Rais Samia kuziba masikio?

Sisi tutamuomba Mungu aliyeumba ardhi na mbingu na ndiye Mpangaji wa Kila jambo
Sasa kama Mungu ndiye mpangaji wa kila jambo hao viongozi wetu wanaofanya maamuzi ya ovyo ambapo mengine upelekea wananchi kupoteza maisha uwa wana kosa gani na kwa nini tuwalaumu?
 
Amedanganywa kadanganyika na kujifika bomu mwenyewe hapo busara ni kukaa kimya na baadae kuufuta huo mkataba wa hovyo.
 
Huna hoja ya msingi mkuu Moyo wa nchi. Hakuna anayempa mtu yoyote bandari bure.

Ukikataa kuwa sehemu ya mjadala wa bandari kwa jeuri tu bila ya sababu ya msingi, usidhani serikali itaendelea kukupigia magoti na kukuomba!. Itaendelea tu.

Kama wewe hujui chochote kinachoendelea pale bandarini ujue kuwa wapo wadau wa bandari wengi tu wanaosubiri kwa hamu hao DP waje kuwekeza.

Huko Mtwara kuna wakulima wa korosho wanaosubiri kwa hamu uwekezaji wa hawa jamaa wakiwa na matumaini na mazao yao kupata masoko ya maana huko nje.
 
Kama SI kupewa nini maana ya mkataba kutokuwa na ukomo, nini maana ya mkataba kutokuvunjwa kwa namna yeyote Ile?
 
Sasa kama Mungu ndiye mpangaji wa kila jambo hao viongozi wetu wanaofanya maamuzi ya ovyo ambapo mengine upelekea wananchi kupoteza maisha uwa wana kosa gani na kwa nini tuwalaumu?
Kiongozi yeyote anayefanya mambo ya hovyo ni lazima karma imurudie na ndio utendaji wa Mungu
 
Usimlinganishe Magu na huyu mama! Magufuli alikuwa na msimamo katika mambo yenye maslahi ya taifa! Walipiga kelele ya Bwawa la umeme akalijenga na kazi inaendelea, walipiga kelele serikali isihamie dodoma akakomaa na mpaka sasa serikali hiko dodoma, n.k.
Sasa huyu anakomaa kwa madhambi ya kuuza rasilimali za nchi ndo umlinganishe na Magufuli? It is not fair!
 
Na ndio maana nimemlinganisha kwenye jambo la bandari na makinikia ya magufuli yaani hatua alizo zichukua magufuli kwa wakosoaji wake kwenye inshu ya MAKANIKIA ndizo anazoziendea mama.
 
HISTORIA HUWA INAJIRUDIA!! MUDA UTAONGEA HATA AKISHUPAZA SHINGO KAMA MENTOR WAKE KIKWETE ANAVYOMPOTOSHA.
 
Kama SI kupewa nini maana ya mkataba kutokuwa na ukomo, nini maana ya mkataba kutokuvunjwa kwa namna yeyote Ile?
Mkataba wenye ukomo ni ule wa biashara sio ule uliopelekwa bungeni.

Bungeni pameenda IGA ambayo ni sawa na ufupisho wa nini kinakwenda kufanyika.

Consession agreements ni mikataba ya utendaji inayosainiwa kati ya mwekezaji na wazalendo, hiyo ndio ina ukomo, hiyo ndio inayokuwa na mambo yote ya pesa na mengine mengi tu ya kibiashara.

Kuna lease agreements ni mikataba ya ukodishaji ambayo DPW anakodishwa ardhi yetu atakayotumia kibiashara.

Wanasheria pori wa mjini wanapotosha mamilioni ya watu lengo lao huu uwekezaji usifanyike, lakini ni sawa na kumpiga teke chura wanamuongezea mwendo tu.
 
Yaani mlitegemea awe tofauti na wengine?
 
Kwa hiyo huu uliopelekwa mpaka bungeni hauna ukomo ln midogo itakayosainiwa itakuwa na ukomo kama hiyo kwako ni sawa basi sina haja ya kuendelea kusumbua kichwa change kujibu hoja zako mkuu
 
Kwa hiyo huu uliopelekwa mpaka bungeni hauna ukomo ln midogo itakayosainiwa itakuwa na ukomo kama hiyo kwako ni sawa basi sina haja ya kuendelea kusumbua kichwa change kujibu hoja zako mkuu
Elewa nilichokwambia kwamba kilichokwenda bungeni ni ufupisho tu wa kile kitakachosainiwa kibiashara kati ya pande mbili. Hatuhitaji kujibizana kama watoto wadogo.
 
Mama yetu raisi wa JMT anasikiliza ushauri wa wananchi wazalendo na sio wapingaji wa hovyo wanaotaka kukwamisha serikali yetu
 
Wanasiasa ni wanafiki wanatafuta millage tu Hila swala la bandari limeingiliwa na wanasiasa watafuta umaarufu na kasababisha kuonekana Lina chembechembe za udini na ubaguzi
Kwa hili wameachwa na upepo kabisa
 
Na Id yake ni Mpya huyu atakufa na kihoro cha chuki
 
Atazibuka tu!
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…