puker
JF-Expert Member
- Nov 22, 2018
- 940
- 1,847
Habari za muda huu ndugu zangu.
Katika hali ya kawaida ni vigumu kunielewa kama hayajakukuta.
Pombe imeniharibia vingi sana kwenye maisha yangu zaidi ya kunipa faida.
- Pombe imemaliza fedha nyingi mno kiasi ambacho speed ya maendeleo yangu ni madogo ukilinganisha na kipato changu.
- Pombe imenipotezea marafiki wa maaana na kubaki na walevi ambao waliowengi ni wapumbavu.
- Pombe imenitenganisha na Mungu ni marachache sana kwa walevi kwenda ibadani maana jana yake ambapo Jumamosi wamekesha kwenye pombe wakifurahia weekend.
- Pombe imenifanya nipate ajali nyingi kwa mwaka huu tu, jana ilikuwa ajali ya 11 ambapo ilitaka kuchukua uhai wangu kabisa lakini Mungu hakuniacha aendelea kunilinda na kunipa muda wa kujibadilisha
- Pombe imenukutanisha na wanawake wa ajabu kwa ajili tu ya kujiridhisha kimwili ambapo na amini wamebeba laana na mkosi mingi mno, lakini Pia Mungu hakuniacha aliendelea kunilinda Afya yangu bado iko poa.
- Pombe imenifanya kutokuwa mwaminifu kazini, nimekuwa mwizi nguli ili mradi tu nipate hela ya kulewa.
-Pombe imenifanya hadi sasa nina miaka 33+ sina mke wala mtoto na sifikirii najiona mjinga sana katika hili.
Nina mengi mno yakustaajabisha na kutia simanzi sababu ya pombe, Nakiona kifo kipo karibu yangu kama nisipo badilika.
Namshukuru Mungu sana kwa kuendelea kua nami hali ya kuwa nimekuwa nikimkose, Namuomba Mungu sana Leo tarehe 01/07/2022 iwe mwisho wa mahusiano na pombe Maisha yangu yote Eeeh mwenyezi Mungu nisaidie.
Katika hali ya kawaida ni vigumu kunielewa kama hayajakukuta.
Pombe imeniharibia vingi sana kwenye maisha yangu zaidi ya kunipa faida.
- Pombe imemaliza fedha nyingi mno kiasi ambacho speed ya maendeleo yangu ni madogo ukilinganisha na kipato changu.
- Pombe imenipotezea marafiki wa maaana na kubaki na walevi ambao waliowengi ni wapumbavu.
- Pombe imenitenganisha na Mungu ni marachache sana kwa walevi kwenda ibadani maana jana yake ambapo Jumamosi wamekesha kwenye pombe wakifurahia weekend.
- Pombe imenifanya nipate ajali nyingi kwa mwaka huu tu, jana ilikuwa ajali ya 11 ambapo ilitaka kuchukua uhai wangu kabisa lakini Mungu hakuniacha aendelea kunilinda na kunipa muda wa kujibadilisha
- Pombe imenukutanisha na wanawake wa ajabu kwa ajili tu ya kujiridhisha kimwili ambapo na amini wamebeba laana na mkosi mingi mno, lakini Pia Mungu hakuniacha aliendelea kunilinda Afya yangu bado iko poa.
- Pombe imenifanya kutokuwa mwaminifu kazini, nimekuwa mwizi nguli ili mradi tu nipate hela ya kulewa.
-Pombe imenifanya hadi sasa nina miaka 33+ sina mke wala mtoto na sifikirii najiona mjinga sana katika hili.
Nina mengi mno yakustaajabisha na kutia simanzi sababu ya pombe, Nakiona kifo kipo karibu yangu kama nisipo badilika.
Namshukuru Mungu sana kwa kuendelea kua nami hali ya kuwa nimekuwa nikimkose, Namuomba Mungu sana Leo tarehe 01/07/2022 iwe mwisho wa mahusiano na pombe Maisha yangu yote Eeeh mwenyezi Mungu nisaidie.