BUMIJA
JF-Expert Member
- Oct 19, 2011
- 6,182
- 11,779
Rangi ni ulevi mwingine unaodatisha watu wengine wanapenda wanawake weupe,wengine weusi n.k.Hata unapomnunulia mpenzi wako nguo ni muhimu kutambua rangi anazopenda.Mie napenda rangi ya njano sana.
Hata kama sijapanga nikiona bidhaa ina rangi ya njano nadata.Hii Imenifanya ninunue vitu vingi na nguo kisa ni rangi niipendayo.Napenda Matunda ya mizeituni,ndizi,machungwa kisa tu ni ya njano.Nayapenda Maboga kisa tu ya njano.
Jamani Wadau rangi ni ulevi wa aina yake.Dah ama kweli rangi humfanya hata umpende kwa rangi yake.Wanawake wnajua rangi sana kuliko wanaume.Ila sijajua kua wana mapenzi na rangi kama sisi wanaume tunavopenda wasichana weupe.
Nyumba,gari,chakula kinavutia kutokana rangi.Chips zina rangi ya njano na wasichana wengi wanazipenda.Nadhani zingekua nyeusi zisingevutia machoni.Lami inavutia mana ni nyeusi,sipati picha lami iwe blue ama nyeupe,sipati picha tuwe na meno meusi,jamani rangi ziheshimiwe.
Hata kama sijapanga nikiona bidhaa ina rangi ya njano nadata.Hii Imenifanya ninunue vitu vingi na nguo kisa ni rangi niipendayo.Napenda Matunda ya mizeituni,ndizi,machungwa kisa tu ni ya njano.Nayapenda Maboga kisa tu ya njano.
Jamani Wadau rangi ni ulevi wa aina yake.Dah ama kweli rangi humfanya hata umpende kwa rangi yake.Wanawake wnajua rangi sana kuliko wanaume.Ila sijajua kua wana mapenzi na rangi kama sisi wanaume tunavopenda wasichana weupe.
Nyumba,gari,chakula kinavutia kutokana rangi.Chips zina rangi ya njano na wasichana wengi wanazipenda.Nadhani zingekua nyeusi zisingevutia machoni.Lami inavutia mana ni nyeusi,sipati picha lami iwe blue ama nyeupe,sipati picha tuwe na meno meusi,jamani rangi ziheshimiwe.