Rais Samia aitisha mkutano wa dharura wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
15,305
9,734
Ndugu zangu Watanzania,

Habari ambayo inaendelea kusambaa kwa kasi ya upepo na kuteka hisia za watu na ambayo imeandikwa na kuripotiwa na Gazeti la Mwananchi inaeleza ya kuwa Rais Samia ameitisha mkutano wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa kwa Dharura. Habari hiyo ambayo imeendelea kuvuma kila kona na kuteka anga la siasa imeleta msisimko wa kipekee huku kila mmoja akitamani kujuwa nini kitajili katika mkutano huo.

Ikumbukwe ya kuwa hicho ni kikao cha juu kabisa kinachowakutanisha wajumbe wa juu na wazito kwelikweli, kimesheheni watu ambao wakizungumza ni lazima nchi itetemeke na kusimama kwa shughuli zote.ni mkutano ambao ukiitishwa ni lazima vyombo vyote vikubwa kutoka kila kona ya Dunia vitume wawakilishi wake katika viunga ambako mkutano huo utafanyika. Kwa kuwa kikao hicho hutoa muelekeo wa nchi na mambo mazito yagusayo nchi na maslahi yake.

Tukae kwa kutulia maana Hicho ni kikao kizito chenye mambo mazito. Endeleeni kuwa watulivu na subira ili kujua nini mama Wa Taifa ,shujaa wa Afrika,jasiri muongoza njia na chuma cha Reli Mama Samia Suluhu Hasssan anakwenda kuzungumza na kwanini Ameitisha kwa dharura.Hiyo ndiyo CCM Ambayo Mambo yake ni lazima yaitetemeshe nchi na kuteka mioyo ya watanzania.Na kila kikao cha CCM huja na matumaini kwa watanzania.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
 
Back
Top Bottom