Rais Magufuli ni Rais Bora lakini.....

Rais Magufuli ni Rais Bora lakini.....

Watanzania tuanze kujiuliza. Kwaanini Unaenda Shule wakati unajua Hakuna Ajira.
Nani aliyewaroga?.
Kuna vijana wanaona yaliowakuta Kaka na Dada zao waliosoma sana. Na wao wanafuata mkumbo huohuo. Kisa Prestige!!.

Elimu unasoma ikusaidie nini kama haitoi Ajira ?.
Unasoma ya nini kama haikuwezeshi kujiajiri?.
Na Kama haikupi descent life?

Tena unakopa Mkopo mrefu wa chuo kikuu unadaiwa na Riba, ukijumlisha na miaka ya kulipa. Unadaiwa Pesa ya kununua Rav 4 ya mtumba.

Graduate, Ukijitazama hata vocha unagongea kwa maparenti ambao hawajabukua kama wewe.

Kusoma sana ni Dalili ya Uoga wa Maisha.
Hakuna Kipya kule ni Muda unapoteza.

Na unarudi kitaa unakuja kuuza vocha kwenye maduka ya Tigo na Voda.
Au kulima kijijini kabisa.

Unakutana na vijana waliachia Form Two wengine La Saba. wanaenda China na Bondeni kwa Madiba kuchukua Mzigo hawajui kubonga kingereza kama chako lakini Mifuko yao imejaa Pesa.

Umebakia tu. You knowww, you knowww..


By ze way.. Niende moja kwa moja kwenye swali lako.

Mheshimiwa Raisi ameruhusu Vijana kupiga biashara popote.
Ametoa na Vitambulisho ili wasisumbuliwe popote. Tena vitambulisho ametoa yeye mwenyewe. Tunaanzaje kuuliza Ajira.

..Tupambane na hali zetu tuweze kujikwamua....

Sawa, kama kujiajiri ni rahisi hivyo. Rais asiibe kura ili kubaki madarakani na yeye aje ajiajiri ili tuende kuiga mafanikio yake, sio yeye ashauri watu kujiajiri wakati yeye mwenyewe anaiba kura ili abaki kwenye ajira.
 
Magufuli is responsible kwa kifo cha huyu mtu,kama huyu kijana alijiua kwa tatizo la akili,nani yupo responsible kujenga mental health facilities kama sio JPM na serikali yake.???..ndege moja ingetosha kabisa kujenga hizi facilities....its time mkuu ai invest kwa watu wake..
Uko vizuri, inaonyesha umesomea una degree ya art wewe. Ni kweli Tunahitaji Mental health facilities. Kwa point hiyo JpM amesababisha kifo cha huyu Kijana.100%.
Lakini tunayo Hospitali ya Mirembe ipo Dodoma. Hii inasaidia hadi Vichaa.


Inasemekana alikua amelewa mfululizo. Nani alimlewesha Pombe ili alaumiwe?. Kampuni ya Bia alizokunywa kijana.

Kwanini tusilaumu mmiliki wa Jengo.
Kujenga jengo refu lililokosa usalama, kiasi mtu anaanguka na kujifia.

Labda Tatizo ni la Familia.
Kwanini tusilaumu viongozi wa Dini na Familia yake kwa kutompa Ushirikiano ili apate matumaini na kuona thamani ya maisha mpaka anajikatia tamaa na kuamua kujiua. Labda Familia haina Professional wa kudili na Mental Health problem.

Zipo Familia zinajali wenye Hela tu. Na kuwadunisha ambao bado wanatafuta kutoka...
Vipi kuhusu Taasisi za Dini?.

Pia Watanzania wana tabia ya kuchangia Harusi na rambirambi lakini hatusaidii Wagonjwa wakiwa bado hai wenye kuhitaji msaada.
 
[emoji4][emoji4][emoji4]
FB_IMG_1545733148932.jpeg
 
Sawa, kama kujiajiri ni rahisi hivyo. Rais asiibe kura ili kubaki madarakani na yeye aje ajiajiri ili tuende kuiga mafanikio yake, sio yeye ashauri watu kujiajiri wakati yeye mwenyewe anaiba kura ili abaki kwenye ajira.
Kuna watu kuiba ni Lazima. That's what they do for a living. Haya hivyo, Raisi haibi bali anachukua.
 
Kuna watu kuiba ni Lazima. That's what they do for a living. Haya hivyo, Raisi haibi bali anachukua.

Hiyo inamaanisha anachukua ili asikose ajira, sasa mbona amaingiza wenzake chaka wakajiajiri huku yeye ajira ndio kila kitu?
 
Uko vizuri. Ni kweli Tunahitaji Mental health facilities. Kwa point hiyo JpM amesababisha kifo cha huyu Kijana.100%.
Lakini tunayo Mirembe ipo Dodoma.


Inasemekana alikua aamelewa mfululizo. Nani alimlewesha Pombe ili alaumiwe?.

Kwanini tusilaumu mmiliki wa Jengo.
Kujenga jengo refu lililokosa usalama, kiasi mtu anaanguka na kujifia.

Labda Tatizo ni la Familia.
Kwanini tusilaumu viongozi wa Dini na Familia yake kwa kutompa matumaini na kuona thamani ya maisha mpaka anajikatia tamaa na kuamua kujiua. Labda Familia haina Professional wa kudili na Mental Health problem. Labda Familia zimebadilika zinajali wenye Hela tu. Na kuwadunisha ambao bado wanatafuta kutoka...

Pia Watanzania wana tabia ya kuchangia Harusi na rambirambi lakini hatusaidii Wagonjwa wakiwa bado hai wenye kuhitaji msaada.

hujui alcoholism ni tatizo la akili pia???...………..watu wanapata msaada na wanapona…...kulewa mfululizo ni sign ya kutaka kukimbia reality...he was blocking something...hizo facilities kama Magufuli angekua amejenga nyingi labda angeomba msaada...pia umetaja Mirembe sasa mimi niko huku Mwaneromango unataka nikamuone daktarin Mirembe sababu I feel soo down and depressed????mnhhhh…..

. mkuu unalaumu jingo? 😀😀😀😀 sijui ni wapi ambapo wenye majengo wanachukua precaution watu wasijiue...honestly speaking hii kitu ndio naisikia leo kwako,lol…….

Viongozi wa dini na familia umesema vizuri hawajui kudili na mtu anaye experience mental health difficulties...ni jukumu la serikali ya Magufuli kuhakikisha wanajamii wana AWARENESS ya matatizo haya na wapi pa kwenda incase wakipatwa haya majanga….na siwalaumu sababu wengi wanaojiua ni watu private sana,unakuta mtu ana familia ila bado anafeel mpweke na ku open na kutoa yanayowasumbua kwa watu wake wa karibu ni ngumu….sasa familia itajuaje huyu mtu anahitaji msaada kama communication ni ngumu?
 
Hiyo inamaanisha anachukua ili asikose ajira, sasa mbona amaingiza wenzake chaka wakajiajiri huku yeye ajira ndio kila kitu?
Charity begines at Home. Huwezi kuwajali wengine kama wewe binafsi hujijali. Nyerere alishindwa kuipigania nchi kwakua hakujijali yeye na familia yake.
Raisi kukuingiza Chaka hiyo Ni Lazima. Haiepukiki. Ndio siasa yenyewe. Umewahi kusikia Vitani Raisi anaingia kupigana Vita mstari wa mbele?.
 
hujui alcoholism ni tatizo la akili pia???...………..watu wanapata msaada na wanapona…...kulewa mfululizo ni sign ya kutaka kukimbia reality...he was blocking something...hizo facilities kama Magufuli angekua amejenga nyingi labda angeomba msaada...pia umetaja Mirembe sasa mimi niko huku Mwaneromango unataka nikamuone daktarin Mirembe sababu I feel soo down and depressed????mnhhhh…..

. mkuu unalaumu jingo? 😀😀😀😀 sijui ni wapi ambapo wenye majengo wanachukua precaution watu wasijiue...honestly speaking hii kitu ndio naisikia leo kwako,lol…….

Viongozi wa dini na familia umesema vizuri hawajui kudili na mtu anaye experience mental health difficulties...ni jukumu la serikali ya Magufuli kuhakikisha wanajamii wana AWARENESS ya matatizo haya na wapi pa kwenda incase wakipatwa haya majanga….na siwalaumu sababu wengi wanaojiua ni watu private sana,unakuta mtu ana familia ila bado anafeel mpweke na ku open na kutoa yanayowasumbua kwa watu wake wa karibu ni ngumu….sasa familia itajuaje huyu mtu anahitaji msaada kama communication ni ngumu?
Kusema za Ukweli. Uko vizuri. Umejenga hoja Vizuri. Nadhani JPM anatakiwa alaumiwe kwa hili.
 
Mkuu, naona unaweza kua na point ila Hujaiweka vizuri maelezo.

Mh.Ole sendeka ana div. Zero form Six lakini ni RC, Mh. Mbowe ana form six(Kama sijaweka rekodi vibaya), Marehemu Steven Ngonyani (Std7) alikua anapanda V8 Cruiser, Mbunge musukuma std 7. Hawa wote wako kwenye system ya utawala. Humprey Polepole kaishia Form 6 katibu Mwenezi CCM alishawahi kua DC. John Mnyika hana degree lakini Mbunge,
Yule mzee jina nimemsahau aliyekua msadizi wa karibu wa Dk slaa na makamu wake wa Raisi kama sijakosea rekodi. Kabla hajakimbilia CCM na kufa kisiasa naye ni Std 7.

Daudi Albert Bashite a.k.a Zero Brain amefoji vyeti lakini anakula good time. Listi ina makanjanja wengi sana wanatutawala.

Inshort kama we ni kijana wa juzi, nikikueleza tulishawahi kua na raisi aliyelazimisha kupewa degree hutaamini.

Njia ya kua mtawala kama John ni kujiingiza kwenye Siasa. Hakuna namna. Masuala ya Elimu sio ya msingi hata Katiba yetu inatanabaisha hivyo. Kujua kusoma na kuandika. That's it.!!
Cha msingi lazima tujifunze kua "Response to Change." Tusifosi Ajira wakati tunajua hazipo. Na hata zilizopo posho zake hazitoshi kutatua changamoto zetu. Tunatakiwa tujiandae kisaikolojia.

Na wengi wanang'ang'ana wakati hata Elimu yenyewe haikupi sifa ya kuajirika. Yaani unapewa mkopo wa 'Elimu Mbovu'. Kwenye interview unafeli. Yaani Inazidi kukuongezea frustrations mtaani. Na deni unadaiwa na jamhuri.

Shida nyingine elimu hiyohiyo mbovu unataka ikuwezeshe kuajirika. Umeuziwa 'kanyaboya' na jamhuri.

Ni kweli Mwisho wa Uraisi wake tutafanya analysis upya. Lakini Kama ataamua kuacha uraisi. Analysis mwishoni ni jambo la kawaida. I
tumie elimu yako ku-survive usawa huu. Hakuna namna.
Kwahiyo nchi iwe ya wanasiasa tu bila wanataaluma sababu ya fedha tu? reckless
 
Kwahiyo nchi iwe ya wanasiasa tu bila wanataaluma sababu ya fedha tu? reckless
In case you forgot what you said...

Wanaoitwa Wasomi tunao wengi sana. Tena wenye Taaluma mbalimbali.

Tunao wale waliomaliza Degree wakarudi chini diploma kusomea Fani kama Ualimu upya na nyingine.

Tunao wale waliomaliza degree, wakarudi versity kusomea degree fani nyingine mpya.

Tunao Na wale ambao walimaliza Degree ya kwanza, wakakosa ramani wakaomba ufadhili wakaenda shule kusomea Masterz. Maarufu kama degree ya kuunganisha.

Lakini bado kama Taifa pamekosekana pa kuwaajiri. Interviews zimekua kama sehemu za kudhalilishana. Graduates wanakua wengi kuliko idadi ya Kazi walizoitiwa.

Na hapo hawataweza kuJA Kuishi kama JPM ALIYESOMA.

So Tuache kudanganyana.
 
Kwanza kabisa nikupe Hongera kubwa kwa namna ulivyowaailisha hoja yako kwa uadilifu mkubwa, maana umejitahidi sana kuwa muungwana, maana ni nadra sana kwa humu jf kupata uzi usio na maneno ya kuudhi au kukera, Hongera kwako, kwa wazazi wako na kwa jamii yote iliyoshiriki kukulea katika maadili hayo mazuuri. Ubarikiwe sana.

Ni kweli kama watanzania tuna mengi yakumpongeza JPM kwa mabadiliko na mageuzi makubwa aliyoyanya kwa kipindi hiki kifupi sana cha miaka mitatu, sitaki niyarudie maana yanafahamika na kila mtu.

Nomba nipishane kidogo na ww kwenye kipengele cha ajira hasa wale graduates wanao uza nyanya, madereva wa bodaboda, mama ntilie na wengine wengi ambao wanafanana na hao, yaani walioamua kujiajiri wenyewe baada ya kukosa ajira. Kuwa na elimu maana yake ni kuwa unauelewa mpana wa mambo na vijimambo, kuona fursa na kuzikimbilia kabla hazija onwa na wengine....!! Lakini pia, kufanya jambo lilelile ambalo wengine hufanya,ww ukalifanya kwa njia tofauti na likakuletea tija kubwa na ukawabariki wanaokuzunguka. Ukifanya jambo kwa kiwango cha mtu kama wa std 7 wakati wewe ni graduate, hapo tunasema 'umesoma lakini haujaelimika',maana yake nini!! Waliuza Ng'ombe ,wakapeleka Ng'ombe ingine shuleni. Hakuna kitu.

Niwashauri graduates wenzangu, kuna ajira nyingi sana zenye kulipa ambazo zipo nje ya mfumo rasmi, wapo walioona fursa hii ya ajira wakakimbilia, hata izo kazi za umma wanazolilia. Tuache kulalama, tumia mda mwingi kufikiria nini ufanye cha kawaida ili kikupe pesa, unitumie muda mwingi kulialia, hakuta kusaidia hata. Kama ni Kilimo Fanya kisasa, kama ni Ufugaji, fanya kwa kufuata kanuni, kama uchinga, Ongeza ubunifu.

Mtaji wala Usiogope, ukishapata wazo la kufanya anza na ulichobarikiwa nacho huku ukiangalia talanta na vipawa ambavyo MUNGU kakujaalia. Uza PC yako au simu yako kupata au kujazia sehemu ya mradi wako, fanya kwa bidii sana kwa Upendo. Baada ya muda utaona matunda ya jasho lako na ujaaliwa, huenda ukwaajiri na wenzio kwa kiwango fulani.

Tusijidanganye eti kuna mwanasiasa atakuja kukuletea maendeleo yako binafsi, hakuna na kama anakuambia hivyo, amini na sadiki kuwa ni muongo na anakudanganya. Serikali huandaa mazingira mazuri tu ya huduma za umma ili kama unatatizo basi litatuliwe kwa urahisi. Mfano shule, huduma za maji, umeme, mawasiliano, uchukuzi, ulinzi na usalama wa raia na Mali, amani na utulivu wa nchi na diplomasia za kimataifa. Kama mwananchi ndio sasa unapaswa kutumia fursa kama hizo kuona cha kufanya ili ujiletee maendeleo yako na familia yako.

By the way, matajiri wengi ni Watu wenye elimu za kawaida, ukiona mtu katajirika huku akiwa Ofisi ya umma, ujue KAPIGA..!!. Magufuli kwa nafasi yake tayari kufanya mengi yaliyo ya muhimu.
mabaashite hofu kuu imewashika
 
Back
Top Bottom