Solution ni moja tu mzee wangu
1. Pangua safu yako ya MaRas na MaDas, uliwaweka kwa kufuata vigezo vya ukada kwa CCM badala ya vigezo vya utaalam, uzoefu etc. Matokeo yake wengi ni poor performers. Kumbuka hawa ndo wana mafungu ya pesa za serikali
2. Toa Tax incentive mzee, punguza import tax za bidhaa mbalimbali, ili kwa sasa watu waagize mzigo ujae nchini.acha biashara zinawiri tena, najua kuwa Exports ni better kiuchumi kuliko import lakini katika hali ya kustabilize tax base yako lazima utengeneze tax payers wa baadae ( Fanya kama alivyofanya mzee Mwinyi )
3. Punguza kodi, lakini Tengeneza mfumo wa serikali kupata stahiki yake bila kupoteza senti. Ili hili lifanikiwe Kwa kuanzia hakikisha kila mtanzania above 18 years ana account ya benki, na tengeneza mfumo rasmi wa ICT wa serikali wa kupata baadhi ya huduma kwa kulipia kupitia mfumo huo, huu mfumo utalink na account ya benk ya mtu hivyo basi serikali itaweza kumonita kila senti ya biashara inayofanyika na hivyo kujua kila senti ya kodi yake itakayokuwa inaingia. Kwa sasa unaweza kuendelea na EFD, lakini EFD ni mfumo butu, huwezi kuumonitor at a real time, Tafuta mfumo mwingine cheaper, robust, easy to use. Unaweza kudesa kwa mifumo ya Wachina ya Wechat Money, Alipay etc. Lakini wa kwetu sharti uwe ni wa serikali na Lazimisha baadhi ya huduma Muhimu watu walipie kwa hii solution!
4. Achana na white elephants projects mzee, Uwanja wa ndege Chato siyo Kipaumbele, Hizo ndege zitakupasua kichwa, jiandae kupeleka ruzuku kubwa tu ya kuliendesha hilo shirika
5. Sisitiza Diplomasia ya Uchumi mzee. Sasa hivi wape mabalozi jukumu la kuwatafuta wawekezaji, na pia kutafuta masoko ya bidhaa zetu hasa za kilimo. Ingia makubaliano na nchi mbalimbali zilizoendelea wakupe quota ya kuuza mazao ya wakulima kwao
6. Usigombane na wanaotusaidia bajeti yetu, yaani wahisani, mambo kama Demokrasia yaache yafanyike, huna haja ya kuwa distracted na uwepo wake, kwa sababu energy kubwa unayotumia kuwaza na kuja na mbinu za kuiminya, ungeitumia kuwaza namna gani uboreshe uchumi mzee wangu tungepiga hatua. by the way una miaka miwili hadi saba ya kukaa madarakani, ni muda mfupi sana, stick na ajenda moja tu uchumi, uchumi, uchumi, Hii ya kuminya upinzani haina maana. Upinzani utakuwepo milele, ukiupunguza nje utaukuta ndani ya CCM
7. Vunja baraza la mawaziri, hawa waliopo akina Mpango wameshindwa kuwa wabunifu wa vyanzo vipya vya mapato, ushauri wao kuhusi fiscal policy hususan ktk miaka ile miwili ya mwanzo ndo umesababisha hali tuliyonayo sasa. Lete sura mpya zenye mawazo mapya
8. Ili upunguze resistance na kelele, na upate kutekeleza ajenda ya maendeleo bila kelele za upinzani, hebu fikiria kuunda serikali ya umoja wa Kitaifa, ya kamseto fulani hivi ambapo utawaingiza wapinzani ndani ya serikali yako mpige kazi. Kwa kufanya hivi, utapunguza kelele mtaani na pia utaweza kutumia vipaji vingi tu vinavyohitajika kwa ajili ya kuleta maendeleo. Mzee si ulisema maendeleo hayana vyama?