Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 39,420
- 25,440
Ndugu zangu Watanzania,
Kutokana na ushupavu, uimara na umadhubuti wa Rais samia katika kuliongoza Taifa letu unaweza kumuita jina lolote lile na likamfaa mama huyu jasiri na madhubuti. Unaweza kumwita jemedari hodari au jasiri muongoza njia au mama wa shoka au mama mchapa kazi. Vyovyote utakavyo mwita katika kuonyesha ushupavu na uimara wake kiuongozi utakuwa hujakosea hata kidogo na hakuna atakaye kushangaa hata kidogo, kwa kuwa kila mmoja hata kipofu ameona kwa kugusa makubwa ya kishujaa, kipekee ya kuigwa aliyoyafanya Rais samia ndani ya muda mfupi wa uongozi wake.
Ni kazi ya kutukuka ameifanya Rais samia, ni kazi ya kupendeza ameifanya Rais samia ni kishindo cha maendeleo kimefanywa na Rais samia, ni mipango ya ushindi imetekelezwa na Rais samia. Ni kiongozi Aliyelishika Na kuligusa Taifa kila Eneo palipohitajika mkono wake.Hateteleki wala hababaikii. Hatua zake kimaendeleo zimekuwa ni za mipango na mikakati yenye kuleta matumaini kwa watanzania.
Ni imara na madhubuti ndio maana Taifa haliyumbi wala kuyumbishwa, ndio maana Taifa limechanua kwa maendeleo, ndio maana Taifa linaendelea kukimbiliwa na wawekezaji wenye Tija kwa uchumi wa Taifa letu, ndio maana Taifa limejaa furaha katika vifua vya watanzania, ndio maana Tanzania inaongoza kwa kasi ya ukuaji wa uchumi katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.
Kazi iendelee, mama ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa,kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Kutokana na ushupavu, uimara na umadhubuti wa Rais samia katika kuliongoza Taifa letu unaweza kumuita jina lolote lile na likamfaa mama huyu jasiri na madhubuti. Unaweza kumwita jemedari hodari au jasiri muongoza njia au mama wa shoka au mama mchapa kazi. Vyovyote utakavyo mwita katika kuonyesha ushupavu na uimara wake kiuongozi utakuwa hujakosea hata kidogo na hakuna atakaye kushangaa hata kidogo, kwa kuwa kila mmoja hata kipofu ameona kwa kugusa makubwa ya kishujaa, kipekee ya kuigwa aliyoyafanya Rais samia ndani ya muda mfupi wa uongozi wake.
Ni kazi ya kutukuka ameifanya Rais samia, ni kazi ya kupendeza ameifanya Rais samia ni kishindo cha maendeleo kimefanywa na Rais samia, ni mipango ya ushindi imetekelezwa na Rais samia. Ni kiongozi Aliyelishika Na kuligusa Taifa kila Eneo palipohitajika mkono wake.Hateteleki wala hababaikii. Hatua zake kimaendeleo zimekuwa ni za mipango na mikakati yenye kuleta matumaini kwa watanzania.
Ni imara na madhubuti ndio maana Taifa haliyumbi wala kuyumbishwa, ndio maana Taifa limechanua kwa maendeleo, ndio maana Taifa linaendelea kukimbiliwa na wawekezaji wenye Tija kwa uchumi wa Taifa letu, ndio maana Taifa limejaa furaha katika vifua vya watanzania, ndio maana Tanzania inaongoza kwa kasi ya ukuaji wa uchumi katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.
Kazi iendelee, mama ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa,kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.