya kuwa ombaomba na kuwa na uwezo wa kujitegemea.
  • Taifa lina kuwa na uwezo wa kukopa na kukopesheka kwa sababu uchumi wake unakuwa imara na una sifa ya kulipa na ndio maana unapata nafasi ya kutangazwa kuingia kwenye Uchumi wa kati.
Mh. Makonda aliendelea kwa kumpongeza Rais Magufuli na Watanzania waliokubali kuendelea kuchapa kazi hata wakati wa corona lakini pia akatoa pongezi kwa Chama Cha Mapinduzi kwa kusimamia utekelezaji wa ilani kwa asilimia 99.

Mh. Makonda aliendelea kwa kumuita Mh. Zitto Kabwe kuwa ni mtu mbishi, na kuwa Mh. Zitto anampango wa kuandika barua kwenda benki ya Dunia kupinga Benki ya Dunia kuitangaza Tanzania kuingia Uchumi wa kati na kuwa miongoni mwa nchi tano duniani zilizoingia kwenye uchumi wa kati mwaka 2020 tena kwenye kipindi ambacho uchumi umetikisika kwa mataifa mengine lakini Tanzania imebaki kuwa salama.
 
Libya,

Mimi ni kijani, kwa Mujibu wa Nape nilimsikiliza akiwa bungeni alisema wao ndo waliandika ilani na serikali hii imekwenda kinyume kabisa na ilani inayotaka kuzingati social welfare services maisha ya raia kuwa bora japo Nape aliipongeza kwa kujenga miundombinu!
 
Tanzania imefika kwenye hivyo vigezo vya uchumi mdogo wa kati.
Kwenye kichwa cha habari umeandika uchumi wa kati

Ukija kwenye habari umeandika hayo maneno hapo juu.
Naomba kujuzwa tofauti ya "uchumi wa kati" na "uchumi mdogo wa kati"
 
Kwenye kichwa cha habari umeandika uchumi wa kati

Ukija kwenye habari umeandika hayo maneno hapo juu.
Naomba kujuzwa tofauti ya "uchumi wa kati" na "uchumi mdogo wa kati"
Nchi iko lower middle income mkuu! Bado hatujafikia uchumi wa kati halisi tuko mbioni kuufikia! ni mbwembwe zetu kijani tu!
 
Huko kwenye uchumi nambari 1 kama USA UK watu wote wanakazi ??
Acheni kutoa kauli au maandishi ya kipimbi pimbi
uchumi wa namba moja sote tunajua kama huna job unakwenda manispaa kuchukua mpunga wa kula kila mwezi hiyo ndio tofauti , tofauti sie maskini wao matajiri, sie huna kazi unashinda kijiweni unakufa njaa wao huna kazi unakula muvi ndani mwako mwisho wa mwezi nenda manispaa kachukue pesa ( unemployment relief/ benefit)!

mkuu amka jitahidi another time usilinganishe US ( mtaji US dollar 20 trillion) na bongo ( mtaji US dollar billion 60)!! mtafute mtu akuelezee tofauti ya hizi pesa!!
 
uchumi wa namba moja sote tunajua kama huna job unakwenda manispaa kuchukua mpunga wa kula kila mwezi hiyo ndio tofauti , tofauti sie maskini wao matajiri, sie huna kazi unakufa njaa wao huna kazi nenda manispaa kachukue pesa! mkuu jitahidi another time usilinganishe US ( mtaji US dollar 20 trillion) na bongo ( mtaji US dollar billion 60)!! mtafute mtu akuelezee tofauti ya hizi pesa!!
Mimi nilikuwa na question kauli ya Odhiambo , sio kufananisha sie na Dunia ya Kwanza
 
Back
Top Bottom