marinabahati
Member
- May 21, 2011
- 10
- 1
Nachukua fursa hii kwa niaba ya wanahabari wote kumtaka Ras Jah atuombe radhi kutokana na matusi mazito aliyotufurumushia kuwa tumenunuliwa na PPF ili tusiandike madudu yatakayofanyika huko.
Kwa kweli sikutarajia Ras Jah atoe matusi hayo kwa kuwa kwa muda mrefu amekuwa akituletea kazi mbambali ambazo pale ilipolazimu, hatukusita kuziweka hadharani. Lakini pia hatuwezi kuweka hadharani kila taarifa hususan pale taarifa anayotupa inakuwa haina ushahidi wowote wa maana.
Baada ya kukataa baadhi ya articles zake sasa ametugeukia eti kwa kuwa tumehudhuria semina ya PPF basi tumenunuliwa. Ninyi wote ni mashahidi kuwa kule Arusha tulialikwa ili kufahamishwa mambo mengi yanayohusu Mfuko wa PPF, na kuonyeshwa vitega uchumi vilivyoko Arusha.
Malipo kiduchu ya kujikimu tuliyopewa leo yanaitwa hongo. Haya ni matusi ya nguoni.
Mwaka jana tulifanyiwa semina kama hii mjini Dodoma na watu wa NSSF, hawa walitupa posho inayoeleweka, wakatupatia usafiri na bado malazi walilipia wao Dodoma Hotel, hapo pia tulihongwa ?
Jambo la kusikitisha zaidi ni kuwa Ras Jah alitufuatilia sana kule Arusha na kutupigia simu mara kwa mara akitaka kutupa taarifa ya kuibomoa PPF, lakini akagonga mwamba, ndipo akaanza visingizio vya kutushushia hadhi yetu.
Huyu Ras Jah si mgeni machoni mwa Wanahabari wengi kwa kuwa hata tulipomwona kule Arusha hatukumtilia maanani sana, kwa sababu yeye kila akikutana na Wanahabari hana jipya zaidi ya kutaka kuleta habari mbaya za kutunga zinazohusu PPF. Mara nyingi amekuwa anatumia namba 0754008840 kuwasiliana nasi.
Lakini Ras Jah ametugusa pabaya hivyo hatuna budi kumweka hadharani na yeye. Huyu jamaa ni Meneja pale PPF katika moja ya ofisi za Kanda lakini siku zote badala ya kushughulikia mambo yatakayoleta maendeleo katika shirika lake yeye anatafuta mambo ya kubomoa.
Jamaa huyuhuyu amekuwa mstari wa mbele kuwashawishi waajiriwa wa sehemu mbalimbali wasijiunge na PPF wakati yeye alitegemewa kuwashawishi wajiunge huko. Kwa bahati mbaya viongozi wa PPF hawamjui kuwa anawasaliti, laiti wangejua wasingemwacha aendeleze madudu yake.
Mambo anayoyafanya ni kama mwenye mtu mwenye kichaa, yaani amekalia tawi halafu analikata kwenye shina, hivi PPF ikianguka yeye atapona kweli ?
Uongozi wa PPF jaribuni kuwapima akili baadhi ya wafanyakazi wenu wanaofanya mambo ya ajabu..
Hili ndilo tatizo la ajira za undugu, kwa kuwa huyu Bwana aliingia PPF akitokea IST ambako alijiunga baada ya kufukuzwa Pricewaterhousecoopers. Wakati huo Mkurugenzi Mkuu alikuwa Naftali Nsemwa ambaye wanatoka kijiji kimoja. Enzi hizo huyo bwana alikuwa ndiye kila kitu, Mhasibu Mkuu na hakuna mtu aliyekuwa akikohoa. Mzee Nsemwa alijua kabisa kuwa huyu bwana ni kichaa lakini alimwajiri hivyohivyo. Halafu gia aliyoingia nayo ni kuwa alikuwa Mlokole Ee bwana eeh, usipime yeye na wenzake wengine walikuwa wakikutana kwa bwana Nsemwa kwa ajili ya maombi, ofisi ya PPF iligeuka ya wanamaombi lakini wote hawa walikuwa fake. Huku maombi, huku dhambi kibao, tuyaache hayo. Ushahidi wa yaliyokuwa yakitendeka nitayatoa live hapahapa JF.
Hata kwenye haya mambo yao ya malipo alishawahi kumlipa Mzee Nsemwa mara tatu na bado mzee huyo aliendelea kupeta kwenye mikataba mifupimifupi. Wakati huo aliona hakuna tatizo kwa kuwa mlipwaji alikuwa anatoka naye kijiji kimoja, Home Boy
Kwenye toleo lijalo nitawaletea mwenendo uliokuwepo wakati huo kati ya Ras Jah na Mzee Nsemwa ili muone kama Ras Jah anastahili kupiga vita ufisadi au la. Mtapima wenyewe.
Hivi Ras Jah kwa nini usiache kazi huko PPF ili upambane vizuri ? Kila siku unakufa na Erio na wenzake halafu bado unafanya kazi chini yao. Acha kazi.
Sasa nakupa siku saba utuombe radhi wanahabari vinginevyo nitakurusha hewani kuanzia Pricwaterhouse, IST na hapo PPF unapopachafua wakati ndio malazi yako.
Usicheze na wandishi wa habari wewe.
Kwa kweli sikutarajia Ras Jah atoe matusi hayo kwa kuwa kwa muda mrefu amekuwa akituletea kazi mbambali ambazo pale ilipolazimu, hatukusita kuziweka hadharani. Lakini pia hatuwezi kuweka hadharani kila taarifa hususan pale taarifa anayotupa inakuwa haina ushahidi wowote wa maana.
Baada ya kukataa baadhi ya articles zake sasa ametugeukia eti kwa kuwa tumehudhuria semina ya PPF basi tumenunuliwa. Ninyi wote ni mashahidi kuwa kule Arusha tulialikwa ili kufahamishwa mambo mengi yanayohusu Mfuko wa PPF, na kuonyeshwa vitega uchumi vilivyoko Arusha.
Malipo kiduchu ya kujikimu tuliyopewa leo yanaitwa hongo. Haya ni matusi ya nguoni.
Mwaka jana tulifanyiwa semina kama hii mjini Dodoma na watu wa NSSF, hawa walitupa posho inayoeleweka, wakatupatia usafiri na bado malazi walilipia wao Dodoma Hotel, hapo pia tulihongwa ?
Jambo la kusikitisha zaidi ni kuwa Ras Jah alitufuatilia sana kule Arusha na kutupigia simu mara kwa mara akitaka kutupa taarifa ya kuibomoa PPF, lakini akagonga mwamba, ndipo akaanza visingizio vya kutushushia hadhi yetu.
Huyu Ras Jah si mgeni machoni mwa Wanahabari wengi kwa kuwa hata tulipomwona kule Arusha hatukumtilia maanani sana, kwa sababu yeye kila akikutana na Wanahabari hana jipya zaidi ya kutaka kuleta habari mbaya za kutunga zinazohusu PPF. Mara nyingi amekuwa anatumia namba 0754008840 kuwasiliana nasi.
Lakini Ras Jah ametugusa pabaya hivyo hatuna budi kumweka hadharani na yeye. Huyu jamaa ni Meneja pale PPF katika moja ya ofisi za Kanda lakini siku zote badala ya kushughulikia mambo yatakayoleta maendeleo katika shirika lake yeye anatafuta mambo ya kubomoa.
Jamaa huyuhuyu amekuwa mstari wa mbele kuwashawishi waajiriwa wa sehemu mbalimbali wasijiunge na PPF wakati yeye alitegemewa kuwashawishi wajiunge huko. Kwa bahati mbaya viongozi wa PPF hawamjui kuwa anawasaliti, laiti wangejua wasingemwacha aendeleze madudu yake.
Mambo anayoyafanya ni kama mwenye mtu mwenye kichaa, yaani amekalia tawi halafu analikata kwenye shina, hivi PPF ikianguka yeye atapona kweli ?
Uongozi wa PPF jaribuni kuwapima akili baadhi ya wafanyakazi wenu wanaofanya mambo ya ajabu..
Hili ndilo tatizo la ajira za undugu, kwa kuwa huyu Bwana aliingia PPF akitokea IST ambako alijiunga baada ya kufukuzwa Pricewaterhousecoopers. Wakati huo Mkurugenzi Mkuu alikuwa Naftali Nsemwa ambaye wanatoka kijiji kimoja. Enzi hizo huyo bwana alikuwa ndiye kila kitu, Mhasibu Mkuu na hakuna mtu aliyekuwa akikohoa. Mzee Nsemwa alijua kabisa kuwa huyu bwana ni kichaa lakini alimwajiri hivyohivyo. Halafu gia aliyoingia nayo ni kuwa alikuwa Mlokole Ee bwana eeh, usipime yeye na wenzake wengine walikuwa wakikutana kwa bwana Nsemwa kwa ajili ya maombi, ofisi ya PPF iligeuka ya wanamaombi lakini wote hawa walikuwa fake. Huku maombi, huku dhambi kibao, tuyaache hayo. Ushahidi wa yaliyokuwa yakitendeka nitayatoa live hapahapa JF.
Hata kwenye haya mambo yao ya malipo alishawahi kumlipa Mzee Nsemwa mara tatu na bado mzee huyo aliendelea kupeta kwenye mikataba mifupimifupi. Wakati huo aliona hakuna tatizo kwa kuwa mlipwaji alikuwa anatoka naye kijiji kimoja, Home Boy
Kwenye toleo lijalo nitawaletea mwenendo uliokuwepo wakati huo kati ya Ras Jah na Mzee Nsemwa ili muone kama Ras Jah anastahili kupiga vita ufisadi au la. Mtapima wenyewe.
Hivi Ras Jah kwa nini usiache kazi huko PPF ili upambane vizuri ? Kila siku unakufa na Erio na wenzake halafu bado unafanya kazi chini yao. Acha kazi.
Sasa nakupa siku saba utuombe radhi wanahabari vinginevyo nitakurusha hewani kuanzia Pricwaterhouse, IST na hapo PPF unapopachafua wakati ndio malazi yako.
Usicheze na wandishi wa habari wewe.