Rais Magufuli atoa ruhusa Wananchi wa Geita kugawiwa "Magwangala" toka Mgodini

barafu

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
6,726
32,818
Leo Rais JPM alikuwa Mkoani Shinyanga katika Wilaya ya Kahama,inajulikana kuwa Kahama ni moja ya Wilaya yenye madini pamoja na Geita.Katika hotuba zake,JPM leo ametoa "Go ahead" kwa mamlaka husika wakiwemo NEMC kuhakikisha kuwa wananchi wanagawiwa "Magwangala" yote yanayotoka Mgodini.

Kwa wanaotoka kandokando ya migodi wanafahamu kuwa "Magwangala" ni yale mabaki ya udongo unaotokana na kusafishwa kwa dhahabu,kwa miaka mingi watu wa mwambao mwa migodi wamekuwa wakifa kwa kupigwa risasi au kuumwa na mbwa wa walinzi wa migodi kwa kuvamia na kuchukuwa magwangala.Rais amewaagiza Mkuu wa Mkoa,Mkuu wa Wilaya na Mamlaka ya mazingira NEMC kuhakikisha kuwa utaratibu unaandaliwa ili watu wapate mgawanyo huo wa "magwangala".

Rais JPM anasema haiwezekani hao wawekezaji waje hapa,wabebe madini yatu na bado waondoke na mabaki ya udongo wa madini yetu,kuanzia sasa ni mwisho kwa wananchi kuzuiwa kuchukuwa magwangala,maana madini ni ya Watanzania na bila hayo madini kuwa Tz hata hao wazungu wasingekuja.Rais anasema hao wazungu walikuja kufuata dhahabu na si "magwangala",kama hawawezi kuyaacha hayo basi wakatafute sehemu nyingine
 
Kwenye hili nampongeza maghufuli, kwenye huu udongo nilikuwa nahisi haya makampuni yanatuibia madini, inaonekana walikuwa hawachekechi vizuri ili wakwepe kodi halafu wanaenda kusafisha vizuri ulaya wanapata kiasi kikubwa lakini sasa itabidi wachekeche Sana wahakukishe wanamaliza madini yote ili wasipate hasara
 
ila mkae mkijua madhara ya hii kitu mtaanzaa kuyaona baada ya miaka 15 ijayo, nyie mpongezeni tuu msidhan sheria iliyowekwa na NEMC ilikuwa ya kibaguzi, tena kama hao wawekezaji wana nia mbaya hii itakuwa fursa yao ya kutuchafulia mazingira kwa kiwango cha hatari ukizingatia mingi ya hiyo migodi ipo karibu na ziwa Victoria!
 
Kabla ya yote ieleweke kwamba Magwangala ni "sehemu ya mwamba usio na dhahabu(WASTE aka UCHAFU) uliolipuliwa kutoka eneo linalosadikika kuwa na dhahabu(ORE BODY)" na wala sio mabaki ya udongo unaotokana na kusafishwa kwa dhahabu!
@@@Lengo la Mh Rais ni zuri lakini zoezi hili halitakua na practicality achilia mbali kuleta matokeo yaliyokusudiwa.
 
Watanzania wakameze makemikali makali makali ya kusafishia dhahabu.....hivi mzungu na mitambo yake ya kisasa inayonusa mpaka vumbi la dhahabu,ataweza kusahau dhahabu ili mswahili na machekecheo yake ya sido aje aione?

Amri ijayo ni kuwaambia wananchi wavamie wawekezaji
 
Muda si mrefu nchi itaanza kupigizana kelele na wawekezaji wa migodi,kila mahali ni vurugu tu,kuanzia sukari,utumishi wa umma,Mara Dodoma,Mara wapinzani wanavamiwa kwenye haki zao,kila mahali vurugu nchi haitulii kwa nini?
 
Magwangala ni mawe yaliyoondolewa kando kando na mkanda wenye dhahabu gold ore belt, KWA kuwa huwa yako kando na mkanda huwa NA dhahabu kiasi Japo si nyingi kama ile ya kwenye mkanda. Jungu kuu........,pia ukipakana NA tajiri sharti unukie harufu ya pesa
 
Leo Rais JPM alikuwa Mkoani Shinyanga katika Wilaya ya Kahama,inajulikana kuwa Kahama ni moja ya Wilaya yenye madini pamoja na Geita.Katika hotuba zake,JPM leo ametoa "Go ahead" kwa mamlaka husika wakiwemo NEMC kuhakikisha kuwa wananchi wanagawiwa "Magwangala" yote yanayotoka Mgodini.

Kwa wanaotoka kandokando ya migodi wanafahamu kuwa "Magwangala" ni yale mabaki ya udongo unaotokana na kusafishwa kwa dhahabu,kwa miaka mingi watu wa mwambao mwa migodi wamekuwa wakifa kwa kupigwa risasi au kuumwa na mbwa wa walinzi wa migodi kwa kuvamia na kuchukuwa magwangala.Rais amewaagiza Mkuu wa Mkoa,Mkuu wa Wilaya na Mamlaka ya mazingira NEMC kuhakikisha kuwa utaratibu unaandaliwa ili watu wapate mgawanyo huo wa "magwangala".

Rais JPM anasema haiwezekani hao wawekezaji waje hapa,wabebe madini yatu na bado waondoke na mabaki ya udongo wa madini yetu,kuanzia sasa ni mwisho kwa wananchi kuzuiwa kuchukuwa magwangala,maana madini ni ya Watanzania na bila hayo madini kuwa Tz hata hao wazungu wasingekuja.Rais anasema hao wazungu walikuja kufuata dhahabu na si "magwangala",kama hawawezi kuyaacha hayo basi wakatafute sehemu nyingine
hili jina lina uhusiano na ule ukoo wa tai ya pekee hapa nchini?
 
Leo Rais JPM alikuwa Mkoani Shinyanga katika Wilaya ya Kahama,inajulikana kuwa Kahama ni moja ya Wilaya yenye madini pamoja na Geita.Katika hotuba zake,JPM leo ametoa "Go ahead" kwa mamlaka husika wakiwemo NEMC kuhakikisha kuwa wananchi wanagawiwa "Magwangala" yote yanayotoka Mgodini.

Kwa wanaotoka kandokando ya migodi wanafahamu kuwa "Magwangala" ni yale mabaki ya udongo unaotokana na kusafishwa kwa dhahabu,kwa miaka mingi watu wa mwambao mwa migodi wamekuwa wakifa kwa kupigwa risasi au kuumwa na mbwa wa walinzi wa migodi kwa kuvamia na kuchukuwa magwangala.Rais amewaagiza Mkuu wa Mkoa,Mkuu wa Wilaya na Mamlaka ya mazingira NEMC kuhakikisha kuwa utaratibu unaandaliwa ili watu wapate mgawanyo huo wa "magwangala".

Rais JPM anasema haiwezekani hao wawekezaji waje hapa,wabebe madini yatu na bado waondoke na mabaki ya udongo wa madini yetu,kuanzia sasa ni mwisho kwa wananchi kuzuiwa kuchukuwa magwangala,maana madini ni ya Watanzania na bila hayo madini kuwa Tz hata hao wazungu wasingekuja.Rais anasema hao wazungu walikuja kufuata dhahabu na si "magwangala",kama hawawezi kuyaacha hayo basi wakatafute sehemu nyingine

Duh huyu rais kiboko yaani anaona fahari raia wake wagawiwe makombo baada ya mgeni kula steki yote. Sisi Waafrica safari yetu ya kujitambua bado ni ndefu sana.
Kwa nn asingefanya mpango hao wananchi waungane kwenye vikundi kisha wapewe maeneo ya kuchimba dhahabu badala ya kuhamasisha wapewe magwangala? Maana bado maeneo yapo.
 
Back
Top Bottom