Rais Magufuli ni Rais Bora lakini.....

Rais Magufuli ni Rais Bora lakini.....

Pearce

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2018
Posts
732
Reaction score
1,746
Kweli ana madhaifu mengi tu tutakubaliana wote kutokana na asili ya kisukuma

Wazee wakisukuma na wanyamwezi wanamsemo fulani "Mkubwa hakosei" na mazingira hayo pengine yana changizo fulani katika tabia zake...

Ukweli hatujasikia tena ujangili wa tembo kiasi mataifa ya ulaya yameacha kabisa kujadili hilo. Hivi mnakumbuka Maafisa wa China walituhumiwa kubeba pembe za ndovu katika ziara ya rais wa China Afrika. Kuna jirani yetu mmoja ambaye alikuwa tajiri sana alijenga nyumba yake usiku na mchana mafundi wanapokezana kiasi ikainuka ndani ya mwezi, tena ni nyumba ya chini chini lakini aliweekea msingi wa ghorofa hatukujua huyu mtu hela zote hamepatia wapi, mpaka magufuli alipoingia madarakani akawekwa ndani ndipo tukajua ni mzee wa pembe za ndovu.

Nchi za ulaya ziliituhumu Tanzania kama geti la kuingizia madawa ya kulevya ulaya na wakati huo tumepoteza ndugu wengi tu huko China wakisafirisha madawa ya kulevya hawajawahi kurudi tena Tanzania mpaka leo.

Huku mtaani kuliibuka kundi la vijana walioenda kujiripua na madawa na walikuwa wakirudi mtaani kusema kweli ilifika kipindi tuliona kusoma ni kama kupoteza muda sababu short cut hipo na tunawaona walivyokuwa na pesa nyingi hadi kununua magari hata manne kwa wakati mmoja.

Yapo mengi tu kwa kweli hatutasahau hata tembo wangekuwa na lugha ya kutamka wangekushukuru Mzee wetu

Ila mzee baba tumeona mengi tu mema yako na hatuwezi sahau tatizo ninaloliona umeunganisha maadui wa taifa (Majangili, Mafisadi, wauza madawa ya kulevya) na waliokupenda kwa juhudi zako awali (Wapenda haki katika jamii) kuwa kundi moja wanaokupinga kila leo

Sababu nilizoziona hasa

Haina siri maelfu ya vijana hawana ajira huwezi fahamu ili mpaka ushiriki ajira zinazotangazwa na ajira portal sababu nimeshiriki sana kule unakuta ajira nafasi moja inagombewa na watu si chini ya 200 hadi watu 400 (aina ya nafasi nilizoomba nikashiriki).

Na wapo vijana wengi wamekata tamaa kabisa ukiacha ya kijana Musa wa Rock city mall alieamua kujiua Siku hizi imekuwa kawaida kuwakuta graduates wakiendesha boda boda wakiuza mitumba hadi makondakta na wauza nyanya (sisemi sababu nadharau hizi kazi hapana). basi nini maana ya kupoteza miaka yote katika elimu sababu nafasi za kazi hizi haziitaji tu hata kufika kidato cha 4 5 au 6.

Kauli zako Mzee baba wakati mwingine zinaumiza sana tupo watanzania wengi sana na wengine vyama vyetu ni justice na right tunaumia tunapoona lipo kundi la watu fulani wanaumizwa tu sababu ya itikadi zao na vyama vyao hii haipo sawa.

Mzee wetu Rais wetu na baba wa taifa hili katika kipindi hiki si haki kwa mwenendo wa hali ya taifa letu kutuunganisha kundi moja na maadui wa taifa hili(wauza madawa ya kulevya, LGBT, majangili, mafisadi na wahujumu uchumi) na vijana wasomi ambao wapo kitaa hawana kazi.

Sababu kundi Ovu litachukulia fursa ya ukosefu wa ajira kama kigezo cha kuwaaminisha vijana tusahau mema yako uliyoyatenda tayari kwa taifa.
 
Rais Magufuli Yuko Vizuri sana.
Hana udhaifu wowote. Mambo mengi ni ya kutengeneza. Sasa mtu akijiua wewe unaushahidi kua sababu ni raisi. Ulimpima.akili yake kujua kama.ni mzima au la? Usijali sana mambo madogomadogo.

Tazama ile big picture. Watanzania wanamuelewa vizuri sana.mheshimiwa Raisi. Kuhusu ajira, amekupa fursa kajiajiri mwenyewe. Huyu ndiye Rais bora zaidi duniani. Anasema Ukweli hata kama haupendi kuusikia..amung'unyi maneni. Huyu ni mcha Mungu kabisa.
 
Raisi Magufuli Yuko Vizuri sana.
Hana udhaifu wowote. Mambo mengi ni ya kutengeneza. Sasa mtu akijiua wewe unaushahidi kua sababu ni raisi. Ulimpima.akili yake kujua kama.ni mzima au la? Usijali sana mambo madogomadogo.

Tazama ile big picture. Watanzania wanamuelewa vizuri sana.mheshimiwa Raisi. Kuhusu ajira, amekupa fursa kajiajiri mwenyewe. Huyu ndiye Rais bora zaidi duniani. Anasema Ukweli hata kama haupendi kuusikia..amung'unyi maneni. Huyu ni mcha Mungu kabisa.
wew ni me or Ke
 
Tumshauri mkuu pia mazingira mabaya aliyopandikiza kwa maelekezo,Baraka zake kwa siasa za hovyo Tanzania, ndio leo KUB na wengine wana kesi lukuki,vifungo ,kupotea,mateso na vifo.CDM INA wafuasi wangapi!? Watanzania na wana ccm wangapi wanafurahia upuuzi huu kuharibu umoja na ustawi wa taifa letu!?
Mkono wa amani ni suluhu kubwa kuliko jeshi na vifaru.
 
Raisi Magufuli Yuko Vizuri sana.
Hana udhaifu wowote. Mambo mengi ni ya kutengeneza. Sasa mtu akijiua wewe unaushahidi kua sababu ni raisi. Ulimpima.akili yake kujua kama.ni mzima au la? Usijali sana mambo madogomadogo.

Tazama ile big picture. Watanzania wanamuelewa vizuri sana.mheshimiwa Raisi. Kuhusu ajira, amekupa fursa kajiajiri mwenyewe. Huyu ndiye Rais bora zaidi duniani. Anasema Ukweli hata kama haupendi kuusikia..amung'unyi maneni. Huyu ni mcha Mungu kabisa.
No one is perfect!!....
 
Achagua kuwa baridi au moto siyo analalamika halafu anasifia
silalamiki mkuu kwenye mema lazima nizungumze na mabaya niyataje vilevile sababu mimi sio mpinzani mkereketwa ila ni kundi la tulipata mwangaza wa elimu na kuchambua mambo
 
Tumshauri mkuu pia mazingira mabaya aliyopandikiza kwa maelekezo,Baraka zake kwa siasa za hovyo Tanzania, ndio leo KUB na wengine wana kesi lukuki,vifungo ,kupotea,mateso na vifo.CDM INA wafuasi wangapi!? Watanzania na wana ccm wangapi wanafurahia upuuzi huu kuharibu umoja na ustawi wa taifa letu!?
Mkono wa amani ni suluhu kubwa kuliko jeshi na vifaru.
ni kweli mkuu uhalisia sasa hivi sio wote wanaopinga muelekeo ni wapinzani hapana hata wengine tusio na itikadi ya vyama vyovyote wala kadi tunaopenda ustawi mzuri wa nchi yetu tunasema pia
 
Raisi Magufuli Yuko Vizuri sana.
Hana udhaifu wowote. Mambo mengi ni ya kutengeneza. Sasa mtu akijiua wewe unaushahidi kua sababu ni raisi. Ulimpima.akili yake kujua kama.ni mzima au la? Usijali sana mambo madogomadogo.

Tazama ile big picture. Watanzania wanamuelewa vizuri sana.mheshimiwa Raisi. Kuhusu ajira, amekupa fursa kajiajiri mwenyewe. Huyu ndiye Rais bora zaidi duniani. Anasema Ukweli hata kama haupendi kuusikia..amung'unyi maneni. Huyu ni mcha Mungu kabisa.
Si kulaumu mkuu lkn hapo ndipo uwezo wa kuchambua mambo ulipofikia
 
Kwanza kabisa nikupe Hongera kubwa kwa namna ulivyowaailisha hoja yako kwa uadilifu mkubwa, maana umejitahidi sana kuwa muungwana, maana ni nadra sana kwa humu jf kupata uzi usio na maneno ya kuudhi au kukera, Hongera kwako, kwa wazazi wako na kwa jamii yote iliyoshiriki kukulea katika maadili hayo mazuuri. Ubarikiwe sana.

Ni kweli kama watanzania tuna mengi yakumpongeza JPM kwa mabadiliko na mageuzi makubwa aliyoyanya kwa kipindi hiki kifupi sana cha miaka mitatu, sitaki niyarudie maana yanafahamika na kila mtu.

Nomba nipishane kidogo na ww kwenye kipengele cha ajira hasa wale graduates wanao uza nyanya, madereva wa bodaboda, mama ntilie na wengine wengi ambao wanafanana na hao, yaani walioamua kujiajiri wenyewe baada ya kukosa ajira. Kuwa na elimu maana yake ni kuwa unauelewa mpana wa mambo na vijimambo, kuona fursa na kuzikimbilia kabla hazija onwa na wengine....!! Lakini pia, kufanya jambo lilelile ambalo wengine hufanya,ww ukalifanya kwa njia tofauti na likakuletea tija kubwa na ukawabariki wanaokuzunguka. Ukifanya jambo kwa kiwango cha mtu kama wa std 7 wakati wewe ni graduate, hapo tunasema 'umesoma lakini haujaelimika',maana yake nini!! Waliuza Ng'ombe ,wakapeleka Ng'ombe ingine shuleni. Hakuna kitu.

Niwashauri graduates wenzangu, kuna ajira nyingi sana zenye kulipa ambazo zipo nje ya mfumo rasmi, wapo walioona fursa hii ya ajira wakakimbilia, hata izo kazi za umma wanazolilia. Tuache kulalama, tumia mda mwingi kufikiria nini ufanye cha kawaida ili kikupe pesa, unitumie muda mwingi kulialia, hakuta kusaidia hata. Kama ni Kilimo Fanya kisasa, kama ni Ufugaji, fanya kwa kufuata kanuni, kama uchinga, Ongeza ubunifu.

Mtaji wala Usiogope, ukishapata wazo la kufanya anza na ulichobarikiwa nacho huku ukiangalia talanta na vipawa ambavyo MUNGU kakujaalia. Uza PC yako au simu yako kupata au kujazia sehemu ya mradi wako, fanya kwa bidii sana kwa Upendo. Baada ya muda utaona matunda ya jasho lako na ujaaliwa, huenda ukwaajiri na wenzio kwa kiwango fulani.

Tusijidanganye eti kuna mwanasiasa atakuja kukuletea maendeleo yako binafsi, hakuna na kama anakuambia hivyo, amini na sadiki kuwa ni muongo na anakudanganya. Serikali huandaa mazingira mazuri tu ya huduma za umma ili kama unatatizo basi litatuliwe kwa urahisi. Mfano shule, huduma za maji, umeme, mawasiliano, uchukuzi, ulinzi na usalama wa raia na Mali, amani na utulivu wa nchi na diplomasia za kimataifa. Kama mwananchi ndio sasa unapaswa kutumia fursa kama hizo kuona cha kufanya ili ujiletee maendeleo yako na familia yako.

By the way, matajiri wengi ni Watu wenye elimu za kawaida, ukiona mtu katajirika huku akiwa Ofisi ya umma, ujue KAPIGA..!!. Magufuli kwa nafasi yake tayari kufanya mengi yaliyo ya muhimu.
 
silalamiki mkuu kwenye mema lazima nizungumze na mabaya niyataje vilevile sababu mimi sio mpinzani mkereketwa ila ni kundi la tulipata mwangaza wa elimu na kuchambua mambo
Mku issue ya ajira ni tatizo la kidunia nzima. Nenda hata America au Ulaya watu wamesoma wana masters kazi yakuajiriwa hakuna. Inabidi tu tukubali kwamba wote wanaomaliza University na vyuo mbalimbali serikali haiwezi kuwapa wote ajira.Solution ni kubuni ajira yoyote ya kuingiza kipato hata kama ni kilimo matunda n.k
 
Raisi Magufuli Yuko Vizuri sana.
Hana udhaifu wowote. Mambo mengi ni ya kutengeneza. Sasa mtu akijiua wewe unaushahidi kua sababu ni raisi. Ulimpima.akili yake kujua kama.ni mzima au la? Usijali sana mambo madogomadogo.

Tazama ile big picture. Watanzania wanamuelewa vizuri sana.mheshimiwa Raisi. Kuhusu ajira, amekupa fursa kajiajiri mwenyewe. Huyu ndiye Rais bora zaidi duniani. Anasema Ukweli hata kama haupendi kuusikia..amung'unyi maneni. Huyu ni mcha Mungu kabisa.
Tuna Raisi mpu..uzi tu
 
Tumshauri mkuu pia mazingira mabaya aliyopandikiza kwa maelekezo,Baraka zake kwa siasa za hovyo Tanzania, ndio leo KUB na wengine wana kesi lukuki,vifungo ,kupotea,mateso na vifo.CDM INA wafuasi wangapi!? Watanzania na wana ccm wangapi wanafurahia upuuzi huu kuharibu umoja na ustawi wa taifa letu!?
Mkono wa amani ni suluhu kubwa kuliko jeshi na vifaru.
Mkuu ukienda kwenye Takwimu za Dunia. Tuko izuri duniani. Na Kwa Africa Mashariki pekee sisi ndio Bora zaidi. Sisi ni namba moja kwa Utawala bora. Sisi ndio taifa ambalo demokrasia tunaongoza.

Tena tumezizidi nchi kama Israel, Saudia nk.

Sasa hao wapinzani waliokosa Dola ukiwasikiliza utapotea bure.
Pia mazingira ya Biashara tupo vizuri Africa mashariki. Hakuna nchi inayotuzidi. Tafuta Takwimu.

World Economic Forum, World Bank na taasisi nyingine.

Cc Pearce
No research No right To speak.
 
Mkuu ukienda kwenye Takwimu za Dunia. Tuko izuri duniani. Na Kwa Africa Mashariki pekee sisi ndio Bora zaidi. Sisi ni namba moja kwa Utawala bora. Sisi ndio taifa ambalo demokrasia tunaongoza.

Tena tumezizidi nchi kama Israel, Saudia nk.

Sasa hao wapinzani waliokosa Dola ukiwasikiliza utapotea bure.
Pia mazingira ya Biashara tupo vizuri Africa mashariki. Hakuna nchi inayotuzidi. Tafuta Takwimu.

World Economic Forum, World Bank na taasisi nyingine.

Cc Pearce
No research No right To speak.
Kamwe si wasikilizi wapinzani nina ufahamu wangu wakupembua masuala mbalimbali hivi hatuoni mabambikio ya kodii

hivi hatuoni matatizo ya ajira

hivi hatuoni watu wengine kwa kuwa na itikadi tofauti wanafanywa maadui wa taifa na kwa masuala tunayoyaona kila siku

kuna fact you can just use ur common sense hutakiwi kwenda kufuata makablasha tu
 
Mkuu ukienda kwenye Takwimu za Dunia. Tuko izuri duniani. Na Kwa Africa Mashariki pekee sisi ndio Bora zaidi. Sisi ni namba moja kwa Utawala bora. Sisi ndio taifa ambalo demokrasia tunaongoza.

Tena tumezizidi nchi kama Israel, Saudia nk.

Sasa hao wapinzani waliokosa Dola ukiwasikiliza utapotea bure.
Pia mazingira ya Biashara tupo vizuri Africa mashariki. Hakuna nchi inayotuzidi. Tafuta Takwimu.

World Economic Forum, World Bank na taasisi nyingine.

Cc Pearce
No research No right To speak.
Demokrasia how wakati Saudi ni nchi ya kifalme [emoji848][emoji848][emoji848][emoji848]

Mkuu kama nilivyoainisha ktk thread yangu hatusahau mazuri yake yapo mengi lkn hatupaswi ficha mabaya yatakayomharibia pia

ni heri mimi ninayesema ukweli sababu ukishaifahamu kweli itakuweka huru kuliko ndugu yangu unayesifia tu kwa vitu ambavyo tunaviona katika jamii yetu sasa hivi
 
Kamwe si wasikilizi wapinzani nina ufahamu wangu wakupembua masuala mbalimbali hivi hatuoni mabambikio ya kodii

hivi hatuoni matatizo ya ajira

hivi hatuoni watu wengine kwa kuwa na itikadi tofauti wanafanywa maadui wa taifa na kwa masuala tunayoyaona kila siku

kuna fact you can just use ur common sense hutakiwi kwenda kufuata makablasha tu

Utawala wote wa Kikwete ulikua na Tatizo la Ajira.
Jpm amelikuta tatizo lilikua baya sana.

Hata Elimu ilishakosa thamani. Elimu iliacha kua Ufunguo.

Jk Aliharibu sana. Hata Upinzani ulioibuka wakati wake. Haukua ishara ya demokrasia bali Uzembe na uharibifu wa kiwango cha Lami. Ugaidi, Ufisadi na ujambazi wa kukatisha tamaa. Leo hao walionufaika na keki wamekatiwa mirija wanaanza kulialia kwasababu Miradi walioanzisha kwa pesa ya wizi, inakufa.

Ilishindikana kuwatia hatiani wengi kwasababu kila mtu alikua mwizi majaji, mawakili, polisi, wafanyazazi katika sekta za umma, viongozi wa dini, nk.
Mtu akiharibu anahamishwa kitengo kingine au mkoa mwingine ili akaibe tena.
Nchi ilikua inaoza.



Lakini kuhusu wapinzani hapa nchini.
Hata nikikuuliza, Ni awamu ipi wapinzani waliacha kunyanyaswa?. Jibu hakuna.

Kwa Mfano, Mrema amepigwa sana mabomu. Amesumbuliwa sana.

Maalim Seif mpaka akaitwa Gaidi. mpemba amevumilia mengi sana.

Wakina Amran Kombe, Horace Kolimba wote hawa waliangamia kwa sababu ya Upinzani. .


Wakati wa JK, Wakina Ulimboka, absalom Kibanda na wengine wengi. Dr. Slaa mpaka akalemaa mkono. Mkutank wa Cdm ulipigwa mabomu Arusha wakati wa JK.

Hivyo sio jambo geni sana. Ni muendelezo uleule. Kama utagusia Case study.


Demokrasia ni global agenda.
Lakini sisi kwa Rank za Mwaka huu tupo kwenye hali nzuri zaidi kwa Afrika mashariki.

Hao majirani zetu Kenya hali yao ni mbaya sana. Walishamuua aliyejaribu kuchunguza kashfa ya Rushwa ya Kenyatta. Alipigwa risasi ndani ya gari lake wakalitobia kila sehemu. Akafia hapohapo kwenye gari yake.

Tutazame takwimu duniani ili tuweze kujilinganisha. Tukijitazama sisi pekee yetu, kuna masuala tuna exagurate sana.
 
Watumishi fanyeni hujuma indirect dhidi ya serikali hii onevu kwenu ni miaka 3 hakuna ongezeko la mishahara na maslahi yenu yanazidi kukandamizwa.
 
Back
Top Bottom