Rais wa FIFA awasilini nchini, apokelewa na Wamasai na kuvishwa shuka

Johnny Sack

JF-Expert Member
Jan 21, 2017
8,833
18,829


fifa.jpg


Rais wa Fifa, Gianni Infantino amewasili nchini leo ambapo amepokelewa na wamasai waliokuwa wakicheza ngoma za asili pamoja na kuvishwa shuka la kimasai

=======

Dar es Salaam. Rais wa Fifa, Gianni Infantino anaongoza kikao cha siku moja kujadili masuala mbalimbali kuhusu soka la vijana na wanawake na maendeleo ya mchezo wake kwa jumla.

Mara baada ya kuwasili ukumbi hapo akiwa katika msafara wa magari manne, Infantino aliyefuatana na Rais wa CAF, Ahmad Ahmad pamoja na Rais wa TFF, Wallance Karia, Mjumbe wa CAF na mwenyekiti wa BMT, Leodegar Tenga na Kaimu Katibu wa TFF, Wilfred Kidau alivalishwa mgolole na wamasai waliokuwa akicheza ngoma nje ya ukumbi wa Mwalimu Nyerere.

Rais huyo wa FIFA baada ya kuvalishwa mgolole pamoja na Rais wa CAF, alivalishwa bangili na alipewa kirungu kiilichotengenezwa kwa kisu.

Walipoingia ndani ya jingo hilo, walipata zawadi maalumu kutoka Bodi ya Utalii Tanzania pamoja na nakala zinazozungumzia Tanzania na hifadhi zake.

Awali wajumbe kutoka nchi 19 walitangulia wakiongozwa na Katibu mkuu wa Fifa, Fatma Samoura ambaye naye alionekana kufurahia mapambo ya kimasai kwa wamasai waliokuwa wakiuza bidhaa zao.

Chanzo: Mwanaspoti
 
Sasa kaja kwenye masuala ya uchungi wa mbuzi na makondoo ya michezo? Au wamemfosi mzee wa watu kukaa kisiasa siasa?
 
Huyo rais awaulize wenzake waliotangulia kuja Tanzania.. Rooney Etoo na timu hizi Everton, Brazil Cameroon...Ukitia mguu hapa TZ unapokelewa vizuri sana kwa kuwa ni nchi ya wanamichezo
 
Back
Top Bottom