Rasilimali za nchi hatizakiwi kutumika kumtetea mtu yeyote yule katika Mahakama ya ICC

Rasilimali za nchi hatizakiwi kutumika kumtetea mtu yeyote yule katika Mahakama ya ICC

Keynez

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2007
Posts
3,620
Reaction score
6,510
Tanzania imekuwa na ujinga mmoja ambapo rasilimali za nchi zimekuwa zinatumika kumlinda, kumtetea na hata kufungulia mashtaka watu kwa kesi binafsi za kiongozi.

Unaweza kukuta mtu anachapisha jambo fulani kuhusu kiongozi fulani, ambalo labda jamii, muhusika au vyombo vya serikali vinalitafsiri ni kashfa, kumvunjia heshma, nk.

Badala ya yeye kiongozi mwenyewe kufungua kesi binafsi, atatumia Polisi, DPP na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kumkamata na kumfungulia mashtaka mtu yule kwa makosa mengine (utasikia makosa ya kimtandao, uchochezi, uhujumu uchumi, nk.) wakati hapo ilitakiwa kiongozi atafute Wakili binafsi na kufungua kesi ya madai.

Huu ulikuwa ni utangulizi. Twende katika hoja ya uzi huu.

Nia ya uzi huu ni kukumbusha kuwa iwapo kuna mtu au watu watafunguliwa mashtaka yoyote katika Mahakama ya ICC kuhusiana na matukio ya MO29, kesi hizo zitawahusu wao binafsi na uhusika wao katika matukio yale.

Rasilimali za nchi hazitakiwi kutumika kuwatetea wala kuwalinda watu hao katika kesi hizo. Kama wataamua kumtumia Wakili Kibatala litakuwa jambo jema ili pesa ibaki hapa hapa nchini.

Haitakiwi pesa na rasilimali zingine za nchi kutumika kulipia wanasheria wa ndani au nje ya nchi kwa ajili ya utetezi wa watu hawa.

Ujumbe huu umfikie CAG!
 
Tanzania imekuwa na ujinga mmoja ambapo rasilimali za nchi zimekuwa zinatumika kumlinda, kumtetea na hata kufungulia mashtaka watu kwa kesi binafsi za kiongozi.

Unaweza kukuta mtu anachapisha jambo fulani kuhusu kiongozi fulani, ambalo labda jamii, muhusika au vyombo vya serikali vinalitafsiri ni kashfa, kumvunjia heshma, nk.

Badala ya yeye kiongozi mwenyewe kufungua kesi binafsi, atatumia Polisi, DPP na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kumkamata na kumfungulia mashtaka mtu yule kwa makosa mengine (utasikia makosa ya kimtandao, uchochezi, uhujumu uchumi, nk.) wakati hapo ilitakiwa kiongozi atafute Wakili binafsi na kufungua kesi ya madai.

Huu ulikuwa ni utangulizi. Twende katika hoja ya uzi huu.

Nia ya uzi huu ni kukumbusha kuwa iwapo kuna mtu au watu watafunguliwa mashtaka yoyote katika Mahakama ya ICC kuhusiana na matukio ya MO29, kesi hizo zitawahusu wao binafsi na uhusika wao katika matukio yale.

Rasilimali za nchi hazitakiwi kutumika kuwatetea wala kuwalinda watu hao katika kesi hizo. Kama wataamua kumtumia Wakili Kibatala litakuwa jambo jema ili pesa ibaki hapa hapa nchini.

Nisingependa na halitakuwa jambo sahihi kuona Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali inatumika kumtetea mtu yoyote katika kesi hizo.
Hujui ulichokiandika, zaidi ya kutawaliwa na ushabiki wa kisiasa.

Unaelewa maana na ukubwa wa kiapo anachokula kiongozi mbele ya hadhara?.

ICC hawaendi watu kama vile tunavyoenda ferry kununua samaki aina ya vibua.
 
Hujui ulichokiandika, zaidi ya kutawaliwa na ushabiki wa kisiasa.

Unaelewa maana na ukubwa wa kiapo anachokula kiongozi mbele ya hadhara?.

ICC hawaendi watu kama vile tunavyoenda ferry kununua samaki aina ya vibua.
Nani alikuwa Mwanasheria wa Bill Clinton katika skendo na kesi ya Monica?

Nani alikuwa Mwanasheria wa Uhuru Kenyatta katika kesi ya ICC?

Nani alikuwa Mwanasheria wa Trump katika kesi ya impeachment?

Niambie kama Ofisi za Mwanasheria Mkuu wa Serikali za Marekani na Kenya au pesa za serikali zilitumika kuwatetea Marais hao.
 
rasilimali za nchi zimekuwa zinatumika kumlinda,

Pia wahuni hawa hupenda kujibainisha na soveriniti / Sovereignty , hivyo lkuwa kichaka chao cha kutafutia kinga.

Sovereignty ni raia wa jamhuri na siyo mali ya watenda maovu waliojipachika ktk mamlaka kupitia uchafuzi wa uchaguzi wanaotakiwa kushtakiwa ICC The Hague


Sovereniti kwa watu," auUhuru wa watu , ndio kanuni kuu ya kidemokrasia kwamba nguvu na mamlaka ya mwisho ya kisiasa yanabaki kwa raia


Dhana Muhimu
  • Uhuru wa Watu (sovereniti ) : Wazo kwamba nguvu ya serikali inatokana na ridhaa ya watawaliwa; watu ndio chanzo kikuu cha mamlaka.
  • Uhuru wa Kisiasa dhidi ya Kisheria : Katika demokrasia, watu wana mamlaka ya kisiasa (mamlaka ya kuchagua viongozi wanaowataka kwa ridhaa), huku wawakilishi waliochaguliwa kupitia uchaguzi huru wakishikilia mamlaka ya kisheria (mamlaka ya kutunga sheria).
  • Uwakilishi : Raia hugawa mamlaka yao kwa maafisa waliochaguliwa kupitia uchaguzi huru (Bunge, Bunge) ambao hutawala kwa niaba yao, na kuwafanya wawajibike kwa wapiga kura.
 
Hujui ulichokiandika, zaidi ya kutawaliwa na ushabiki wa kisiasa.

Unaelewa maana na ukubwa wa kiapo anachokula kiongozi mbele ya hadhara?.

ICC hawaendi watu kama vile tunavyoenda ferry kununua samaki aina ya vibua.
Screenshot_20260111-210830~2.png
 
Pia wahuni hawa hupenda kujibainisha na soveriniti / Sovereignty , hivyo lkuwa kichaka chao cha kutafutia kinga.

Sovereignty ni raia wa jamhuri na siyo mali ya watenda maovu waliojipachika ktk mamlaka kupitia uchafuzi wa uchaguzi wanaotakiwa kushtakiwa ICC The Hague


Sovereniti kwa watu," auUhuru wa watu , ndio kanuni kuu ya kidemokrasia kwamba nguvu na mamlaka ya mwisho ya kisiasa yanabaki kwa raia


Dhana Muhimu
  • Uhuru wa Watu (sovereniti ) : Wazo kwamba nguvu ya serikali inatokana na ridhaa ya watawaliwa; watu ndio chanzo kikuu cha mamlaka.
  • Uhuru wa Kisiasa dhidi ya Kisheria : Katika demokrasia, watu wana mamlaka ya kisiasa (mamlaka ya kuchagua viongozi wanaowataka kwa ridhaa), huku wawakilishi waliochaguliwa kupitia uchaguzi huru wakishikilia mamlaka ya kisheria (mamlaka ya kutunga sheria).
  • Uwakilishi : Raia hugawa mamlaka yao kwa maafisa waliochaguliwa kupitia uchaguzi huru (Bunge, Bunge) ambao hutawala kwa niaba yao, na kuwafanya wawajibike kwa wapiga kura.
Ufafanuzi mzuri. Kama wameshindwa kuwaelewa Wananchi, ngoja wakaeleweshwe huko ICC.
 
Utaratibu Huwa unakuaje hadi wanamkamata mtuhumiwa yoyote hao ICC?
Isingeundwa ile tume ya Chande mpaka muda huu Samia angeshapelekwa ICC.

Makosa yaliyofanyika yanaitwa 'crime against humanity' mauaji ya binadamu, makosa yanayotendwa dunia nzima kila siku hivyo yanaruhusiwa kisheria kuundiwa tume ya Rais hata kama ni yeye anayehusika na mauaji hayo.

Ingekuwa imetendwa genocide mauaji ya halaiki, mfano SSH angekuwa kafanya uhalifu dhidi ya kabila fulani mmoja la Tanzania mpaka muda huu angeshakamatwa na kushtakiwa na kuhukumiwa.
 
Isingeundwa ile tume ya Chande mpaka muda huu Samia angeshapelekwa ICC.

Makosa yaliyofanyika yanaitwa 'crime against humanity' mauaji ya binadamu, makosa yanayotendwa dunia nzima kila siku hivyo yanaruhusiwa kisheria kuundiwa tume ya Rais hata kama ni yeye anayehusika na mauaji hayo.

Ingekuwa imetendwa genocide mauaji ya halaiki, mfano SSH angekuwa kafanya uhalifu dhidi ya kabila fulani mmoja la Tanzania mpaka muda huu angeshakamatwa na kushtakiwa na kuhukumiwa.
Taja kesi yoyote ya ICC ambayo mtuhumiwa alikamatwa ndani ya miezi 3 toka tukio analoshitakiwa nalo lilipotokea.
 
Sina rekodi hizo sifanyi kazi ya kuzitunza. Rais kuunda tume tayari keshajiwekea kinga ya kisheria.
Kama hauna rekodi hizo, nini kinakufanya useme "sasa hivi angekuwa ameshakamatwa, kushtakiwa na kuhukumiwa" kama unavyodai?

Tunajua Tume ya Chande ni "delaying tactic" ila ICC wanaweza kudili na wewe hata miaka 10 mbele huko. Hiyo siyo kinga. ICC haipotezi mamlaka yake kisa Rais kaunda Tume yake ya uchunguzi.
 
Tanzania imekuwa na ujinga mmoja ambapo rasilimali za nchi zimekuwa zinatumika kumlinda, kumtetea na hata kufungulia mashtaka watu kwa kesi binafsi za kiongozi.

Unaweza kukuta mtu anachapisha jambo fulani kuhusu kiongozi fulani, ambalo labda jamii, muhusika au vyombo vya serikali vinalitafsiri ni kashfa, kumvunjia heshma, nk.

Badala ya yeye kiongozi mwenyewe kufungua kesi binafsi, atatumia Polisi, DPP na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kumkamata na kumfungulia mashtaka mtu yule kwa makosa mengine (utasikia makosa ya kimtandao, uchochezi, uhujumu uchumi, nk.) wakati hapo ilitakiwa kiongozi atafute Wakili binafsi na kufungua kesi ya madai.

Huu ulikuwa ni utangulizi. Twende katika hoja ya uzi huu.

Nia ya uzi huu ni kukumbusha kuwa iwapo kuna mtu au watu watafunguliwa mashtaka yoyote katika Mahakama ya ICC kuhusiana na matukio ya MO29, kesi hizo zitawahusu wao binafsi na uhusika wao katika matukio yale.

Rasilimali za nchi hazitakiwi kutumika kuwatetea wala kuwalinda watu hao katika kesi hizo. Kama wataamua kumtumia Wakili Kibatala litakuwa jambo jema ili pesa ibaki hapa hapa nchini.

Haitakiwi pesa na rasilimali zingine za nchi kutumika kulipia wanasheria wa ndani au nje ya nchi kwa ajili ya utetezi wa watu hawa. Ujumbe huu umfikie CAG!
Naunga mkono hoja
 
Kama hauna rekodi hizo, nini kinakufanya useme "sasa hivi angekuwa ameshakamatwa" kama unavyodai?

Tunajua Tume ya Chande ni "delaying tactic" ila ICC wanaweza kudili na wewe hata miaka 10 mbele huko. Hiyo siyo kinga. ICC haipotezi mamlaka yake kisa Rais kaunda Tume yake ya uchunguzi.
Endeleeni na ndoto zenu za mchana, hakuna wa kuwazuia kuota.

Inapokuwa imeundwa tume maana yake hao ICC waje na tume ifanye kazi na hii iliyopo.

Sheria zinaongozwa na wataalam waliobobea kwenye fani.
 
Endeleeni na ndoto zenu za mchana, hakuna wa kuwazuia kuota.

Inapokuwa imeundwa tume maana yake hao ICC waje na tume ifanye kazi na hii iliyopo.

Sheria zinaongozwa na wataalam waliobobea kwenye fani.
Ingekuwa rahisi hivyo kila mtuhumiwa angefanya hivyo. Muda utatuambia anayeota ni nani.

Natumaini hautakimbia uzi huu. Watu kama nyie huwa nakutana nao sana, baadae huwa mnapotea.
 
Isingeundwa ile tume ya Chande mpaka muda huu Samia angeshapelekwa ICC.

Makosa yaliyofanyika yanaitwa 'crime against humanity' mauaji ya binadamu, makosa yanayotendwa dunia nzima kila siku hivyo yanaruhusiwa kisheria kuundiwa tume ya Rais hata kama ni yeye anayehusika na mauaji hayo.

Ingekuwa imetendwa genocide mauaji ya halaiki, mfano SSH angekuwa kafanya uhalifu dhidi ya kabila fulani mmoja la Tanzania mpaka muda huu angeshakamatwa na kushtakiwa na kuhukumiwa.
Ulishawahi kusikia wapi mtuhumiwa anachagua mpelelezi wa kesi yake na jaji wa kusikiliza? Jisikilize kabla ya kisikilizwa! Samia ni mtuhumiwa, mama tax ni mtuhumiwa pia. Hawa wanakuwaje sehemu ya tume?
 
Ulishawahi kusikia wapi mtuhumiwa anachagua mpelelezi wa kesi yake na jaji wa kusikiliza? Jisikilize kabla ya kisikilizwa! Samia ni mtuhumiwa, mama tax ni mtuhumiwa pia. Hawa wanakuwaje sehemu ya tume?
Unaposema watuhumiwa unasahau juu ya viapo vyao. Tatizo mnaongea mkiwa na akili za wanasiasa vichwani mwenu.

Ni viongozi halali ambao walichaguliwa kwa kura halali wakala viapo halali.
 
Isingeundwa ile tume ya Chande mpaka muda huu Samia angeshapelekwa ICC.

Makosa yaliyofanyika yanaitwa 'crime against humanity' mauaji ya binadamu, makosa yanayotendwa dunia nzima kila siku hivyo yanaruhusiwa kisheria kuundiwa tume ya Rais hata kama ni yeye anayehusika na mauaji hayo.

Ingekuwa imetendwa genocide mauaji ya halaiki, mfano SSH angekuwa kafanya uhalifu dhidi ya kabila fulani mmoja la Tanzania mpaka muda huu angeshakamatwa na kushtakiwa na kuhukumiwa.
Na wewe ulisomeshwa na serikali?
Jiandae kurudisha pesa zetu fasta.
Huna ulichokielewa.
 
Back
Top Bottom