GE2025 Rais Samia: Hakutakuwa Na Vurugu Siku Ya Uchaguzi, Mimi Ndiyo Amiri Jeshi Mkuu

GE2025 Rais Samia: Hakutakuwa Na Vurugu Siku Ya Uchaguzi, Mimi Ndiyo Amiri Jeshi Mkuu

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
36,357
Reaction score
23,760
Ndugu zangu Watanzania,

Rais wetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan. Kwa Moyo wa Ujasiri ,kujiamini na Kwa Uhodari Mkubwa sana wa kiuongozi Amewatoa hofu watanzania wote kuwa wajitokeze kwa wingi na kufurika kwenda kupiga kura siku ya uchaguzi.

Na kwamba siku hiyo ya Uchaguzi hakutakuwa na vurugu ya aina yoyote ile, kwa sababu vyombo vya Ulinzi na Usalama vipo imara , tayari na vimejitayarisha kuwalinda watanzania na usalama wa Taifa letu.

Kwa Ujasiri Mkubwa Rais Wetu Mpendwa akatamka ya kuwa yeye ndiye Amiri Jeshi Mkuu na anawahakikishia Watanzania kutamalaki kwa amani ,utulivu na usalama Nchini. Na kwamba hicho ni kipaombele kikubwa.

Mama yetu Mpendwa ameendelea kusema ya kuwa Haitakuwa na maana ikiwa kwa sasa watajitokeza kwa wingi katika mikutano ya kampeni halafu wakajitokeza wachache kwenda kupiga kura. Rais wetu Mpendwa ametoa Rai na kuwasihi watu kwenda kupiga kura kwa wingi na kuichagua CCM ili iweze kuwaletea maendeleo na kuendelea pale ilipoishia.

Rais wetu Mpendwa amesema ya kuwa serikali ya CCM imefanya kazi kubwa sana ya kutatua kero mbalimbali ikiwepo kuunda tume mbalimbali za kushughulikia changamoto mbalimbali. Na kwamba kazi hiyo itaendelea kufanyika. Amewataka watanzania kutojihusisha na vurugu za aina yoyote ile na badala yake kulinda amani yetu ambayo ndiyo msingi wa maendeleo ya Taifa letu.
Screenshot_20250920-201129_1.jpg


Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.

c84bc876-12eb-416e-8b0c-72a802252151.jpeg

8a7c7d16-0904-43bf-bfff-ba2a2cf52644.jpeg
 
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
👇
Niliwahi kuambiwa na afisa mmoja wa juu wa vyombo vya usalama kuhusiana na huyo Abduli, kwa kweli inasikitisha na kukatisha tamaa sana. Wanasema huyo mtu ni kama ana jeshi lake binafsi linaloripoti kwake moja kwa moja. Na mipango yote inafanyika nyumbani kwake. Na nyumbani kwake kuna mifumo ya ulinzi wa ajabu aliyoyengenezewa na wachina. Na hiyo nyumva yake, ni kama bank, kuna mamilioni ya dola zimerundikwa tu. Na kuingia ni kwa sensor ya vidole vya watu wachache sana. Wengine wote kuingia huko kwake ni lazima uongozane na hao watu wake anaowaamini. Hapo nyumbani kwake ndipo mipango yote haramu ya kuwaangamiza watu, uporaji wa rasilimali za Tanganyika, ndipo hufanyika.
 
Back
Top Bottom