Rais Samia, Mawaziri wako ndio wanaokuzunguka

Rais Samia, Mawaziri wako ndio wanaokuzunguka

Jimmywatanzania

JF-Expert Member
Joined
May 8, 2015
Posts
514
Reaction score
275
Mh. Rais Samia, hakuna deal kubwa ambayo haimuhushishi waziri, kuendelea kuwaamini Mawaziri walewale ambao Wizara zao zimetajwa kwa CAG ni kuendelea kuwalea panya kwenye kabati la mkate.

Waziri anatumia muda mwingi kukupamba badala ya kutatua kero za raia. Mabango yametapakaa yakikuonesha umeondoa uhasama na kuleta maridhiano. Je, wewe Mh. Rais aliyependekeza hayo? Kama ni utashi wa Waziri, fedha ametoa wapi, kama ni wafadhili ni vyema tukawajua?

Mawaziri wako ndio wanaokuumiza, upole na udemokrasia wako wanachukulia udhaifu. Kuanza upya si vibaya futa wote uanze upya, taifa linakusubiri.
 
Mkulu vunja Bunge Futa serikali yako yooote kila mtu arudi kwao.
Agiza Mkuu wa Jeshi la Wananchi aongoze nchi kwa week moja tu.
Kaa na wenye uchungu na nchi wenye weledi wakusaidie kupanga baraza dogo la mawaziri.
Wapo unaohitaji kuwafukuza kazi bila woga wala haya… hazina afya umeme utalii habari etc

Utatushukuru baadae
 
Lakini aliwaruhusu kula kwa kiasi, labda kosa ni wanakula sana mpaka wanatoboa masufuria na kuvunja sahani.
 
Mnamuonea mama tu
Mama keshawakanya kwa hasira hawarudii Tena
Kawaambia pumbavu! Stupid! Na pepo hawataiona!
Imeisha hiyoo
Hatumuonei mama ila tunamkumbusha tu kikulacho ki nguoni mwako"
 
Mh. Rais Samia, hakuna deal kubwa ambayo haimuhushishi waziri, kuendelea kuwaamini Mawaziri walewale ambao Wizara zao zimetajwa kwa CAG ni kuendelea kuwalea panya kwenye kabati la mkate.

Waziri anatumia muda mwingi kukupamba badala ya kutatua kero za raia. Mabango yametapakaa yakikuonesha umeondoa uhasama na kuleta maridhiano. Je, wewe Mh. Rais aliyependekeza hayo? Kama ni utashi wa Waziri, fedha ametoa wapi, kama ni wafadhili ni vyema tukawajua?

Mawaziri wako ndio wanaokuumiza, upole na udemokrasia wako wanachukulia udhaifu. Kuanza upya si vibaya futa wote uanze upya, taifa linakusubiri.
Mwigulu, nape, makamba ni virusi
 
Siyo kufukuza tu filisi kabisa,au mtutajie majina ya wezi then to deal nao
 
Bashe ana unafuu kidogo, sema alikosea sana kipindi kile anabishana na Mpina, kwani mpina alikuwa sahihi na yeye alionekana mwizi na fisadi.
Ripoti ya CAG itamuumbua tu.sijui kama unakumbuka zile pikipiki boxer zaidi ya 6,000 za maafisa kilimo? bei yake halisi haijulikani.kwa ujumla vijana wake wamefeli sana.
 
Back
Top Bottom