Rasmi kocha Fadlu Davis awaaga wanasimba

Rasmi kocha Fadlu Davis awaaga wanasimba

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram aliyekuwa kocha wa Simba Sc Fadlu Davis amewaaga wanasimba Kwa kuandika...

"Ni kwa moyo mzito naiaga Simba SC. Tangu nilipowasili, nilihisi shauku ya klabu hii kubwa na upendo wa mashabiki wake wa ajabu. Pamoja tulipigana, tukasherehekea, na tukaimarika kupitia kila ushindi na kila changamoto. Shukrani zangu za dhati kwa Rais Mo Dewji kwa uongozi wake wa kutia moyo, maono na usaidizi wake wa kudumu.

Kwa wachezaji: endeleeni kupigana, endeleeni kuamini, na endeleeni kuinua beji kwa heshima.

Kwa wafanyakazi na wasimamizi: asanteni kwa uaminifu wenu na kujitolea bila kuchoka nyuma ya pazia.
Kwa mashabiki wa Simba: ninyi ndiyo mapigo ya moyo ya klabu hii. Sauti zenu, nyimbo zenu, shauku yenu isiyoyumba zitasikika daima katika kumbukumbu yangu.

Asanteni kwa kukaribisha familia yangu kama yenu.

Simba daima itabaki sehemu yangu, na ninaikitakia klabu mafanikio, mafanikio na vikombe mbele.

Asanteni sana, forever Nguvu Moja."
Screenshot_20250922-155747.png
 
Kila la heri kwake. Kwa kweli kelele zilikuwa ni nyingi mpaka zikageuka kuwa kero.
 
Salamu za huzuni ziwafikie mikia star, sis kama wana Daima mbele nyuma mwiko tumeskitishwa sana na majanga yanayo endelea huko kwenu.
 
Mamluki was Simba wanachokitafuta watakipata
Unaruka mkojo unaenda kukanyaga😭😭😭
 
Huyo siyo kocha; hata huko Raja Casablanca hatadumu. Hajui kutumia wachezaji, anatagemea uwezo binafsi wa wachazej badala ya yeye kuwafundisha mbinu za ushindi. Nimesikia kuwa alichukizwa na Simba kushindwa kumsajiri fei toto
 
Semaji la caf limewaambia kolo fans kua kocha kaenda mapumziko siku mbili

Jamaa sijui huwa anawachukuliaje mashabiki wa 5imba.
 
Fadlu Davis kawaacha wachezaji top na mastaa kibao wakiwemo alasane kante mdogo wake na ngolo kante,jean charles ahoua,kibu d mkandaji na elie mpanzu kibisawala na amekimbilia uarabuni,ina mana kaona hawa kina mkandaji ni mbwembwe za semaji lakini uhalisia ni zero? Nenda baba tutakukumbuka daima na ipo siku utarudi kuendeleza kipigo kutoka kwa YANGASC
 
Hamna kocha pale nyinyi mmefikisha makocha 10 mpaka sasa
Nyinyi hata aje kocha gani! Mtalalamika tu. Maana kuanzia viongozi wenu, mpaka nyinyi mashabiki; wote ni makocha wenye leseni A za CAF.
 
Nyinyi hata aje kocha gani! Mtalalamika tu. Maana kuanzia viongozi wenu, mpaka nyinyi mashabiki; wote ni makocha wenye leseni A za CAF.
Sasa nyinyi ambao hamna leseni za Caf kinachowafanya mbadilishe mara kwa mara ni kitu gani.
 
Sasa nyinyi ambao hamna leseni za Caf kinachowafanya mbadilishe mara kwa mara ni kitu gani.
Kocha aliyebadilishwa kwenye timu yetu ni Miguel Gamondi tu. Na ilikuwa ni baada ya kushindwa kudhibiti nidhamu ya wachezaji nje na ndani ya uwanja.

Makocha wengine mfano Nabi aliondoka baada ya kuipa timu mafanikio! Na wengine waliondoka baada ya kupata ofa nono. Ila siyo kwa sababu ya gubu la mashabiki, au baadhi ya viongozi wa timu.
 
Back
Top Bottom