PostGE2025 RC Chalamila: Hatukusema Wananchi wakae ndani

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
5,185
Reaction score
17,704
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amezungumza na Global TV na kuelezea hali ya ulinzi na usalama ilivyo jijini Dar es Salaam, amesema "Hatukusema Wananchi wakae ndani"

Your browser is not able to display this video.
 
Wanaendesha nchi kihuni sana. Jana nilisema humu ndani, wanataka faida za curfew bila kutangaza hiyo curfew waziwazi.

Wanasema wanatoa ushauri ila ni amri ili baadae warudi kama hivi wajisifu nchi ilikuwa imetulia na hatukuwalazimisha watu wakae ndani.

Kesho utawaambia watu tena kwamba unawashauri wakae ndani watakugomea maana watakumbuka uliwahi kusema hivyo baadae ukawaambia haukuwalazimisha kukaa ndani.

Nchi ina ombwe kubwa la kiuongozi. Shida ni kwamba, mtaongoza nchi kwa njia za janja janja kama hivi mpaka lini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…