Rais Magufuli akifanya mambo haya, Watanzania watamlilia wenyewe aongezewe muda wa kutawala

Mh Rais yeye mwenyewe kasema hataki kuongezewa muda na mbona twamlazimisha etii hata afanye nini muda wake ukiisha asepe
 
Iv president uwa anapitia hizi nyuzi kweli..... au anatakiwa kuzipata vipi?? Kuna nondo za kutosha sana humu
 
Kuna mtu juzi alianzisha uzi unaosema kuwa watanzania wanatamani magari ambayo hayapo duniani; lisinywe mafuta, likimbie, vipuri viwe vya bure etc wewe sasa unatamani kodi zipunguzwe ila wanaotafuta ajira wote waajiriwe! Unataka nyongeza ya mshahara wakati kodi zimefutwa! It’s impossible my friend
 
Umeandika Mambo mazuri Sana,lakini ukidhubutu kuivunja katiba ,utakuwa umeingiza ugonjwa mbaya,na wangine hata Kama watabolonga ,wataivunja ili waendelee kubaki on power.
 
A
Hayo yote uloyoyataja yanahitaji pesa. Sasa kwa kodi anazotegemea hizi hawezi kuyafanya.

Anachojua ni kukamua ngombe maziwa ila malishoni hawezi mpeleka.
 
Maajabu hayaishi. Yaani kwa uovu wote aliowafanyia watanzania, halafu eti waandamane kumtaka aendelee?

1) Kuua demokrasia ya uchaguzi, uhuru wa maoni na uhuru wa vyombo vya habari
2) Upendeleo wa wazi kwa kijiji chake. Kutumia rasilimali za nchi nzima kujengea miradi isiyo na tija kijijini kwake
3) Kufanya teuzi za upendeleo kwa kuteua watu wengi wa kanda yake kuongoza taasisi mbalimbali za serikali
4) Kuwatesa watu kwa kuwafunga kwa muda mrefu kisha kuwalazimisha wakubali kuwa wamehujumu uchumi
5) Kuua biashara kwa kuwabambikia kodi zisizolipika wafanyabiashara
6) Kuangusha ukuaji wa uwekezaji toka 28% mpaka 4%
7) Kuangusha ukuaji wa sekta ya utalii toka 15% mpaka 3.6%
8) Kuangusha thamani ya mauzo ya mazao ya kilimo kwa 50%
9) Kuharibu mazingira ya uwekezaji kiasi cha wawekezaji wengi kuhama nchi na kwenda mataifa jirani
10) Kuharibu mazingira ya uwekezaji sekta ya madini, mpaka kuifikisha Tanzania kwenye nafasi ya kwanza kuwa na mazingira mabaya Duniani
11) Kuendesha uongozi wa kilaghai na udanganyifu kama vile kuwadanganya wananchi kuwa Tanzania hakuna corona kumbe dhamira yake ni kutokuwa tayari kutumia rasilimali za Taifa kunusuru maisha ya wananchi
12) Kushindwa kufanya maandalizi ya mazingira ya kuwahudumia waathirika wa corona, na badala yake kupora pesa iliyotolewa na jamii ya kimataifa kwaajili ya kupambana na corona, na kupeleka kwenye maigizo ya uchaguzi , kisha kuwadanganya wananchi kuwa tumetumia pesa ya ndani kugharamia uchaguzi
13) Kuua ajira
14) Kutopandisha mishahara kwa wafanyakazi kwa miaka 6
15) Kutunga sheria gandamizi ili kuua uhuru wa watu wa kupashana habari
16) Kuanzisha kodi mbalimbali kuwakamua wananchi wa hali ya chini kama vile kodi za vocha, kodi za ufugaji kuku, kodi za visima vya maji, kodi za mashamba, kodi za mazao ya miti ya kupanda, kodi ya nyumba za vijijini, n.k.

Mimi naamini, kila mtanzania, hata yule mwenye akili ndogo kabisa, ukiwaacha wanafiki, huyu mtu hata aseme leo hii kuwa anaondoka, itakuwa ni sherehe kubwa kila kona ya nchi. Ameleta madhara zaidi kuliko faida.

Kitu kimoja kikubwa asichokijua, hakuna hata nchi moja iliyokuwa maskini halafu ilipata maendeleo kwa haraka kwa kuongeza uwingi na ukubwa wa kodi. Kadiri kodi zinavyokuwa nyingi na kubwa, ndivyo unavyoua uwekezaji, ndivyo unavyoua ajira, ndivyo unavyoua soko la bidhaa, ndivyo unavyoua teknolojia, na ndivyo unavyoua mwingiliano wa kisekta ambao husaidia sekta kuinuana.
 
Habari zenu mabibi na mababu!

Kwanza kabisa ni ukweli usiopingika kuwa kwa sasa kila mtu anapoambiwa au kusikia kuongezewa muda wa kutawala Rais magufuli anashikwa na ghadhabu na kutamani ata kumpiga mtu ngumi kutokana na ugumu wa maisha uliopo.

Sio watumishi wa Serikali, sio wafanyabiashara, machinga, wastaafu, wanachuo, wahitimu wa chuo, mama ntilie, wachuuzi, n.k wote hawa hawataki kusikia ata kidogo msamiati wa Rais magufuli kuongezewa muda wa kutawala, wamemchoka vibaya mnoo kiasi kwamba mpaka wanajuta kwanini walimpa uraisi na bila kupepesa macho wanatamani ata kesho tu Amalize muda wake wa kutawala waangalie ustaarabu wa raisi ajae.

Na wale wanaoshupalia kuwa aongezewe ni wabunge ambao wapo bungeni wakiona hawana cha kupoteza kwamba akitawala milele basi wao wakijipendekeza watakuwa kwenye maisha salama, lakini viongozi ambao wamemwagwa hawapo ata bungeni ukiwafata uwaambie JPM aongezewe Muda usipokuwa makini wanaweza kukupiga makofi mfano mfate lugola alafu mwambie JPM tumpe milele bhana kama hatokutukana, kwahyo wale wanaoshupalia ni wale ambao wananufaika nae tu ila mzee baba hakuna anaempenda watu washamchoka.

^^^^^^^^^^
Mambo ambayo akiyafanya Rais magufuli Watanzania wenyewe bila kushurutishwa watamlilia na kuandamana barabarani kuomba Rais Magufuli aongezewe muda wa kutawala ata milele.

1. Kuongeza nyongeza ya mishahara na kupandisha madaraja kwa watumishi wa umma. (hawa watu wametaabika na wana hali mbaya sana kwa muda wa miaka 6 sasa mpka barabarani wanajiongelesha wenyewe kwa stress, Magu akitaka apate mapambio ya kuongezewa muda wa kutawala basi hawa watu awapandishe mishahara kwa asilimia kubwa % na kuwalipa madeni yao wataongoza kumsifu na kumshinikiza).

2. Kuajiri vijana waliopo mtaani. (siku hizi wahitimu wa vyuo wamejaa mtaani kama njugu vile hawana kazi yoyote ile, sio walimu, sio manesi, madokta, bwana mifugo n.k, hili kundi ni kubwa mnoo na linaongoza kumchukia magufuli vibaya mno adi kutamani Mungu angempenda zaidi mana mtaani wanataabika hatari, vijana hawa hawana ata familia lakini wanaongoza kuwa na msongo wa mawazo).

3. Wastaafu kulipwa pesheni zao. (hapa wazee wengi wanasononeka na kushikwa na hasira mtu amemaliza kutumikia taifa lakini haki yake mwenyewe anazungushwa mpaka anakata tamaa, mzee kastaafu ila ana miaka mitano bado hajapewa pesa zake hayo mapenz yakutaka rais aongezewe muda wa kutawala atayatolea wapi!! Hawa ni wengi mnoo wengine mpaka wanakufa wamekosa stahiki zao.)

4. Wafanyabiashara kupunguziwa kodi za hovyo zinazowapekea kufunga biashara zao.

5. Wakulima wa korosho kulipwa pesa zao. (hawa watu sio tu kuwa wana hasira na huyu bali wana kisasi kikali san na ukitaka kujua machungu yao uwakute wanaongea kikabila, kiasi kwamba wanamuombea majaliwa angalau aje kuwa Raisi ili apunguze machungu ya watu wake wa kusini.)

6. Wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu kupunguziwa riba.

7. Wakulima kutafutiwa masoko ya uhakika na kupunguziwa gharama za pembejeo.

8. Kuzuia mfumuko wa bei kwa bidhaa mbalimbali. Mf. Mafuta, sukar, cement.

9. Mikopo himilivu kwa vijana na wanawake.

10. Bima bora za afya kwa Watanzania.

11. Kuhamasisha Matajiri duniani kuwekeza viwanda mbalimbali Tanzania.

Mh Raisi akiyafanya hayo bila chuki wala roho mbaya Watanzania wenyewe wataamua na kumshinikiza kwa maandamano atawale ata milele hadi afie ikulu.

~Gai da Seboga

Haya uliyoandika ni wajibu kwa rais yoyote, na sio majukumu ya ziada mpaka useme akifanya anastahili kuongezewa muda wa kukaa madarakani. Tunapaswa kila rais anayeingia madarakani atekeleze mambo haya maana sio hisani.
 
Mh Raisi akiyafanya hayo bila chuki wala roho mbaya Watanzania wenyewe wataamua na kumshinikiza kwa maandamano atawale ata milele hadi afie ikulu.
Haya ndiyo matatizo ya waTanzania hawa.

Unaacha mambo ya msingi unarukia peremende? Utamu wa peremende utakufikisha wapi?

Hayo yoooote uliyoyaorodhesha hapo kuwa ndio yatakayomfanya akubalike ni mambo ya kitaratibu, yasiyohusu uamzi wa mtu mmoja.

Mwambie aruhusu taratibu zilizopo zifanye kazi, mengi ya hayo utayapata; huhitaji kwenda kupiga magoti kwa yeyote.

Afuate katiba na sheria zake,...HAKI itapatikana kwa kila mmoja.

Angefanya hivyo toka mwanzo, hata sehemu ambazo zingekuwa ngumu kuzitekeleza kwa kukosa uwezo, watu wangeelewa na wasingemlaumu yeye binafsi.

Mada yako ni ya kulambisha watu sukari. Utamu unakwisha, unarudi palepale pa mwanzo.
 
11) Kuendesha uongozi wa kilaghai na udanganyifu kama vile kuwadanganya wananchi kuwa Tanzania hakuna corona kumbe dhamira yake ni kutokuwa tayari kutumia rasilimali za Taifa kunusuru maisha ya wananchi
Umeandika mambo mazito sana.

Na sasa maono yenye umuhimu kwake ni kufundisha historia, wala hawazii sayansi na teknologia! Tunarudi nyuma huku wenzetu wakienda mbio mbele. Tumepoteza sana, na tutajutia.

Great Thinker.
 
Habari zenu mabibi na mababu!

Kwanza kabisa ni ukweli usiopingika kuwa kwa sasa kila mtu anapoambiwa au kusikia kuongezewa muda wa kutawala Rais magufuli anashikwa na ghadhabu na kutamani ata kumpiga mtu ngumi kutokana na ugumu wa maisha uliopo.

Sio watumishi wa Serikali, sio wafanyabiashara, machinga, wastaafu, wanachuo, wahitimu wa chuo, mama ntilie, wachuuzi, n.k wote hawa hawataki kusikia ata kidogo msamiati wa Rais magufuli kuongezewa muda wa kutawala, wamemchoka vibaya mnoo kiasi kwamba mpaka wanajuta kwanini walimpa uraisi na bila kupepesa macho wanatamani ata kesho tu Amalize muda wake wa kutawala waangalie ustaarabu wa raisi ajae.

Na wale wanaoshupalia kuwa aongezewe ni wabunge ambao wapo bungeni wakiona hawana cha kupoteza kwamba akitawala milele basi wao wakijipendekeza watakuwa kwenye maisha salama, lakini viongozi ambao wamemwagwa hawapo ata bungeni ukiwafata uwaambie JPM aongezewe Muda usipokuwa makini wanaweza kukupiga makofi mfano mfate lugola alafu mwambie JPM tumpe milele bhana kama hatokutukana, kwahyo wale wanaoshupalia ni wale ambao wananufaika nae tu ila mzee baba hakuna anaempenda watu washamchoka.

^^^^^^^^^^
Mambo ambayo akiyafanya Rais magufuli Watanzania wenyewe bila kushurutishwa watamlilia na kuandamana barabarani kuomba Rais Magufuli aongezewe muda wa kutawala ata milele.

1. Kuongeza nyongeza ya mishahara na kupandisha madaraja kwa watumishi wa umma. (hawa watu wametaabika na wana hali mbaya sana kwa muda wa miaka 6 sasa mpka barabarani wanajiongelesha wenyewe kwa stress, Magu akitaka apate mapambio ya kuongezewa muda wa kutawala basi hawa watu awapandishe mishahara kwa asilimia kubwa % na kuwalipa madeni yao wataongoza kumsifu na kumshinikiza).

2. Kuajiri vijana waliopo mtaani. (siku hizi wahitimu wa vyuo wamejaa mtaani kama njugu vile hawana kazi yoyote ile, sio walimu, sio manesi, madokta, bwana mifugo n.k, hili kundi ni kubwa mnoo na linaongoza kumchukia magufuli vibaya mno adi kutamani Mungu angempenda zaidi mana mtaani wanataabika hatari, vijana hawa hawana ata familia lakini wanaongoza kuwa na msongo wa mawazo).

3. Wastaafu kulipwa pesheni zao. (hapa wazee wengi wanasononeka na kushikwa na hasira mtu amemaliza kutumikia taifa lakini haki yake mwenyewe anazungushwa mpaka anakata tamaa, mzee kastaafu ila ana miaka mitano bado hajapewa pesa zake hayo mapenz yakutaka rais aongezewe muda wa kutawala atayatolea wapi!! Hawa ni wengi mnoo wengine mpaka wanakufa wamekosa stahiki zao.)

4. Wafanyabiashara kupunguziwa kodi za hovyo zinazowapekea kufunga biashara zao.

5. Wakulima wa korosho kulipwa pesa zao. (hawa watu sio tu kuwa wana hasira na huyu bali wana kisasi kikali san na ukitaka kujua machungu yao uwakute wanaongea kikabila, kiasi kwamba wanamuombea majaliwa angalau aje kuwa Raisi ili apunguze machungu ya watu wake wa kusini.)

6. Wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu kupunguziwa riba.

7. Wakulima kutafutiwa masoko ya uhakika na kupunguziwa gharama za pembejeo.

8. Kuzuia mfumuko wa bei kwa bidhaa mbalimbali. Mf. Mafuta, sukar, cement.

9. Mikopo himilivu kwa vijana na wanawake.

10. Bima bora za afya kwa Watanzania.

11. Kuhamasisha Matajiri duniani kuwekeza viwanda mbalimbali Tanzania.

Mh Raisi akiyafanya hayo bila chuki wala roho mbaya Watanzania wenyewe wataamua na kumshinikiza kwa maandamano atawale ata milele hadi afie ikulu.

~Gai da Seboga
Hakika
 
Kuna mtu juzi alianzisha uzi unaosema kuwa watanzania wanatamani magari ambayo hayapo duniani; lisinywe mafuta, likimbie, vipuri viwe vya bure etc wewe sasa unatamani kodi zipunguzwe ila wanaotafuta ajira wote waajiriwe! Unataka nyongeza ya mshahara wakati kodi zimefutwa! It’s impossible my friend
Wapi nmesema kod zfutwe?? Kodi za sasa n kandamizi mpk biashara znafungwa. La ajabu n lipi wakt mara kibao anatwambia nchii hii ni tajiir, tuutumie utajiri wetu kufanya hayo.
 
Back
Top Bottom