RC Makonda, Dar ni jiji la wote, vyama vyote. Mbowe sio mwanasiasa uchwara aliyefilisika, Zitto sio mshirikina. Tunakupenda, heshimu wote uheshimiwe

RC Makonda, Dar ni jiji la wote, vyama vyote. Mbowe sio mwanasiasa uchwara aliyefilisika, Zitto sio mshirikina. Tunakupenda, heshimu wote uheshimiwe

Mimi sioni ubaya wa kauli ya RC Makonda, hasa kwa wasiomjua ndio huwa wanapata tabu, kinachomfanya Makonda aendelee kuwa RC wa Dar ni hizo kauli zake ambazo kwa wasiojua siasa huchukulia kama ni zakukela, la hasha, Makonda ni mtu wa watu,na hufanya hivyo kwa mikakati mahusi ya kisiasa.

So mwacheni RC apige kazi, hizo kauli zake ni moja ya majukumu yake na ndio zinamfaya aendeleee kuwa RC bora na anayependwa na watu wengi sana kwa tz yetu

Sent using Jamii Forums mobile app
RC Bora!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huo ndio mnara wa babeli watu wananena kwa lugha zao.nMadaraka yamekuwa machungu wanasiasa wanamtafuta mchawi.

Na huo ndio mwanzo lakini ule mwisho bado so usiogope Pascal. Wanasiasa wetu wataongea mambo ya kushangaza zaidi ya hayo unayoyaita matukano.

Maendeleo hayana vyama!
Akili zinakujaaaa! Zinaondokaaa!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanabodi

Huu mtindo wa viongozi wetu wenye dhamana kutoa kauli za hovyo hovyo, kauli za udhalilishaji na za kimipasho mipasho zinazidi kushika kasi, japo najua wanamuiga nani kwa utoaji wa kauli hizi, hivi hawamuoni Makamo wa rais Mhe. Mama Samia Suhuhu Hassan, kwani yeye hana mdomo?. Ua hawamuoni Waziri Mkuu, Mhe. Kasim Majaliwa Majaliwa, kwani yeye hana mdomo?

Mbona viongozi hawa hawatumii lugha za kuudhi?. Mwalimu Nyerere aliwahi kuwashangaa viongozi wa taifa lete kwa kukuri kuwa kila awamu, ina mazuri yake na mabaya yake, akawashangaa viongozi badala ya kuiga mazuri, wao wanaiga mabaya!. Hivyo viongozi wetu pia wana mazuri yao na mabaya yao, hivyo nyie viongozi, msiige kile kitu cha viongozi wakuu wenu, igeni mazuri yao, mabaya yao waachieni. Nyie mnaiga tuu yote yakiwemo mabaya!. Miongoni mwa baadhi ya mabaya ya awamu hii, ni kauli za hovyo hovyo za baadhi ya viongozi ambazo badala ya kujenga umoja na mshikamano, zinachochea utengano na mifarakano.

Mimeisikia hii kauli ya hii ya RC Makonda



Kiukweli kauli hii sio kauli nzuri. RC Makonda, Makonda ni Mkuu wa Mkoa wetu wa Dar es Salaam. Jiji la Dar es Salaam ni metropolitan society, lina watu wa aina zote na vyama vyote dini zote, hali zote. Ni Jiji la wote. Makonda amemuita Mhe. Mbowe ni mwanasiasa uchwala aliyefilisika, amemuita Mhe. Zitto ni mganga wa kienyeji na mshirikina!. Hizo ni lugha za matukano, ni lugha za kuudhi.
Kwa wanaopenda makala fupi, tuishie hapa
kwa wale wakata issues tuendelee
Pascal mayalla,Ana unguli wa kinafiki.
Naamini anaendesha maisha kwa njia hiyo pia. Aliandika bandiko la kusifia muamala unasoma.

Leo hapa ana danganya kumkosoa makonda akiamini sisi ni watoto.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pachal, semea nafsi yako usisemee watu, siyo kila mtu anampenda unayempenda.

Kwanza kafanya kosa la kukusanya watu na huku kuna janga la kimataifa, Pili naunga mkono hoja kuwa asiwatukane viongozi wa wapinzani kwani katika mkoa anaouongoza wapo wapinzani pia ambao wanakerwa na kauli zake.

Kisha yeye ni kiongozi wa umma, aachane na mambo ya siasa kwani anawaongoza wote wananchi kwa pamoja na hatakiwi kubagua, Baada ya kujiheshimu, ATULIZANE.
Acha zako!
Kauri za mbowe lazima zishutumiwe na viongozi!
Makonda yupo sawa maana ndiyo kauri wanazozitumia hata wao kumtukania rais
 
Kama mbowe cyo mwanasiasa uchwara ni nani! Maana huwezi kuhamasisha mikutano ndani ya corona tena imeanzia jimboni kwako.

Ila baada ya mwanao kuugua unatangaza kuzuia huku ukitaka makanisa yafungwe.
Kama siyo siasa uchwala basi nipeni jibu ni siasa gani.
 
Kama mbowe cyo mwanasiasa uchwara ni nani! Maana huwezi kuhamasisha mikutano ndani ya corona tena imeanzia jimboni kwako.

Ila baada ya mwanao kuugua unatangaza kuzuia huku ukitaka makanisa yafungwe.
Kama siyo siasa uchwala basi nipeni jibu ni siasa gani.
Unachoandika kinafanana na lishe duni uliyopata, rudi huku makete ukatwe govii yako kwa msaada wa watu wa Marekani
 
Elimu /busara na exposure ni jambo muhimu sana,ukikosa vyote lazima uwe kituko mbele ya jamii,maana utaona kama unajenga kumbe unabomoa mpaka nyumba yako mwenyewe
 
Bahati Nzuri Mungu alituweka wote sawa kwa kila kitu kasoro haya ya Dunia ambayo hupita kwa muda..Ni muda wake ni jukumu lake ama autumie vibaya au autumie kujijenga.

akiutumia Vibaya hata wanae atawaachia shida manake watachukiwa bure kumbe hawana kosa ila kwa kujijenga atapendwa na kizazi angalia Kizazi cha Kennedy kule US.

Nyerere,, au Mandela Vs..Watoto wa Ghadafi au Sadam Hussen naamini kuna siku walitamani kukana majina yao.Tujifunze.
 
Back
Top Bottom