Rais Magufuli akutana na Mabalozi wa Marekani na Italia

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,980
92.jpg

111.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha pamoja na kuzungumza na Balozi wa Marekani hapa nchini Mark Childress Ikulu jijini Dar es Salaam
121.jpg

131.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha na kufanya mazungumzo na Balozi wa Italia hapa nchini anayemaliza muda wake Luigi Scotto Ikulu jijini Dar es Salaam
=========================================================​
Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mhe. Mark Childress aliyekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amesema kutolewa kwa fedha hizo ni uthibitisho kuwa kutotolewa kwa fedha za awamu ya pili ya mradi wa changamoto za milenia (MCC-2) hakujaondoa uhusiano na ushirikiano wa Tanzania na Marekani ikiwemo utoaji wa misaada ya maendeleo.

"Tumezungumza mambo kadhaa, na wiki hii Tanzania na Marekani kupitia shirika letu la misaada la USAID tunatarajia kutiliana saini mkataba wa zaidi ya dola milioni 400 kwa ajili ya mwaka ujao, pia tumezungumza kuwa kutakuwa na dola milioni 800 zitakazotolewa na Marekani kwa ajili ya miradi mbalimbali na hii haihusiani na MCC.

"Ukweli ni kwamba tunayo mengi ya kufanya pamoja katika sekta mbalimbali zikiwemo afya, elimu na kilimo na tutafanya kila juhudi kuhakikisha haya yanafanikiwa" Amesema Balozi Mark Childress muda mfupi baada ya kumaliza mazungumzo na Rais Magufuli.

Kwa upande wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amesema serikali yake ya awamu ya tano itaendeleza na kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano na Marekani na kwamba fedha za msaada kutoka Marekani ni muhimu kwa maendeleo ya Tanzania.

Katika hatua nyingine Rais Magufuli ameagana na Balozi wa Italia hapa nchini Mheshimiwa Luigi Scotto ambaye amemaliza muda wake wa miaka mitatu.

Balozi Luigi Scotto amesema katika kipindi chake amewezesha kuongezeka kwa biashara kati ya Italy na Tanzania kwa asilimia 35 na ameielezea Tanzania kuwa ni nchi nzuri aliyoipenda na kwamba ataendelea kutangaza fursa zilizopo Tanzania huko Italia na kwingineko.
 
Mimi huwa siwaamini hawa watawala wa nchi za Magharibi.

Kwa sasa wamegundua kama Rais Magufuli haingiliki kwa njia waliyokuwa wamezoea na wanachokifanya kwa sasa ni kutumia njia nyingine katika kutimiza malengo yao.

We must take anything they say with a grain of salt!

Inawezekana kinachotafutwa kwa sasa ni mkataba wa Symbion ukubaliwe na Ikulu kwa sababu inavyoonekana Rais Magufuli imeweka kizingiti katika kuridhia mkataba mpya na serikali.

Rais endelea kuwa masikini jeuri kwa sababu maliasili tulizonazo ni silaha na ngao imara katika kupambana na siasa za kiuchumi za nchi za Magharibi.
 
Kwanini siku hizi hawa mabalozi wa ulimwengu wa Kwanza wanapishana kila siku Ikulu??

Mara balozi wa China, mara wa Japan, mara wa Uingereza, mara wa Germany.

Kuna nini Mgogoni??

Siku hizi Ikulu wanagawa juice ya bure??

Au palipo na mzoga ndipo tai wengi hukusanyika.??
 
Kwanini siku hizi hawa mabalozi wa ulimwengu wa Kwanza wanapishana kila siku Ikulu??

Mara balozi wa China, mara wa Japan, mara wa Uingereza, mara wa Germany.

Kuna nini Mgogoni??

Siku hizi Ikulu wanagawa juice ya bure??

Au palipo na mzoga ndipo tai wengi hukusanyika.??
Watu wa nchi za Magharibi ni wazuri sana katika kusoma boby language na tone za watu.

Mimi ninadhani wanajaribu kukutana na Rais Magufuli uso kwa uso ili waweze kumfahamu vizuri kupitia boby language na tone yake ili waweze kujenga picha timilifu kuhusu mstakabali wa uwekezaji wao kisiasa na kiuchumi nchini.
 
On a serious note;Hivi si alikashifu misaada ya nje na kusema haiwezekani nchi tajiri kama hii itegemee misaada kutoka nje?

Hiyo kauli kuwa misaada ya Marekani ni muhimu ameitoaje tena?

Kumbe yale matusi yote dhidi ya MCC yalikuwa ni sizitaki mbichi hizi?

Kweli wazungu wanajua unafiki wa viongozi wetu na wanawapeleka hivyohivyo.Unafiki haujawahi kuleta afya.
 
"Tanzania ni nchi tajiri, hatuwezi kua omba omba "
Hoja yako ni nini?

Umeona andiko linalosema Rais Magufuli ameomba omba?

Rais Magufuli alishasema, hataki misaada yenye masimango kwa maana kuwa hawezi kubadilisha mtazamo wake kama Rais wa Tanzania ili apate msaada.

Wanaotoa msaada wanatoa katika msingi aliojiwekea Rais Magufuli na siyo msingi waliojiwekea watoa misaada.
 
Sijui ametumia lugha gani kuwasiliana nao

On a serious note;Hivi si alikashifu misaada ya nje na kusema haiwezekani nchi tajiri kama hii itegemee misaada kutoka nje?

Hiyo kauli kuwa misaada ya Marekani ni muhimu ameitoaje tena?

Kumbe yale matusi yote dhidi ya MCC yalikuwa ni sizitaki mbichi hizi?

Kweli wazungu wanajua unafiki wa viongozi wetu na wanawapeleka hivyohivyo.Unafiki haujawahi kuleta afya.
Ben, Boss huwa hanuniwi.

Magufuli hana namna.
 
Sijui ametumia lugha gani kuwasiliana nao

On a serious note;Hivi si alikashifu misaada ya nje na kusema haiwezekani nchi tajiri kama hii itegemee misaada kutoka nje?

Hiyo kauli kuwa misaada ya Marekani ni muhimu ameitoaje tena?

Kumbe yale matusi yote dhidi ya MCC yalikuwa ni sizitaki mbichi hizi?

Kweli wazungu wanajua unafiki wa viongozi wetu na wanawapeleka hivyohivyo.Unafiki haujawahi kuleta afya.

On serious note; Rais Magufuli hajasema hataki msaada bali alisema hataki misaada ya masimango, kwa maana nyingine, watoe misaada kwa kutumia terms and conditions alizoziweka Rais Magufuli.

Ni kweli viongozi wetu ni wanafiki kwa sababu kuna wengine kwa miaka zaidi ya minane walikuwa wanatuambia Lowassa ni fisadi papa na hafai kuwa Rais wa Tanzania lakini kabla ya miezi mitatu ya Uchaguzi Mkuu 2015, wakamchukua Lowassa na kumfanya mgombea Urais na kuanza tena kutuaminisha kuwa Lowassa siyo fisadi papa na anafaa kuwa Rais wa Tanzania.
 
On a serious note;Hivi si alikashifu misaada ya nje na kusema haiwezekani nchi tajiri kama hii itegemee misaada kutoka nje?

Hiyo kauli kuwa misaada ya Marekani ni muhimu ameitoaje tena?

Kumbe yale matusi yote dhidi ya MCC yalikuwa ni sizitaki mbichi hizi?

Kweli wazungu wanajua unafiki wa viongozi wetu na wanawapeleka hivyohivyo.Unafiki haujawahi kuleta afya.
Wewe pacha wake Lowasa hakuna aliye wabembeleza na Rais husema wazi na aliwambia waige mfano wa China na sasa wameleta wenyewe!
 
Nikikumbuka yale masusla ya "Tena Sukari yenyewe ni very inferior kutoka nje ukilinganisha na ya hapa kwetu" huwa napata hofu sana nikimuona amekaa na wazungu kama hivi
 
On a serious note;Hivi si alikashifu misaada ya nje na kusema haiwezekani nchi tajiri kama hii itegemee misaada kutoka nje?

Hiyo kauli kuwa misaada ya Marekani ni muhimu ameitoaje tena?

Kumbe yale matusi yote dhidi ya MCC yalikuwa ni sizitaki mbichi hizi?

Kweli wazungu wanajua unafiki wa viongozi wetu na wanawapeleka hivyohivyo.Unafiki haujawahi kuleta afya.

misaada ya masharti mkuu! hicho ndicho alikuwa hakitaki! ...
 
Kwanini siku hizi hawa mabalozi wa ulimwengu wa Kwanza wanapishana kila siku Ikulu??

Mara balozi wa China, mara wa Japan, mara wa Uingereza, mara wa Germany.

Kuna nini Mgogoni??

Siku hizi Ikulu wanagawa juice ya bure??

Au palipo na mzoga ndipo tai wengi hukusanyika.??
"Cha mtu huliwa na mtu bali chuma pekee huliwa na kutu"
 
Ben, Boss huwa hanuniwi.

Magufuli hana namna.
Wakumbuke Rais Magufuli is here to stay for 5 years or more.

Mbaya zaidi, kwa sasa lazima kwanza CHADEMA wamuweke pembeni Lowassa na genge lake ili watu wenye fikra pevu waweze kuanza kuiangalia CHADEMA kama chama chenye fikra mbadala kiutawala.
 
On a serious note;Hivi si alikashifu misaada ya nje na kusema haiwezekani nchi tajiri kama hii itegemee misaada kutoka nje?

Hiyo kauli kuwa misaada ya Marekani ni muhimu ameitoaje tena?

Kumbe yale matusi yote dhidi ya MCC yalikuwa ni sizitaki mbichi hizi?

Kweli wazungu wanajua unafiki wa viongozi wetu na wanawapeleka hivyohivyo.Unafiki haujawahi kuleta afya.
Hakika umenena ben, Tanzania ni sikio la kufa aisee, sitaki nataka
 
Back
Top Bottom