Waberoya
Platinum Member
- Aug 3, 2008
- 15,169
- 10,785
Eee Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na nchi. Pokea heshima na utukufu, tunaliinua jina na enzi yako ya milele yote.
Asante kwa uchaguzi mkuu wa Tanzania ambao umepita salama bila machafuko yoyote. Asnte kwa kutupa Rais mpya kabisa katika historia ya Tanzania. Asante kwa kutupa Slaa.
Mungu huwa unatangaza mwisho kutoka mwanzo na umesema tukiwa na Imani kama chembe ya haladali tunaweza kuamsha milima. Kwetu sisi CCM ni mlima na kwa imani tumeingusha. Umesema pia Imani ni hakika ya mambo yatarijiwayo ni bayana yasiyoonekana. Ndio maana kwa imani nimeona Slaa ni rais ni nitaishi nikiamini kuwa ni rais.
Najua uchaguzi bado kufanya, lakini katika imani mambo mawili nimekueleza kuwa utakuwa wa amani nay a kuwa Slaa ni rais. Ninakushukuru Mungu wewe ufanyaje miujiza, ufanyaye njia pasipo na njia.
Hata kama hali zote zinaonyesha CCM kupendelewana NEC, naomba ashikwe na kigugumizi mtangaza matokeo hata kama akipanga kumtangaza Yule mtu washindwe watangaze jina la Slaa. Mungu umefanya na unafanya miujiza kila siku. Siku ya 31 ya mwezi huu nayo umeshafanya miujiza.
Mungu mlinde Mh.Slaa katika urais wake ,mpe nguvu na hekima ya kuongoza nchi hii.Mpe uweza wa kuwatumikia watanzania kwa uwezo wake akili zake zote. Mpe afya yeye na viongozi wote wa serikali.
Linda umoja wa watanzania,linda amani , linda kila zuri la watanzania. Tupe moyo wa kukubali matokeo, wafariji CCM kwa kushindwa, wape nguvu ya kukubali na kuitoa nchi kwa Rais mpya.
Msaidie rais wa zamani Kikwete yeye na familia yake, wape umoja na amani ndani ya nyumba yao ili isivunjike kwa kutafutana wabaya. wape hekima ya kujua wabaya sio CCM ni wakati tu na mambo yake.
Ninaomba haya nikiamini
Amen.
Asante kwa uchaguzi mkuu wa Tanzania ambao umepita salama bila machafuko yoyote. Asnte kwa kutupa Rais mpya kabisa katika historia ya Tanzania. Asante kwa kutupa Slaa.
Mungu huwa unatangaza mwisho kutoka mwanzo na umesema tukiwa na Imani kama chembe ya haladali tunaweza kuamsha milima. Kwetu sisi CCM ni mlima na kwa imani tumeingusha. Umesema pia Imani ni hakika ya mambo yatarijiwayo ni bayana yasiyoonekana. Ndio maana kwa imani nimeona Slaa ni rais ni nitaishi nikiamini kuwa ni rais.
Najua uchaguzi bado kufanya, lakini katika imani mambo mawili nimekueleza kuwa utakuwa wa amani nay a kuwa Slaa ni rais. Ninakushukuru Mungu wewe ufanyaje miujiza, ufanyaye njia pasipo na njia.
Hata kama hali zote zinaonyesha CCM kupendelewana NEC, naomba ashikwe na kigugumizi mtangaza matokeo hata kama akipanga kumtangaza Yule mtu washindwe watangaze jina la Slaa. Mungu umefanya na unafanya miujiza kila siku. Siku ya 31 ya mwezi huu nayo umeshafanya miujiza.
Mungu mlinde Mh.Slaa katika urais wake ,mpe nguvu na hekima ya kuongoza nchi hii.Mpe uweza wa kuwatumikia watanzania kwa uwezo wake akili zake zote. Mpe afya yeye na viongozi wote wa serikali.
Linda umoja wa watanzania,linda amani , linda kila zuri la watanzania. Tupe moyo wa kukubali matokeo, wafariji CCM kwa kushindwa, wape nguvu ya kukubali na kuitoa nchi kwa Rais mpya.
Msaidie rais wa zamani Kikwete yeye na familia yake, wape umoja na amani ndani ya nyumba yao ili isivunjike kwa kutafutana wabaya. wape hekima ya kujua wabaya sio CCM ni wakati tu na mambo yake.
Ninaomba haya nikiamini
Amen.