Rais wangu una kazi kubwa sana ya kutengeneza mfumo

Omuchimati

JF-Expert Member
Aug 23, 2014
427
202
Rais wangu mpendwa naandika huu ujumbe mfupi lakini wenye maana sana kama ukiutilia maanani,nakupongeza kwa kazi kubwa unayoifanya ya kutumbua majipu na kurudisha nidhamu kwa serikali na kwa raia wa Tanzania.

Kama we mwenyewe unavyokiri ni kazi ngumu na haukutegemea utakutana na ugumu huo uliokutana nao hadi siku moja ukaamua kumshirikisha mjoli wa mwenyezi Mungu Polycarp cardinal Pengo,bila kukosea nakumbuka alipata kutamka kwenye misa moja Jumapili akakwambia ni bora mtu mmoja kuangamia kuliko kupoteza taifa zima,na akili kuwa ulimweleza ugumu unaokutana nao.

Nina ombi moja kwako,ule ugumu unaokutana nao usitamani kumwachia mtu mwingine akutane nao,ndio maana ninasema una kazi kubwa ya kutengeneza mfumo,mi sijui utautengeneza vipi kwa muono wako,lakini mi nilitamani vijana wadogo waanze kufundishwa kuipenda nchi yao toka wadogo,watu waishi maisha ambayo hayatofautiani sana.
 
Back
Top Bottom