Rais Mwinyi nchini Zanzibar, Mkapa nchini Burundi, Kikwete nchini Libya!

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,975
Tanzania imeendelea kutambulika katika uso wa Afrika na Duniani kote!

Tutakumbuka kuwa Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi aliteuliwa kuwa Kiongozi wa Waangalizi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwenye Uchaguzi Mkuu wa Uganda ambao umemaliza majuzi. Na ninaamini kama isingekuwa umri wake, kwa sasa angekuwa kwenye majukwaa ya kimataifa kama msuluhishi wa migogoro ya kisiasa kama alivyokuwa anafanya katika mgogoro wa Zanzibar.

Marais wa Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya kuangaza huku na kule, wamemuona Mzee Mkapa anafaa sana kuwa msuluhishi wa kisiasa nchini Burundi.

Ikumbukwe pia viongozi wakuu wa Afrika waliangaza Afrika yote na kumuona Mzee Kikwete. Februari mosi, mwaka huu walitutangazia kuwa Rais (mstaafu) Jakaya Kikwete, ameteuliwa na Umoja wa Afrika (AU) kuwa mwakilishi wake katika kusuluhisha mgogoro wa Libya.

Hata kwenye mgogoro wa Kenya, Mzee Mkapa na Kikwete walifanya kazi ya ziada mpaka Rais Mwai Kibaki na kiongozi wa upinzani Raila Odinga wakatia saini makubaliano ya kugawana madaraka na hivyo kumaliza mzozo wa kisiasa uliozuka baada ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi wa rais mwezi Desemba mwaka 2007.

Hii ni heshima kwa taifa na pia ni kigezo katika feedback/taswira kuhusu mtazamo wa mataifa mengine kuhusu uwezo wa Tanzania na viongozi wake katika majukwaa ya usuluhishi wa kisiasa.

Alichokianzisha Mwl. Nyerere katika majukwaa ya siasa za kimataifa, Marais waliofuata wanakiendeleza...
 
Mzee Lowassa Nae Viongozi wa Makanisa ya Kilokole walikutana Lubumbashi Congo wakamtunuku Tuzo ya Amani. Tanzania kweli ni msitu wa Vipaji.
 
Ma-think tanks kutoka Tanzania. Hakika ni fahari kwa watanzania kwa viongozi wetu kuonekana lulu Africa. Pia ni fahari kwa ccm kwani imesheheni hazina zinazotambulika kimataifa. Hawana uhuni wa kubadili gia angani hawa.
 
Siku dunia itafaham unafiki wa hawa watu itakuwa too late.

Niukweli uliowazi Mwl Julius K. Nyerere aliiweka vema Tanzania kwenye raman ya dunia ....wanavuna kazi ya Nyerere.

wenyewe ni hawa nimajanga tu

Mwinyi
mwandishi katabaro wa mbuga ya loliondo

mkapa
Mauwaji ya zanzibar na watu kukimbilia shimoni

mwembe chai waislam walipigwa shaba nk

Mgogoro wa zanzibar hivi sasa nk

kikwete
mauwaji ya
Daudi mwangosi
Ali zona
Dr Sengodo Mvungi
Soweto Arusha
stendi ya basi Arusha
nk

Hapa kwao yamewashinda na ccm yao

-wezi wa kura

-kuminya demokrasia

-kutesa wapinzani

-kupiga raia mabomu nakwasweka vizuizin hovyohovyo

-kulazimisha madaraka nk

ccm ni mnyama wa hovyo hajapata kutokea popote dunia hii.....nje kajivika ngozi ya kondoo ilhali ndani ni fisi maji na muuwaji mkuu.
 
Tanzania imeendelea kutambulika katika uso wa Afrika na Duniani kote!

Tutakumbuka kuwa Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi aliteuliwa kuwa Kiongozi wa Waangalizi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwenye Uchaguzi Mkuu wa Uganda ambao umemaliza majuzi. Na ninaamini kama isingekuwa umri wake, kwa sasa angekuwa kwenye majukwaa ya kimataifa kama msuluhishi wa migogoro ya kisiasa kama alivyokuwa anafanya katika mgogoro wa Zanzibar.

Marais wa Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya kuangaza huku na kule, wamemuona Mzee Mkapa anafaa sana kuwa msuluhishi wa kisiasa nchini Burundi.

Ikumbukwe pia viongozi wakuu wa Afrika waliangaza Afrika yote na kumuona Mzee Kikwete. Februari mosi, mwaka huu walitutangazia kuwa Rais (mstaafu) Jakaya Kikwete, ameteuliwa na Umoja wa Afrika (AU) kuwa mwakilishi wake katika kusuluhisha mgogoro wa Libya.

Hata kwenye mgogoro wa Kenya, Mzee Mkapa na Kikwete walifanya kazi ya ziada mpaka Rais Mwai Kibaki na kiongozi wa upinzani Raila Odinga wakatia saini makubaliano ya kugawana madaraka na hivyo kumaliza mzozo wa kisiasa uliozuka baada ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi wa rais mwezi Desemba mwaka 2007.

Hii ni heshima kwa taifa na pia ni kigezo katika feedback/taswira kuhusu mtazamo wa mataifa mengine kuhusu uwezo wa Tanzania na viongozi wake katika majukwaa ya usuluhishi wa kisiasa.

Alichokianzisha Mwl. Nyerere katika majukwaa ya siasa za kimataifa, Marais waliofuata wanakiendeleza...
"Marais wa Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya kuangaza huku na kule, wamemuona Mzee Mkapa anafaa sana kuwa msuluhishi wa kisiasa nchini Burundi"

Hapa ndipo ninapotamani TRUMP, mgombea urais wa USA kupitia Republican ninavyoomba apate ridhaa ya wamerekani kuliongoza taifa hilo na dunia. Maneno yake haya kwenda kombo aliposema Afrika ina hitaji kutawaliwa tena na akiwa Rais atawashughulikia marais vin'gan'gamizi.

Haingilii akilini Rais mstaaafu Mkapa ametoka kapa kwa kushindwa kuleta suluhu nchi yake mwenyewe na akaamua ku- " take side" halafu leo anaonekana kuwa anafaa kuwa msuluhishi.

Aidha wakati mikono yake na macho yake yamekaukiana damu ya wazanzibari walio " fyokozeka" chini ya utawala wake leo anapewa dhamana ya kuepusha damu isimwagike. Kichekesho
 
Tanzania imeendelea kutambulika katika uso wa Afrika na Duniani kote!

Tutakumbuka kuwa Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi aliteuliwa kuwa Kiongozi wa Waangalizi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwenye Uchaguzi Mkuu wa Uganda ambao umemaliza majuzi. Na ninaamini kama isingekuwa umri wake, kwa sasa angekuwa kwenye majukwaa ya kimataifa kama msuluhishi wa migogoro ya kisiasa kama alivyokuwa anafanya katika mgogoro wa Zanzibar.

Marais wa Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya kuangaza huku na kule, wamemuona Mzee Mkapa anafaa sana kuwa msuluhishi wa kisiasa nchini Burundi.

Ikumbukwe pia viongozi wakuu wa Afrika waliangaza Afrika yote na kumuona Mzee Kikwete. Februari mosi, mwaka huu walitutangazia kuwa Rais (mstaafu) Jakaya Kikwete, ameteuliwa na Umoja wa Afrika (AU) kuwa mwakilishi wake katika kusuluhisha mgogoro wa Libya.

Hata kwenye mgogoro wa Kenya, Mzee Mkapa na Kikwete walifanya kazi ya ziada mpaka Rais Mwai Kibaki na kiongozi wa upinzani Raila Odinga wakatia saini makubaliano ya kugawana madaraka na hivyo kumaliza mzozo wa kisiasa uliozuka baada ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi wa rais mwezi Desemba mwaka 2007.

Hii ni heshima kwa taifa na pia ni kigezo katika feedback/taswira kuhusu mtazamo wa mataifa mengine kuhusu uwezo wa Tanzania na viongozi wake katika majukwaa ya usuluhishi wa kisiasa.

Alichokianzisha Mwl. Nyerere katika majukwaa ya siasa za kimataifa, Marais waliofuata wanakiendeleza...
Amani ya Africa Kwanza, Tunawatakia kila la kheri katika majukumu na jitihada za kuhakikisha inapatikana Amani Barani Africa.
 
Ukimiliki Binti Hamdan Meghji shombe shombe ya Kiarabu na Kihindi yenye figure ya waarabu wa Mtendeni Tabora( chini ya mgongo kama wana TV ya Chogo) kuna haja ya Waarabu wa Vitani!

Tanzania hakuna Miarabu, Muarabu wa hapa ni ngozi tuu Roho ni ya kinyamwezi, ni tofauti sana Na kule kwenye mitende.
 
Back
Top Bottom