Omuchimati
JF-Expert Member
- Aug 23, 2014
- 427
- 202
Salamu nyingi zikufikie Rais wangu mpendwa John Joseph Pombe Magufuli, nakupongeza sana kwa namna unavyoendesha mapambano ya kiuchumi na ya kimfumo vilevile, ni miaka mingi ilipita katika bara la Africa kumpata Rais mwenye hulka na tabia kama yako, Watanzania si budi kumshukuru MUNGU kwa kutupatia Rais wa namna yako, MUNGU AZIDI KUKUWEZESHA NA KUKUPA UJASIRI ZAIDI WA KUSONGA MBELE.
Rais wangu mpendwa unapopambana na mifumo mibaya ndani ya nchi yetu nakuomba kwa moyo wa dhati na kwa unyenyekevu usivisahau vyombo vya dola, hawa ni wanao ambao wanaishi maisha ya hatari kila uchao, wanahangaika kuiweka nchi hii salama masaa 24 ndani ya mwaka mzima, angalia posho zao, angalia hali ya maisha yao, nitaanza kuelezea moja baada ya nyingine:
JESHI LA POLISI: Jeshi la polisi limekuwa mstari wa mbele katika kulinda raia pamoja na mali zao, nalipa heko Jeshi hili kwa kazi nzuri wanazofanya kila kukicha katika nchi yetu , nadhani hawa ndio watumishi wa umma wanaowahi kuamka mapema na wanakuwa wa mwisho pia kulala, Amiri Jeshi wangu Mkuu Joseph Magufuli, vijana hawa licha ya kuanza kuwaboroshea mazingira yao ambayo yalikuwa taaabani, bado una kazi kubwa ya kuimarisha maisha yao haswa upande wa makazi, wengi bado wanaishi kwenye nyumba ambazo ni duni kulingana na mazingira ya kazi yao wanaendelea kupata msongo wa maisha kutokana na mazingira yao, imarisha posho sana haswa ukizingatia shughuli yao ni ya masaa ishirini na nne, ni shughuli yenye kuhitaji uzalendo wa hali ya juuu na weledi usiokuwa na mipaka, ukisha yafanya haya kwa hawa vijana wako Rais wangu mpendwa mulika mfumo mzima wa Jeshi la polisi katika kupandisha vyeo na upewaji wa Promotion, kwa weledi wanagu mdogo nilionao huwa naaamini kabisa upandishwaji cheo wa kazi za medani haswa hizi za kijeshi hutegemea sana utendaji kazi wako katika ulingo wa medani hyo, pia imarisha vifaa, yakiwemo mavazi na vitendea kazi, nayaleta kwako haya Rais wangu sio kwamba we ndie mwenye kuyatendea kazi unao wasaidizi wazuri kabisa katika Jeshi hili wakipewa mwongozo wanaweza kuyasimamia kwa umakini kabisa.
JESHI LA WANANCHI TANZANIA, hawa ndio walinda mipaka yetu na nchi kwa ujumla, wnafanya kazi yao vizuri kwa sababu hadi sasa nchi yetu ipo shwari kabisa,kilio chao sio tofauti kabisa na Jeshi la polisi yale niliyosema awali hap juu yazingatiwe kabisa, lakini ningependa kushauri licha tu ya kuwa walinzi wa mipaka yetu, ningefurahi kuona Jeshi hili linaongezewa majukumu ya kufanya, isiwe tu wakati wa dharura na majanga, haswa nilifurahishwa na jambo ambalo walilofanya majuzi la kuanza kusambaza vifaa vya mahabara mashuleni, naamini kulitumia Jeshi hili Zaidi ya hapo, sababu miongoni mwao wamejaa wazalendo, nch hiii ya Tanzania tutapiga hatua Zaidi mbele.
Baaada ya kueleza kwa ufupi kuhusu majeshi hayo hapa Tanzania, kuna Jeshi la magereza, paia ambalo mahitaji yake sio tofauti sana na mahitaji ya majeshi mengine, kuna Jeshi pia ambalo ni moyo wa nchi TISS,Mhe Rais angalia upya sharia zilizounda TISS, je zinaendana na wakati tulionao? Je zinawapa nguvu hawa vijana wako kufanya kazi pasipo kuwa na shaka? nakuomba itazame sheria hiii na kwa muongozo wako naamini kabisa kuna jambo linaweza kufanyika.
Nimeandika haya yote MHE, Rais John Pombe Magufuli, sababu unapoimarisha mfumo , mfumo huu utaimarika kwa kuviiiamarisha vyombo vya dola, ambavyo ndilo jicho la nchi yetu, pia nakupongeza sana kwa ujasiri ulionao wa kuonyesha madhaifu yalioifikisha nchi hii hapa tulipo, hakika ni ujasiri wa hali ya juu.
Rais wangu mpendwa unapopambana na mifumo mibaya ndani ya nchi yetu nakuomba kwa moyo wa dhati na kwa unyenyekevu usivisahau vyombo vya dola, hawa ni wanao ambao wanaishi maisha ya hatari kila uchao, wanahangaika kuiweka nchi hii salama masaa 24 ndani ya mwaka mzima, angalia posho zao, angalia hali ya maisha yao, nitaanza kuelezea moja baada ya nyingine:
JESHI LA POLISI: Jeshi la polisi limekuwa mstari wa mbele katika kulinda raia pamoja na mali zao, nalipa heko Jeshi hili kwa kazi nzuri wanazofanya kila kukicha katika nchi yetu , nadhani hawa ndio watumishi wa umma wanaowahi kuamka mapema na wanakuwa wa mwisho pia kulala, Amiri Jeshi wangu Mkuu Joseph Magufuli, vijana hawa licha ya kuanza kuwaboroshea mazingira yao ambayo yalikuwa taaabani, bado una kazi kubwa ya kuimarisha maisha yao haswa upande wa makazi, wengi bado wanaishi kwenye nyumba ambazo ni duni kulingana na mazingira ya kazi yao wanaendelea kupata msongo wa maisha kutokana na mazingira yao, imarisha posho sana haswa ukizingatia shughuli yao ni ya masaa ishirini na nne, ni shughuli yenye kuhitaji uzalendo wa hali ya juuu na weledi usiokuwa na mipaka, ukisha yafanya haya kwa hawa vijana wako Rais wangu mpendwa mulika mfumo mzima wa Jeshi la polisi katika kupandisha vyeo na upewaji wa Promotion, kwa weledi wanagu mdogo nilionao huwa naaamini kabisa upandishwaji cheo wa kazi za medani haswa hizi za kijeshi hutegemea sana utendaji kazi wako katika ulingo wa medani hyo, pia imarisha vifaa, yakiwemo mavazi na vitendea kazi, nayaleta kwako haya Rais wangu sio kwamba we ndie mwenye kuyatendea kazi unao wasaidizi wazuri kabisa katika Jeshi hili wakipewa mwongozo wanaweza kuyasimamia kwa umakini kabisa.
JESHI LA WANANCHI TANZANIA, hawa ndio walinda mipaka yetu na nchi kwa ujumla, wnafanya kazi yao vizuri kwa sababu hadi sasa nchi yetu ipo shwari kabisa,kilio chao sio tofauti kabisa na Jeshi la polisi yale niliyosema awali hap juu yazingatiwe kabisa, lakini ningependa kushauri licha tu ya kuwa walinzi wa mipaka yetu, ningefurahi kuona Jeshi hili linaongezewa majukumu ya kufanya, isiwe tu wakati wa dharura na majanga, haswa nilifurahishwa na jambo ambalo walilofanya majuzi la kuanza kusambaza vifaa vya mahabara mashuleni, naamini kulitumia Jeshi hili Zaidi ya hapo, sababu miongoni mwao wamejaa wazalendo, nch hiii ya Tanzania tutapiga hatua Zaidi mbele.
Baaada ya kueleza kwa ufupi kuhusu majeshi hayo hapa Tanzania, kuna Jeshi la magereza, paia ambalo mahitaji yake sio tofauti sana na mahitaji ya majeshi mengine, kuna Jeshi pia ambalo ni moyo wa nchi TISS,Mhe Rais angalia upya sharia zilizounda TISS, je zinaendana na wakati tulionao? Je zinawapa nguvu hawa vijana wako kufanya kazi pasipo kuwa na shaka? nakuomba itazame sheria hiii na kwa muongozo wako naamini kabisa kuna jambo linaweza kufanyika.
Nimeandika haya yote MHE, Rais John Pombe Magufuli, sababu unapoimarisha mfumo , mfumo huu utaimarika kwa kuviiiamarisha vyombo vya dola, ambavyo ndilo jicho la nchi yetu, pia nakupongeza sana kwa ujasiri ulionao wa kuonyesha madhaifu yalioifikisha nchi hii hapa tulipo, hakika ni ujasiri wa hali ya juu.