Sooth
JF-Expert Member
- Apr 27, 2009
- 3,922
- 5,626
Rais wetu anaongea sana. Anatoa maelezo mengi hata yasiyopaswa kutolewa. Ni muhimu akatambua kwa nafasi yake anapata fursa ya kuzijua siri za nchi ambazo raia hawapaswi kuzijua, hivyo achunge sana maneno yake kwenye hotuba zake za 'freestyle' kama akapera.
Mfano wa leo ni kauli kwamba hawezi kuongeza mishahara. Je rais ana maanisha hatatoa nyongeza ya kila mwaka ambayo ipo kisheria au lile ongezeko ambalo ni hisani kwa mwajiri kutoa? Kama anazungumzia statutory annual increment ambayo ipo kisheria anakosea sana. Maisha kitaani ni magumu sana, maisha yanakuwa magumu zaidi pale rais ambaye ndiye mwajiri mkuu anapobana haki za wafanyakazi wake halafu anajigamba jukwaani.
Rais angetumia busara ya kukaa kimya tu, yaani mshahara haongezi na hasemi kitu. Kuliko sasa ambapo ameamsha mjadala watu wanaanza kuhoji kama ni kweli wanastahili nyongeza au la. Unamtambiaje kuwa huongezi mshahara mfanyakazi ambaye umemuongezea makato ya HESLB hadi kufikia 15% ya mshahara wake, tofauti na mkataba aliojaza?
Mfano wa leo ni kauli kwamba hawezi kuongeza mishahara. Je rais ana maanisha hatatoa nyongeza ya kila mwaka ambayo ipo kisheria au lile ongezeko ambalo ni hisani kwa mwajiri kutoa? Kama anazungumzia statutory annual increment ambayo ipo kisheria anakosea sana. Maisha kitaani ni magumu sana, maisha yanakuwa magumu zaidi pale rais ambaye ndiye mwajiri mkuu anapobana haki za wafanyakazi wake halafu anajigamba jukwaani.
Rais angetumia busara ya kukaa kimya tu, yaani mshahara haongezi na hasemi kitu. Kuliko sasa ambapo ameamsha mjadala watu wanaanza kuhoji kama ni kweli wanastahili nyongeza au la. Unamtambiaje kuwa huongezi mshahara mfanyakazi ambaye umemuongezea makato ya HESLB hadi kufikia 15% ya mshahara wake, tofauti na mkataba aliojaza?