Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 36,356
- 23,760
Ndugu zangu Watanzania,
Rais wetu mpendwa na jemedari wetu kipenzi cha Watanzania, Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hassan — mama wa shoka, chuma cha reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita, nyota ya matumaini, na nuru ya wanyonge.
Ameonyesha kujawa na ucha Mungu, hofu ya Mungu, na kutenda haki katika uteuzi wa wagombea ubunge. Ameongoza mchakato mgumu wa kuwapata wagombea ubunge, lakini ametenda haki na haki imeonekana kutendeka. Jambo ambalo limeondoa kabisa malalamiko, manung’uniko, na lawama kutoka kwa wagombea na wanachama.
Ambapo hata wale ambao hawakupata nafasi ya kupenya kwenye tatu bora katika ngazi ya wilaya na mkoa, sasa wamejikuta wametendewa haki na majina yao kurejeshwa kwa ajili ya kupigiwa kura na wajumbe katika mkutano mkuu wa jimbo.
Kwa hakika jambo hilo limekijenga, kukiimarisha, na kukiacha chama kikiwa na umoja na mshikamano wa hali ya juu sana. Kwa sababu kila mwanachama ameridhika kabisa na mchakato ulivyokwenda pamoja na maamuzi ya Kamati Kuu iliyoongozwa na Rais Samia katika uteuzi wa wagombea.
Rais Samia anaendelea kuonyesha kuwa yeye ni zaidi ya kiongozi — ni kiongozi na nusu. Amehakikisha rushwa haichukui nafasi wala kuwa mwamuzi wa maamuzi ya kupendekeza wagombea. Kwa sababu anajua wagombea wakipita na kupitishwa kwa nguvu ya rushwa au pesa chafu, itaangamiza na kukigawa chama na kukiacha na makovu makubwa sana. Hii ndiyo sababu alihakikisha mchakato unakuwa wa haki na wagombea wote wanatendewa haki.
Watanzania tuna kila sababu ya kwenda kutiki kwa Rais Samia na wagombea wote wa CCM katika uchaguzi ujao.
Kazi iendelee. Mama ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya Watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa: Mama anatosha kuendelea kuliongoza taifa letu kwa muhula wa pili.
Rais wetu mpendwa na jemedari wetu kipenzi cha Watanzania, Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hassan — mama wa shoka, chuma cha reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita, nyota ya matumaini, na nuru ya wanyonge.
Ameonyesha kujawa na ucha Mungu, hofu ya Mungu, na kutenda haki katika uteuzi wa wagombea ubunge. Ameongoza mchakato mgumu wa kuwapata wagombea ubunge, lakini ametenda haki na haki imeonekana kutendeka. Jambo ambalo limeondoa kabisa malalamiko, manung’uniko, na lawama kutoka kwa wagombea na wanachama.
Ambapo hata wale ambao hawakupata nafasi ya kupenya kwenye tatu bora katika ngazi ya wilaya na mkoa, sasa wamejikuta wametendewa haki na majina yao kurejeshwa kwa ajili ya kupigiwa kura na wajumbe katika mkutano mkuu wa jimbo.
Kwa hakika jambo hilo limekijenga, kukiimarisha, na kukiacha chama kikiwa na umoja na mshikamano wa hali ya juu sana. Kwa sababu kila mwanachama ameridhika kabisa na mchakato ulivyokwenda pamoja na maamuzi ya Kamati Kuu iliyoongozwa na Rais Samia katika uteuzi wa wagombea.
Rais Samia anaendelea kuonyesha kuwa yeye ni zaidi ya kiongozi — ni kiongozi na nusu. Amehakikisha rushwa haichukui nafasi wala kuwa mwamuzi wa maamuzi ya kupendekeza wagombea. Kwa sababu anajua wagombea wakipita na kupitishwa kwa nguvu ya rushwa au pesa chafu, itaangamiza na kukigawa chama na kukiacha na makovu makubwa sana. Hii ndiyo sababu alihakikisha mchakato unakuwa wa haki na wagombea wote wanatendewa haki.
Watanzania tuna kila sababu ya kwenda kutiki kwa Rais Samia na wagombea wote wa CCM katika uchaguzi ujao.
Kazi iendelee. Mama ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya Watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa: Mama anatosha kuendelea kuliongoza taifa letu kwa muhula wa pili.