Rais Magufuli amethibitisha tena kuwa mhimili wake ndiyo uliojichimbia zaidi chini hapa nchini

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,160
Serikali yoyote duniani inaweza kuitwa ina utawala bora, iwapo tu itazingatia utawala wa sheria, kama unavyoitwa kwa kiingereza "power seperation" ambao unaheshimu mgawanyo wa madaraka kati ya mihimili 3 mikuu, ambayo ni serikali, Bunge na Mahakama, katika kile kinachoitwa "check and balance"

Hapa nchini kwetu, kama ambavyo aliwahi nukuliwa mkuu wetu wa nchi, akitamba kuwa mhimili wa serikali ndiyo "superior" kwa wenyewe kujichimbia chini zaidi na hivyo kuwa juu ya mihimili hiyo mingine!

Hilo limethibitika baada ya Rais Magufuli kumteua kada na CCM, Dr Wilson Mahera, kuwa ndiyo Mkurugenzi mpya wa uchaguzi hapa nchini, kitendo ambacho ni uvunjaji wa waziwazi wa Katiba yetu ya nchi, kwani analazimika kuteua mkurugenzi wa uchaguzi ambaye siyo kada wa chama chake

Hivi kitendo hicho cha Rais tunaweza kukielezaje, kama siyo kuudharau mhimili wa mahakama??

Sote tunakumbuka uamuzi wa hivi karibuni wa mahakama kuu, wa kusema kuwa wakurugenzi wa wilaya hawawezi tena kuwa wasimamizi wa uchaguzi zinazohusisha uchaguzi za vyama vingi hapa nchini baada ya mahakama hiyo kujiridhisha kuwa wapo wakurugenzi ambao pia ni makada wa CCM zaidi ya 74 hapa nchini ambao wamepewa madaraka hayo ya kusimamia chaguzi hizo

Ingawa tunajua kuwa serikali imekata rufaa kupinga uamuzi huo, kwa kuwa rufaa hiyo haijaanza kusikilizwa , kwa hiyo kwa sasa inafahamika wazi kuwa maDED, HAWAPASWI kusimamia chaguzi za aina yoyote hapa nchini

Hivi kitendo cha Rais wetu kumteua kada huyo wa CCM, siyo kitendo cha kuidharau mhimili huo wa mahakama kwa maamuzi iliyoyafanya??

Hivi kitendo hicho kina tofauti gani na mathalani mechi ya mpira wa miguu ya watani wa jadi ya Yanga na Simba, kubaini kuwa mwanachama wa kindakindaki wa moja ya klabu hiyo ndiye aiyeteuliwa kuwa "refa" wa mechi hiyo??

Ni dhahiri kuwa timu pinzani itagomea kucheza mechi hiyo kwa kuamini kuwa "refa" aliyeteuliwa kusimamia mechi hiyo, hatotenda haki kwa upande wao

Uthibitosho mwingine wa Rais wetu kuingilia mihimili mwingine ni hivi karibuni kunukuliwa akimweleza Spika wa Bunge letu kuwa amefanya vyema kumtimua aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, ambaye dunia nzima inajua kuwa yupo nje ya nchi kwa matibabu, kutokana na "watu wasiojulikana" kumminia risasi nyingi kwa lengo la kumuua, lakini kwa kudra ya Mwenyezi Mungu, alimnusuru kimiujiza na akanusurika kuuawa na hadi hivi sasa anaendelea kupata matibabu nje ya nchi

Hivi Rais Magufuli anawezaje kumwita Tundu Lissu kuwa amelitelekeza jimbo hilo wakati dunia nzima inafahamu kuwa Tundu Lissu yupo nje ya nchi akijitibu??

Hayo ni matukio mawili kati ya mengi sana, ambayo nchi yetu chini ya utawala huu wa serikali ya awamu ya tano unavyojaribu kwa kila njia ili kuua upinzani,ambao umedumu hapa nchini kwa zaidi ya miaka 25 hivi sasa

Kama nchi ni lazima tuheshimu kwa nguvu zote misingi ya kulinda demokrasia yetu na tufahamu pia kitendo cha kuvuruga zoezi la uchaguzi, ni kitendo kitakachohatarisha amani ya nchi yetu, ambayo ndiyo lulu pekee ambayo nchi yetu inajivunia nayo
 
Watanzania tutashutuka baada ya mambo kuharibika hata hitila alikuwa na wafuasi wengi mabutu seseko alikuwa na wafuasi kibao hata muhasi Jonas savimbi naye alikuwa na wafuasi lakini wazawa walishituka baadaye
 
Watanzania tutashutuka baada ya mambo kuharibika hata hitila alikuwa na wafuasi wengi mabutu seseko alikuwa na wafuasi kibao hata muhasi Jonas savimbi naye alikuwa na wafuasi lakini wazawa walishituka baadaye
Absolutely true

Hivi hao viongozi wastaafu hawazioni "indicators" zote zinazoonyesha kuwa nchi yetu hivi sasa inatawaliwa kidikteta??

Ni kwanini hawajitokezi na kukemea mwenendo huu wa utawala wa serikali ya awamu ya tano??

Wanasubiri kuona damu ikimwagika nchini, ndipo watakapoingilia kati??
 
Mpambavu hukata tawi alilokaria na akiporomoka nalo anaaza kusema eti amerogwa. Kama kuna mtu anayetakiwa kulinda na kuheshimu katiba ni Rais kwani cheo cha Urais ni cheo ambacho kinapatikana kwa kutegemea katiba na sheria.

Na wakati wa kuapishwa huapishwa kulinda katiba ya nchi na sheria, haapi kujenga viwanda wala kununua ndege. Rais anapo kiuka sheria ni kwamba huyo raisi amefeli vibaya sana, na hafaii hata kuitwa Rais.

Kwa sababu Rais mlinzi na msimamizi mkuu wa sheria na katiba na hiyo ndio kazi kubwa aliyopewa na wananchi. Wananchi kwa kumsikiliza maelezo yake ya kampeni walimwamini kuwa atalinda katiba yao bila upendeleo na kwa imani hiyo waka mchagua.

Sasa inapo tokea amevuja katiba au ameacha kuheshimu sheria basi huyo sio Rais bali ni tapeli wa njia ya kuaminiwa.

Hiyo ndio tafsiri ya Rais asiye heshimu Katiba, nitapeli kama matapeli wengine.
 
Wameharibu hata ubongo wa vijana, wanadai eti mihimili mingine inakwamisha maendeleo tumwache rais afanye kazi!!! Huwa natamani kulia kusikia jinsi baadhi ya watu walivyooza akili kabisa!

Uwezo wa kufikiri wa waTZ unaelekea kuuliwa kabisa!! Tutakuwa taifa la watu wapumbavu kabisa tusioweza kupambanua mambo hata madogo tu!!

Kiongozi huyu hatufai kabisa!! Anaua uwezo wa kufikiri!! Kwa watu wenye akili hata kidogo, huyu hafai kabisa kuendelea na kazi hii ....
 
mpambavu hukata tawi alilokaria na akiporomoka nalo anaaza kusema eti amerogwa. kama kuna mtu anaye takiwa kulinda na kuheshimu katiba ni raisi kwani cheo cha uraisi ni cheo ambacho kinapatikana kwa kutegemea katiba na sheria. na wakati wa kuapishwa huapishwa kulinda katiba ya nchi na sheria, haapi kujenga viwanda wala kununua ndege. raisi anapo kiuka sheria ni kwamba huyo raisi amefeli vibaya sana, na hafaii hata kuitwa raisi. kwasababu raisi mlinzi na msimamizi mkuu wa sheria na katiba na hiyo ndio kazi kubwa aliyo pewa na wananchi. wananchi kwa kumsikiliza maelezo yake ya kampeni walimwamini kuwa atalinda katiba yao bila upendeleo na kwa imani hiyo waka mchagua. sasa inapo tokea amevuja katiba au ameacha kuheshimu sheria basi huyo sio raisi bali ni tapeli wa njia ya kuaminiwa. hiyo ndio tafusiri ya raisi aiye heshimu katiba. nitapeli kama matapeli wengine.
Hakika nchi hii inaelekea kubaya.............

Ni muhimu kwa kila mwananchi hivi sasa kukemea kwa nguvu zote uvunjifu huu wa sheria wa waziwazi
 
Wameharibu hata ubongo wa vijana, wanadai eti mihimili mingine inakwamisha maendeleo tumwache rais afanye kazi!!! Huwa natamani kulia kusikia jinsi baadhi ya watu walivyooza akili kabisa!

Uwezo wa kufikiri wa waTZ unaelekea kuuliwa kabisa!! Tutakuwa taifa la watu wapumbavu kabisa tusioweza kupambanua mambo hata madogo tu!!

Kiongozi huyu hatufai kabisa!! Anaua uwezo wa kufikiri!! Kwa watu wenye akili hata kidogo, huyu hafai kabisa kuendelea na kazi hii ....
Hivi kuna nchi yoyote iliyokuwa na miundo mbinu mizuri barani Afrika zaidi ya Afrika Kusini??

Wangejiuliza hao vijana, ni kwa vipi dunia yote iliwawekea vikwazo nchi hiyo enzi zile za ubaguzi wa rangi?

Demokrasia ndiyo kigezo kikuu cha nchi yoyote duniani

Nchi yoyote ambayo inapuuza haki za msingi wa binadamu, inafaa isusiwe na dunia nzima.
 
Kwani uongo? Mhimili mmoja una mamlaka zaidi juu ya zingine. Ndo unagawa pesa za mishahara na miradi ya hao wengine, ndo una jeshi kwa ajili ya usalama wa hao wengine e.t.c.
 
How will you prove the validity of your claim against this presidential appointment? What does the law say? Is there any law which has been contravened?

Ni lini appointee wa Rais kwenye Tume ya Uchaguzi hajawahi kuwa kada wa chama: mbona wamekuwa wakifanya vyema tu? Kwa nini una wasiwasi na huyu, au chuki binafsi dhidi ya mteuliwa?
 
Mhimili ule umeangamia kabisa,mhimili hata kwa mtu asiye na upeo wa taaluma atagundua kwamba hadhi na heshima yake imepotoa kutokana na kuingiliwa na kupangiwa kipi wafanye na kipo wasifanye.

Mhimili ulikua ni kimbilio la wengi,mhimili ulitegemewa na kuaminiwa sana na matajiri na masikini,wakulima na wafanyakazi na hata watu wa vijiweni.

Kati ya mihimili ambayo iliheshimiwa sana.
Hua najiuliza,hv wenye sauti wanashindwa kukemea? Hivi anayesimamia mhimili ule hajisikii vibaya?

Ni kwanini haumii kuona yatakayo jitokeza baada ya watu kukata tamaa?
Haogopi historia yake kuandikwa vibaya?
Ole kwa kizazi cha taifa lile la wadanganyika,taifa la wakaldayo ambalo wazee wa taifa hilo wameamua kukaa kimya

Ni ndoto tu jamani,najaribu kuota
 
Mahakamani utashinda kama ni kesi ya madai ila VS Jamhuri hushindi kamwe. Vitisho vitatumika
 
Kiongozi wa Muhimili huo kazi yake siku hizi ni kuhudhuria kuapishwa viongozi wa serikali.
 
Hakika sasa inaeleweka rasmi kwa nini huyu CJ wa sasa ali-act kwa muda mrefu kwenye nafasi hiyo kabla ya kuthibitishwa rasmi..

Kabaki kuwa CJ wa kwenda kuhudhuria kila shuguli ya Ikulu..

Mpaka sura yake inatia kinyaa.
 
Hivi kuna nchi yoyote iliyokuwa na miundo mbinu mizuri barani Afrika zaidi ya Afrika Kusini??

Wangejiuliza hao vijana, ni kwa vipi dunia yote iliwawekea vikwazo nchi hiyo enzi zile za ubaguzi wa rangi?

Demokrasia ndiyo kigezo kikuu cha nchi yoyote duniani

Nchi yoyote ambayo inapuuza haki za msingi wa binadamu, inafaa isusiwe na dunia nzima.
Baadhi ya watanzania wamekufa kabisa ubongo!! Eti mtu akisimamia kununua Ndege tu tena bila kufuata utaratibu tayari anaabudiwa!! hata akiua watu hovyo
 
Absolutely true

Hivi hao viongozi wastaafu hawazioni "indicators" zote zinazoonyesha kuwa nchi yetu hivi sasa inatawaliwa kidikteta??

Ni kwanini hawajitokezi na kukemea mwenendo huu wa utawala wa serikali ya awamu ya tano??

Wanasubiri kuona damu ikimwagika nchini, ndipo watakapoingilia kati??
waliishafungwa midomo si nyingi !!
 
Y
Mhimili ule umeangamia kabisa,mhimili hata kwa mtu asiye na upeo wa taaluma atagundua kwamba hadhi na heshima yake imepotoa kutokana na kuingiliwa na kupangiwa kipi wafanye na kipo wasifanye.

Mhimili ulikua ni kimbilio la wengi,mhimili ulitegemewa na kuaminiwa sana na matajiri na masikini,wakulima na wafanyakazi na hata watu wa vijiweni.

Kati ya mihimili ambayo iliheshimiwa sana.
Hua najiuliza,hv wenye sauti wanashindwa kukemea? Hivi anayesimamia mhimili ule hajisikii vibaya?

Ni kwanini haumii kuona yatakayo jitokeza baada ya watu kukata tamaa?
Haogopi historia yake kuandikwa vibaya?
Ole kwa kizazi cha taifa lile la wadanganyika,taifa la wakaldayo ambalo wazee wa taifa hilo wameamua kukaa kimya

Ni ndoto tu jamani,najaribu kuota
Yaani ni jambo la ajabu kwa mhimili uliopewa mamlaka kikamilify kutafsiri sheria, lakini Leo hii unakwepa wajibu wake na kudai kuwa ukisikiliza kesi "Fulani" utakuwa umeingilia mamlaka ya mhimili mwingine!

Hata yanatokea Tanzania pekee!
 
How will you prove the validity of your claim against this presidential appointment? What does the law say? Is there any law which has been contravened?

Ni lini appointee wa Rais kwenye Tume ya Uchaguzi hajawahi kuwa kada wa chama: mbona wamekuwa wakifanya vyema tu? Kwa nini una wasiwasi na huyu, au chuki binafsi dhidi ya mteuliwa?
The law says that President SHALL appoint a Tanzanian to hold that post,but that person who is appointed SHOULD NOT BE A MEMBER OF ANY PARTY

Wewe hajaona tu bado namna Rais alivyovunja Katiba ya nchi,kwa kumteua Mkurugenzi wa uchaguzi, ambaye ni kada wa chama chake cha CCM??
 
Kwani uongo? Mhimili mmoja una mamlaka zaidi juu ya zingine. Ndo unagawa pesa za mishahara na miradi ya hao wengine, ndo una jeshi kwa ajili ya usalama wa hao wengine e.t.c.
Una uelewa mbovu kuhusu separation of power. Kutoa mishahara ulinzi na kukusanya kodi ni majukumu waliyopewa na katiba, na wengine walipewa wajukumu mengine. Haimaanishi mhimili mmoja uko juu ya mwingine.
 
Back
Top Bottom