Rais wa Gambia asema hang'atuki mamlakani ngo'

comrade igwe

JF-Expert Member
Jan 12, 2015
7,295
3,939
_93059974_yahyajammeh.jpg

Yahya Jammeh wa Gambia
Rais wa gambia Yahya Jammeh ameonya kuwa atakataa jaribio lolote la viongozi wa kieneo kumlazimisha kuondoka madarakani licha ya kushindwa katika uchaguzi na mfanyibiashara Adama Barrow.

Akihutubia wanachama wa muungano wa Bar Afrika nchini humo Bw Jammeh alisema: ''Waje wajaribu kuniondoa.wanasubiri nini? mimi ni mtu mpenda amani lakini haimaanishi kwamba sitalitetea taifa langu, kwa ujasiri na uzalendo na kuibuka mshindi''.

Amesema kuwa alikataa wito wa muungano wa viongozi wa mataifa ya Magharibi ECOWAS akiwemo rais Muhammadu Buhari wa Nigeria na Ellen Johnson Sirleaf wa Liberia kuondoka nchini Gambia.

Akiongezea: ''Wao ni kina nani wa kuniambia mimi niondoke nchini mwangu.

Amewashtumu viongozi hao kwa kuingilia a ya ndani ya Gambia.

ECOWAS tayari imesema kuwa inamtambua bw Barrow kama rais wa taifa hilo na kwamba litachukua hatua zozote kuhakikisha kuwa matokeo ya uchaguzi yanaheshimiwa.

Viongozi wa kieneo watahudhuria kuapishwa kwa Bw Barrow mnamo mwezi Januari 18 kulingana na taarifa ya Ecowas.

Rais Jammeh awali alikuwa amekubali matokeo ya uchaguzi huo manamo tarehe mosi mwezi Disemba ,lakini baadaye akaitisha uchaguzi mpya utakaoandaliwa na tume ya uchaguzi inayomcha mungu.

Alisema kwamba matokeo hayo uchaguzi yaligubikwa na dosari.

Chanzo: BBC SWAHILI
 
_93059974_yahyajammeh.jpg

Yahya Jammeh wa Gambia
Rais wa gambia Yahya Jammeh ameonya kuwa atakataa jaribio lolote la viongozi wa kieneo kumlazimisha kuondoka madarakani licha ya kushindwa katika uchaguzi na mfanyibiashara Adama Barrow.

Akihutubia wanachama wa muungano wa Bar Afrika nchini humo Bw Jammeh alisema: ''Waje wajaribu kuniondoa.wanasubiri nini? mimi ni mtu mpenda amani lakini haimaanishi kwamba sitalitetea taifa langu, kwa ujasiri na uzalendo na kuibuka mshindi''.

Amesema kuwa alikataa wito wa muungano wa viongozi wa mataifa ya Magharibi ECOWAS akiwemo rais Muhammadu Buhari wa Nigeria na Ellen Johnson Sirleaf wa Liberia kuondoka nchini Gambia.

Akiongezea: ''Wao ni kina nani wa kuniambia mimi niondoke nchini mwangu.

Amewashtumu viongozi hao kwa kuingilia a ya ndani ya Gambia.

ECOWAS tayari imesema kuwa inamtambua bw Barrow kama rais wa taifa hilo na kwamba litachukua hatua zozote kuhakikisha kuwa matokeo ya uchaguzi yanaheshimiwa.

Viongozi wa kieneo watahudhuria kuapishwa kwa Bw Barrow mnamo mwezi Januari 18 kulingana na taarifa ya Ecowas.

Rais Jammeh awali alikuwa amekubali matokeo ya uchaguzi huo manamo tarehe mosi mwezi Disemba ,lakini baadaye akaitisha uchaguzi mpya utakaoandaliwa na tume ya uchaguzi inayomcha mungu.

Alisema kwamba matokeo hayo uchaguzi yaligubikwa na dosari.

Chanzo: BBC SWAHILI
Miafrica inatia aibu sana !
 
Ile desturi yetu ya uchifu na chifu kuwa kiongozi wa maisha bado inatutafuna Afrika. Mtu ukipata uongozi unataka kifo ndo kije kikutenganishe na hayo madaraka. Itatuchukua miongo mingi na umwagaji mwingi wa damu kubadilika.
 
Maumivu ya kichwa uanza pole pole naona kuna jamaa moja pia anataka kutupeleka uko lazima tumkemee kwa nguvu zetu zote nchi inaongozwa na katiba sio matamko tu ya kila siku uku atujui ya natoka wapi
 
Jecha Salum Jecha ameonyesha mfano mbaya,sasa wanamuiga
Jecha haingii hapo huyu alipindua nchi 1994 akiwa kijana mdogo wa cheo cha chini akaongoza kijeshi baadaye akaruhusu uchaguzi naye akiacha ujeshi na kuwa raia akawa anashiinda tu ila ni MDINI sana,sasa Tume ndiyo ikatangaza kashindwa.Yaani Rais kaipinga Tume,Hapa kwetu mpinzani ndiyo kaipinga Tume.
 
Back
Top Bottom