Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,005
- 9,872
Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky amezishutumu nchi za Magharibi kwa woga, wakati ambapo nchi yake inapambana kuzuia uvamizi wa Urusi.
Akilihutubia taifa jana usiku baada ya Rais wa Marekani, Joe Biden kusema hataki mabadiliko ya utawala Urusi, Zelensky amekemea kigeugeu cha nchi za Magahribi kuhusu nani na jinsi gani akabidhi ndege na silaha nyingine, huku mashambulizi ya makombora ya Urusi yakiwaua raia.
Zelensky ameomba kupewa ndege za kivita na vifaru ili aweze kujilinda kutokana na uvamizi wa Urusi. Kiongozi huyo wa Ukraine amesema nchi za Magharibi zinahitaji ujasiri zaidi katika kuisaidia Ukraine kupambana na Urusi.
Wakati huo huo, Zelensky amesema vipaumbele vyake vitakuwa uhuru na uadilifu wa eneo hilo katika duru ijayo ya mazungumzo na Urusi. Amesema uhakikisho madhubuti wa usalama ni wa lazima.
Zelensky pia amewaonya raia wa Ukraine kuhusu hatari ya kushirikiana na Urusi.
DW Swahili
Akilihutubia taifa jana usiku baada ya Rais wa Marekani, Joe Biden kusema hataki mabadiliko ya utawala Urusi, Zelensky amekemea kigeugeu cha nchi za Magahribi kuhusu nani na jinsi gani akabidhi ndege na silaha nyingine, huku mashambulizi ya makombora ya Urusi yakiwaua raia.
Zelensky ameomba kupewa ndege za kivita na vifaru ili aweze kujilinda kutokana na uvamizi wa Urusi. Kiongozi huyo wa Ukraine amesema nchi za Magharibi zinahitaji ujasiri zaidi katika kuisaidia Ukraine kupambana na Urusi.
Wakati huo huo, Zelensky amesema vipaumbele vyake vitakuwa uhuru na uadilifu wa eneo hilo katika duru ijayo ya mazungumzo na Urusi. Amesema uhakikisho madhubuti wa usalama ni wa lazima.
Zelensky pia amewaonya raia wa Ukraine kuhusu hatari ya kushirikiana na Urusi.
DW Swahili