Miongoni mwa mambo yanayosababisha CCM iendelee kupoteza ni kuwapuuza watumishi wa Umma ikiwa namengineyo. Linaonekana kama jambo dogo ila amini kuwa watumishi wamebeba mnyororo mkubwa wa wategemezi, na ikiwa hawa ni wategemezi wao yaani baba, mama, Mjomba, Kaka, Dada na wengine weeengi ujue pia hawa wategemezi wanaheshimu mawazo ya hao wanaowategemea angalao kuendesha maisha yako kiasi fulani.Na ikatokea huyu mtumishi akilalamika kuwa serikali haiwajali, kumbuka hasira yaho (Wategemezi) inahamia kwenye serikali maana mkate unakuwa haupatikani.
Sasa hivi watumishi wa Umma wanaonekana si kitu kwako Mheshimiwa, wanafanyakazi kwa vitisho, Mshahara uko palepale wakati bei za bidhaa ziko juu. Usitaraji utafanya jambo ambalo litasaidia kupunguza ukali wa maisha zaidi ya kuwawezesha uliyonao ili nao wawawezeshe wengine. Hii ni Afrika na si Ulaya,tunategemeana saana.
Mwisho, ikumbukwe waliyochangia saana kuiangusha CCM ni Watumisi hususani wa Umma maana ndiyo wanaaminiwa na jamii yao kuliko mwanasiasa yeyote yule. Tumia wataalam wako kulichunguza hili utajua ukweli wa haya. Njaa mbaya saana, na maskini haaminiki.
"Magufuli bila Kuwajali Watumishi wa Umma utakutana na Magumu zaidi ya Kikwete"