Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,436
- 5,234
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan ameahidi kukamilisha ujenzi wa bandari kavu yenye ukubwa wa ekari 1800 katika eneo la Katenjele lililopo Tunduma mkoani Songwe.
Dkt. Samia amesema bandari hiyo itaondoa changamoto ya malori kupaki muda mrefu barabarani yakiwa yanaelekea Tunduma mpakani mwa Tanzania na Zambia.
Dkt. Samia amesema hayo leo Septemba 03, 2025 wakati akinadi sera za CCM kwa wananchi wa mkoa wa Songwe, ikiwa ni mwendelezo wa mikutano ya kampeni za chama hicho.
Dkt. Samia amesema bandari hiyo itaondoa changamoto ya malori kupaki muda mrefu barabarani yakiwa yanaelekea Tunduma mpakani mwa Tanzania na Zambia.
Dkt. Samia amesema hayo leo Septemba 03, 2025 wakati akinadi sera za CCM kwa wananchi wa mkoa wa Songwe, ikiwa ni mwendelezo wa mikutano ya kampeni za chama hicho.