The Whistleblower
JF-Expert Member
- Dec 9, 2022
- 269
- 459
Zimetapakaa Taarifa kuwa mtandao wa X zamani Twitter utafungiwa na Serikali.
Yumkini chokochoko hizo zinatengenezwa na vijana wa UVCCM pamoja na wasaidizi wako wachache wanaopenda kukupaka mafuta kwa mgongo wa chupa ili waendelee kubakia kwenye nafasi zao.
Rais Samia,ni vyema utambue kuwa nafasi uliyonayo ni ngumu na nzito sana.
Unapokuwa kiongozi mkuu,unageuka kuwa jalala,kila mtu anatupia uchafu kwa kadri anavyojisikia.
Hakuna kiongozi asiyetukanwa Duniani,awe mwema au mwovu, sasa hao wana CCM kama wanaona mtandao wa X unakukosoa au kukutukana eti ufungiwe watakuharibia kabisa.
Utaonekana kiongozi wa hovyo anayechukia Uhuru wa Habari.
Wanataka usifiwe tu Eti usikosolewe kwani wewe umekuwa Mungu?
Kumbuka walivyokuwa wakimsifia Magufuli na baada ya kuondoka Duniani wanamzodoa sasa hivi.
Rais Samia, wewe ni mwanadamu,una mazuri yako na mabaya yako.
Epuka machawa watakupeleka pabaya sana.
Yumkini chokochoko hizo zinatengenezwa na vijana wa UVCCM pamoja na wasaidizi wako wachache wanaopenda kukupaka mafuta kwa mgongo wa chupa ili waendelee kubakia kwenye nafasi zao.
Rais Samia,ni vyema utambue kuwa nafasi uliyonayo ni ngumu na nzito sana.
Unapokuwa kiongozi mkuu,unageuka kuwa jalala,kila mtu anatupia uchafu kwa kadri anavyojisikia.
Hakuna kiongozi asiyetukanwa Duniani,awe mwema au mwovu, sasa hao wana CCM kama wanaona mtandao wa X unakukosoa au kukutukana eti ufungiwe watakuharibia kabisa.
Utaonekana kiongozi wa hovyo anayechukia Uhuru wa Habari.
Wanataka usifiwe tu Eti usikosolewe kwani wewe umekuwa Mungu?
Kumbuka walivyokuwa wakimsifia Magufuli na baada ya kuondoka Duniani wanamzodoa sasa hivi.
Rais Samia, wewe ni mwanadamu,una mazuri yako na mabaya yako.
Epuka machawa watakupeleka pabaya sana.