Rais Samia anajenga barabara ya Same - Kisiwani - Mkomazi km 97

Hizi habari ni za lini?
Katika wananchi ambao wameachwa na Serikali yao Wakati huo huo wanachangia uchumi kwa kiwango Cha juu Sana ni Same Mashariki ...Wanazalisha ndizi Sana zinazoliwa Dar, Wanazalisha Mchele, Wanazalisha Tangawizi , mahindi , maharage , Samaki, Mbuga ya wanyama ya mkomazi
Ila tangu Mwaka 1985 Serikali iliahidi kutengeneza Barabara kwa kiwango Cha lami ila Hadi Leo hamna kitu
Tulipata wabunge wahuni kama vile Chediel Mgonja,
Naghenjwa kaboyoka
Anne Kilango kidogo anaongea bungeni hata kama Serikali haitekekezi ila angalau anaongea
Ila Hawa wengine wametuchuna tu kwa kweli
Samia amewakumbuka sasa
 
Chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kazi inaendelea kwa kasi katika kila kona ya nchi,Kaskazini baada ya kusahauliwa kwa muda leo mama anawafungua kwa kasi.


Ona hii barabara ya Same – Kisiwani-Mkomazi kujengwa lami,​


Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Eng. Godfrey Kasekenya amesema Serikali iko katika hatua za mwisho za maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Same – Kisiwani-Mkomazi yenye urefu wa (KM 96.46).
Screenshot_20211122-114713.png

Akikagua maandalizi ya ujenzi wa barabara hiyo Eng. Kasekenya amesema awamu ya kwanza ya ujenzi huo itahusisha KM 11.9 ambapo ujenzi utaanzia sehemu ya Mroyo – Ndungu hadi Kihurio.
Screenshot_20211122-114742.png

Barabara hiyo ambayo inapita pembezoni mwa hifadhi ya taifa ya Mkomazi itachochea na kurahisisha huduma za usafiri na uchukuzi, kilimo, utalii na biashara kwa wakazi wa tarafa za Gonja, Ndungu, Kihurio, Bendera na Mkomazi wilayani Same na hivyo kukuza uchumi wa wakazi hao.

“Tumejipanga kuijenga barabara hii kwa lami na kuhakikisha inakamilika kwa wakati na ubora uliokusudiwa”, amesisitiza Naibu Waziri Kasekenya.
Screenshot_20211122-114727.png

Aidha amekagua ujenzi wa madaraja ya Mamba na Yongoma ambayo ujenzi wake umekamilika katika barabara ya Mwembe-Myamba-Ndungu na kuzungumzia umuhimu wa wananchi kulinda miundombinu hiyo ili itumike wakati wote wa mwaka.
Screenshot_20211122-114511.png


Naye Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), Mkoa wa Kilimanjaro Eng. Motta Kyando amesema ujenzi wa madaraja na makalvati katika barabara ya Mwembe hadi Ndungu ni zoezi endelevu hivyo kuwataka wananchi kuepuka kulima karibu na hifadhi ya barabara ili kuepuka mmomonyoko wa udongo.

Naye Mbunge wa Same Mashariki Mhe. Anne Kilango Malechela amesema ujenzi wa barabara ya Same-Kisiwani-Mkomazi (KM 96.46), na Mwembe-Myamba-Ndungu (KM 90.19), ukikamilika utafungua uchumi wa wakazi wa wilaya ya Same ambao kwa kiasi kikubwa unategemea shughuli za kilimo cha mazao ya tangawizi na ndizi na kuhuisha utalii katika hifadhi ya taifa ya Mkomazi.
Kazi ya Rais Samia inavutia sanaa
 
Kama mambo ndio haya basi Tanzania kama kuna wakati tumepata Rais bora na wa kweli nadhani ni sasa,Tufanye kazi kwa bidii sana,

Hakika huyu Mama ni Mpango wa Mungu,

#WATANZANIA TUFANYE KAZI KWA BIDII
 
" Kwa mwendo huu Tanzania tutafika tunakotaka kwenda tena kwa kuwahi sana, Hongera Mama Samia, Watanzania tuko nyuma yako We chapa kazi achana na Wasio na jema "
 
Hii ya RAIS SAMIA atoa Hela si sahii, ilikuwa staili ya mwendazake, mseme Serikali yatoa sh kadhaa
 
Chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kazi inaendelea kwa kasi katika kila kona ya nchi,Kaskazini baada ya kusahauliwa kwa muda leo mama anawafungua kwa kasi.


Ona hii barabara ya Same – Kisiwani-Mkomazi kujengwa lami,​


Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Eng. Godfrey Kasekenya amesema Serikali iko katika hatua za mwisho za maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Same – Kisiwani-Mkomazi yenye urefu wa (KM 96.46).
Screenshot_20211122-114713.png

Akikagua maandalizi ya ujenzi wa barabara hiyo Eng. Kasekenya amesema awamu ya kwanza ya ujenzi huo itahusisha KM 11.9 ambapo ujenzi utaanzia sehemu ya Mroyo – Ndungu hadi Kihurio.
Screenshot_20211122-114742.png

Barabara hiyo ambayo inapita pembezoni mwa hifadhi ya taifa ya Mkomazi itachochea na kurahisisha huduma za usafiri na uchukuzi, kilimo, utalii na biashara kwa wakazi wa tarafa za Gonja, Ndungu, Kihurio, Bendera na Mkomazi wilayani Same na hivyo kukuza uchumi wa wakazi hao.

“Tumejipanga kuijenga barabara hii kwa lami na kuhakikisha inakamilika kwa wakati na ubora uliokusudiwa”, amesisitiza Naibu Waziri Kasekenya.
Screenshot_20211122-114727.png

Aidha amekagua ujenzi wa madaraja ya Mamba na Yongoma ambayo ujenzi wake umekamilika katika barabara ya Mwembe-Myamba-Ndungu na kuzungumzia umuhimu wa wananchi kulinda miundombinu hiyo ili itumike wakati wote wa mwaka.
Screenshot_20211122-114511.png


Naye Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), Mkoa wa Kilimanjaro Eng. Motta Kyando amesema ujenzi wa madaraja na makalvati katika barabara ya Mwembe hadi Ndungu ni zoezi endelevu hivyo kuwataka wananchi kuepuka kulima karibu na hifadhi ya barabara ili kuepuka mmomonyoko wa udongo.

Naye Mbunge wa Same Mashariki Mhe. Anne Kilango Malechela amesema ujenzi wa barabara ya Same-Kisiwani-Mkomazi (KM 96.46), na Mwembe-Myamba-Ndungu (KM 90.19), ukikamilika utafungua uchumi wa wakazi wa wilaya ya Same ambao kwa kiasi kikubwa unategemea shughuli za kilimo cha mazao ya tangawizi na ndizi na kuhuisha utalii katika hifadhi ya taifa ya Mkomazi.
Kazi iendelee
 
Ungeniambia Barbara ya kongwa to mpwapwa... Au Chipogoro to kibakwe... Au hata NAKO to kiteto mpaka babati kupitia simanjiro zinawekwa lami ningekuelewa. Coz Hawa raia wa haya maeneo Toka uhuru upatikane hawaajawahi kuniona lami. Kweli unakuja n stori za kaskazini ambao wapo km milion kumi Kwa maendeleo ya kimiundombinu kwelii??????? Ndio maana NDUGAI Akasema wagogo wanachukiwa
Daaah
 
Miradi yote iliyoachwa na Hayati Dkt John John Joseph Pombe Magufuli Rais Samia Suluhu Hassan anaitekeleza kwa 100%

Sihiyo tu tayari mingine mipya inaendelea na Ujenzi,

Tunawajibu wa kumwombea Mama huyu,

Sema serikali inajenga acha ufala kwani samia ndio anatoa mfuko pesa au kodi zetu?
 
Chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kazi inaendelea kwa kasi katika kila kona ya nchi,Kaskazini baada ya kusahauliwa kwa muda leo mama anawafungua kwa kasi.


Ona hii barabara ya Same – Kisiwani-Mkomazi kujengwa lami,​


Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Eng. Godfrey Kasekenya amesema Serikali iko katika hatua za mwisho za maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Same – Kisiwani-Mkomazi yenye urefu wa (KM 96.46).
Screenshot_20211122-114713.png

Akikagua maandalizi ya ujenzi wa barabara hiyo Eng. Kasekenya amesema awamu ya kwanza ya ujenzi huo itahusisha KM 11.9 ambapo ujenzi utaanzia sehemu ya Mroyo – Ndungu hadi Kihurio.
Screenshot_20211122-114742.png

Barabara hiyo ambayo inapita pembezoni mwa hifadhi ya taifa ya Mkomazi itachochea na kurahisisha huduma za usafiri na uchukuzi, kilimo, utalii na biashara kwa wakazi wa tarafa za Gonja, Ndungu, Kihurio, Bendera na Mkomazi wilayani Same na hivyo kukuza uchumi wa wakazi hao.

“Tumejipanga kuijenga barabara hii kwa lami na kuhakikisha inakamilika kwa wakati na ubora uliokusudiwa”, amesisitiza Naibu Waziri Kasekenya.
Screenshot_20211122-114727.png

Aidha amekagua ujenzi wa madaraja ya Mamba na Yongoma ambayo ujenzi wake umekamilika katika barabara ya Mwembe-Myamba-Ndungu na kuzungumzia umuhimu wa wananchi kulinda miundombinu hiyo ili itumike wakati wote wa mwaka.
Screenshot_20211122-114511.png


Naye Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), Mkoa wa Kilimanjaro Eng. Motta Kyando amesema ujenzi wa madaraja na makalvati katika barabara ya Mwembe hadi Ndungu ni zoezi endelevu hivyo kuwataka wananchi kuepuka kulima karibu na hifadhi ya barabara ili kuepuka mmomonyoko wa udongo.

Naye Mbunge wa Same Mashariki Mhe. Anne Kilango Malechela amesema ujenzi wa barabara ya Same-Kisiwani-Mkomazi (KM 96.46), na Mwembe-Myamba-Ndungu (KM 90.19), ukikamilika utafungua uchumi wa wakazi wa wilaya ya Same ambao kwa kiasi kikubwa unategemea shughuli za kilimo cha mazao ya tangawizi na ndizi na kuhuisha utalii katika hifadhi ya taifa ya Mkomazi.
Nyumbani
 
Back
Top Bottom