Rais Kikwete ni extra ordinary

Rais Kikwete ni extra ordinary

Malisa Godlisten

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2010
Posts
202
Reaction score
1,588
Jana wakati akipokea Katiba pendekezwa ambayo inasubiri kwenda kupigiwa kura na wananchi, Rais Kikwete alisema hivi "Hatuwezi kusema kama tutaendelea na mchakato kwa sasa, au tatasitisha hadi mwakani kwa sababu mazungumzo bado yanaendelea."

Rais Kikwete aliitangazia dunia jana kuwa hata yeye hajui mchakato unaendelea lini, kama ni sasa au ni baada ya uchaguzi mwakani. Wengi walidhani Rais yupo sahihi kuwa hajui lini mchakato unaendelea. Ukweli ni kwamba Rais alitoa kauli ile ili kuondoa sintofahamu iliyopo kwny jamii kuhusu lini mchakato huu unaendelea.

Sintofahamu hii inatokana na kupingana kwa kauli za watu wawili ambao wote wanadai wametumwa na Rais Kikwete.

Wa kwanza ni Waziri, AshaRose Migiro aluyesema "Mchakato unaendelea kama kawaida, waTZ wajiandae kupiga kura ya maoni."

Wa pili ni Mzee John Cheyo aliyesema bungeni kuwa "Mchakato utasitishwa hadi baada ya uchaguzi mkuu mwakani".

Baada ya kauli ya Migiro na ya Cheyo kupingana, Rais Kikwete ameshindwa kuwa na msimamo. Ameogopa kuegemea upande wa Cheyo (aliyefanya nae mazungumzo Ikulu) au wa Migiro (aliyemteua). So ameamua kuwa "neutral" kwa kusena hajui mxhakato utaendelea lini, ili asimkwaze Migiro wala Cheyo.

MY TAKE.!
Miongoni mwa hasara kubwa tulizonazo watanzania ni pamoja na kuwa Rais asiye na msimamo. Sifa kubwa ya kiongozi bora ni kuwa na MSIMAMO na kuutetea msimamo huo hata kama utapingwa na wengi. Kama ni msimamo wenye maslahi kwa umma usimamie na usiyumbeyumbe. Hii itakujengea heshima kubwa hata utakapoondoka madarakani.

Mao Tse Tsung ni miongoni mwa viongozi waliokua na misimamo mikali sana. Na bahati mbaya misimamo yake mingi ilipingwa na wananchi wengi wa China.. lakini hakubadili misimamo yake licha ya kupingwa na wengi.. maana alijua ni misimamo yenye tija kwa taifa.. na leo China inanufaika sana na misimamo ileile ya Mao Tse Tung waliyoipinga zamani.

Hapa kwetu Rais Kikwete hana misimamo kwa sababu anapenda kuonekana mzuri kotekote. Hapendi kukwaza upande "A" wala upande "B". Anataka kote aonekane mwema.

Rais Kikwete wakati anahutubia jana alijua kabisa kuwa Waziri wake wa Sheria, Migiro alishasema mchakato unaendelea. Na alijua pia kuwa vyama vya siasa kupitia kwa mzee Cheyo vilishasema hadi mwakani baada ya uchaguzi.

Sasa Kikwete jana akaona akisema mchakato unaendelea ataonekana mbaya kwa kina Cheyo, na akisema unasitishwa hadi mwakani atatofautiana na waziri wake Migiro. Kwa hiyo eti akaamua kukaa katikati kwa kusema "mazungumzo yanaendelea". Ajabu sana hii. mazungumzo yapi? Na nani? Na yataendelea hadi lini?

Lakini tabia hii ya Rais Kikwete ya kupenda kuwa Padri na Imamu kwa wakati mmoja si ya jana wala juzi, nadhani ni ya kuzaliwa (inborn character). Maana mambo mengi sn amekuwa katikati hata yale ambayo alitakiwa kuonesha msimamo wake kama kiongozi mkuu wa nchi.

Wakati wa sakata Dowans Rais Kikwete aliwahi kusema "suala hili tulishaanza kuona lina walakini tangu mwanzo". Lakini Dowans hiyohiyo ilipojibadili jina kuwa Symbion, ni Kikwete huyohuyo aliyemualika Rais Obama na kwenda kuzindua mitambo. Akazindua mitambo ya watu walewale aliosema ameona wana "walakini" tangu mwanzo.

Tunashindwa tumueleweje Rais wetu. Si moto, si baridi. Si mweupe si mweusi. Hakubali wala hakatai. Rais asiye na msimamo.

Mwanafalsafa Plato aliwahi kusema "nothing can be and not be, at the same time in the same context"... Yani kitu hakiwezi kuwepo halafu tena kisiwepo kwa wakati huohuo na kwa namna hiyohiyo.

Yani huwezi kuwa mnene halafu tena ukawa mwembamba kwa wakati huohuo. Huwezi kuwa mweupe halafu tena ukawa mweusi kwa wakati huohuo...Mtu pekee duniani aliyeweza kuwa mnene na mwembamba kwa wakati mmoja... akawa mweusi na mweupe kwa wakati huohuo ni Rais wetu mtukufu Jakaya Kikwete. Our President is Extra Ordinary.!!

JIPU LIMEPASUKA, SIWEZI KUWA ADUI KWA KUSEMA UKWELI.!

Malisa GJ || Your Partner In Critical Thinking.!
 
Kikwete will be remembered as a worst president to ever happen in this planet since its creation, He has even surpassed Idd Amin as a worst President ever!What a wasted vote!!!
KIKWETE baba lao, kishawanyamazisha tayari, mliobaki ni mavuvuzela tu. Wengine tumeshamuelewa tunasubiri kumwaga kura za ndiyo kuikubali Katiba iliyopendekezwa
 
Mimi nina swali: hivi haya mapendekezo yatapigiwa kura na wananchi au ndo imepita hivyo?
 
KIKWETE baba lao, kishawanyamazisha tayari, mliobaki ni mavuvuzela tu. Wengine tumeshamuelewa tunasubiri kumwaga kura za ndiyo kuikubali Katiba iliyopendekezwa

Wewe ni wa jinsia gani?
Kama we ni wa kike ni halali kusema hayo kwa u-baba aliokuonesha ingawa hapa si mahali pake. Kama we ni wa kiume, basi ni bahati mbaya kuwa na tabia hiyo tusiyoipenda nchini, hata kama tutanyimwa misaada.
 
Binafsi niliisubiri hotuba yake tangia saa 12 asubuhi na nilivyoona nimepoteza siku nzima na betri zinaanza kuishiwa nguvu mida ya jioni nikazima redio lakini mtu kanishtua ndio nikaanza tena kusikiliza.
Nilikuwa nikisubiria muda wote wa hotuba kuwa kuna sehemu ataongea kama Rais wa Tanzania lakini mpaka hotuba inaisha mida ya saa mbili na nusu sikuhisi sehemu yoote kuwa hii ni hotuba ya kihistoria kama waandaa shrehe walivyoinasibu!
Baada ya kutafakari sana nikaona ni kama ile hotuba ya ufunguzi wa bunge la katiba ambapo alipoulizwa alisemaga kuwa 'alikuwa anatoa maoni' kitu kilichowashangaza wengi maana muda wa maoni ulishapita.
Nilichosikitika zaidi ni wazi JK na wenzake walijua kabisa hawana mpango na KATIBA MPYA na hata haya mabadiliko madogo wangeliweza kuyafanya kwa kutumia bunge la kawaida ambako wako wengi. Sasa ilikuwa ya nini kupoteza pesa za walipa kodi bila sababu ya msingi!???
 
Mimi nina swali: hivi haya mapendekezo yatapigiwa kura na wananchi au ndo imepita hivyo?

Ukweli ni kuwa CCM hawawezi kukubali kura ipigwe kabla ya Uchaguzi kwa sababu kubwa mbili, kwanza, wanajua wananchi hawajaridhishwa na huu mchakato na pia sasa hivi ukinzani ni mkubwa mno hata ndani ya chama kwenyewe, hivyo wanahitaji kuzua jambo jingine hapa kati kati ili kuhamisha public attention kutoka kwenye katiba kwenye huo upuuzi mwingine, tunaweza sikia rais anataka kupangua baraza la mawaziri (Lukuvi kesha lianzisha kwa Nyalandu), na sababu ya pili, hawana fedha ya kuhonga na kununua kadi za kupigia kura, hivyo they need time kukwapua fedha za kufanikisha uharamia wao.

CC Malisa Godlisten
 
Last edited by a moderator:
KIKWETE baba lao, kishawanyamazisha tayari, mliobaki ni mavuvuzela tu. Wengine tumeshamuelewa tunasubiri kumwaga kura za ndiyo kuikubali Katiba iliyopendekezwa
Jah Pipo.....
Sakata rumba, na usiposakata rumba tunakufukuza ukada.
 
Jana wakati akipokea Katiba pendekezwa ambayo inasubiri kwenda kupigiwa kura na wananchi, Rais Kikwete alisema hivi "Hatuwezi kusema kama tutaendelea na mchakato kwa sasa, au tatasitisha hadi mwakani kwa sababu mazungumzo bado yanaendelea."

Rais Kikwete aliitangazia dunia jana kuwa hata yeye hajui mchakato unaendelea lini, kama ni sasa au ni baada ya uchaguzi mwakani. Wengi walidhani Rais yupo sahihi kuwa hajui lini mchakato unaendelea. Ukweli ni kwamba Rais alitoa kauli ile ili kuondoa sintofahamu iliyopo kwny jamii kuhusu lini mchakato huu unaendelea.

Sintofahamu hii inatokana na kupingana kwa kauli za watu wawili ambao wote wanadai wametumwa na Rais Kikwete.

Wa kwanza ni Waziri, AshaRose Migiro aluyesema "Mchakato unaendelea kama kawaida, waTZ wajiandae kupiga kura ya maoni."

Wa pili ni Mzee John Cheyo aliyesema bungeni kuwa "Mchakato utasitishwa hadi baada ya uchaguzi mkuu mwakani".

Baada ya kauli ya Migiro na ya Cheyo kupingana, Rais Kikwete ameshindwa kuwa na msimamo. Ameogopa kuegemea upande wa Cheyo (aliyefanya nae mazungumzo Ikulu) au wa Migiro (aliyemteua). So ameamua kuwa "neutral" kwa kusena hajui mxhakato utaendelea lini, ili asimkwaze Migiro wala Cheyo.

MY TAKE.!
Miongoni mwa hasara kubwa tulizonazo watanzania ni pamoja na kuwa Rais asiye na msimamo. Sifa kubwa ya kiongozi bora ni kuwa na MSIMAMO na kuutetea msimamo huo hata kama utapingwa na wengi. Kama ni msimamo wenye maslahi kwa umma usimamie na usiyumbeyumbe. Hii itakujengea heshima kubwa hata utakapoondoka madarakani.

Mao Tse Tsung ni miongoni mwa viongozi waliokua na misimamo mikali sana. Na bahati mbaya misimamo yake mingi ilipingwa na wananchi wengi wa China.. lakini hakubadili misimamo yake licha ya kupingwa na wengi.. maana alijua ni misimamo yenye tija kwa taifa.. na leo China inanufaika sana na misimamo ileile ya Mao Tse Tung waliyoipinga zamani.

Hapa kwetu Rais Kikwete hana misimamo kwa sababu anapenda kuonekana mzuri kotekote. Hapendi kukwaza upande "A" wala upande "B". Anataka kote aonekane mwema.

Rais Kikwete wakati anahutubia jana alijua kabisa kuwa Waziri wake wa Sheria, Migiro alishasema mchakato unaendelea. Na alijua pia kuwa vyama vya siasa kupitia kwa mzee Cheyo vilishasema hadi mwakani baada ya uchaguzi.

Sasa Kikwete jana akaona akisema mchakato unaendelea ataonekana mbaya kwa kina Cheyo, na akisema unasitishwa hadi mwakani atatofautiana na waziri wake Migiro. Kwa hiyo eti akaamua kukaa katikati kwa kusema "mazungumzo yanaendelea". Ajabu sana hii. mazungumzo yapi? Na nani? Na yataendelea hadi lini?

Lakini tabia hii ya Rais Kikwete ya kupenda kuwa Padri na Imamu kwa wakati mmoja si ya jana wala juzi, nadhani ni ya kuzaliwa (inborn character). Maana mambo mengi sn amekuwa katikati hata yale ambayo alitakiwa kuonesha msimamo wake kama kiongozi mkuu wa nchi.

Wakati wa sakata Dowans Rais Kikwete aliwahi kusema "suala hili tulishaanza kuona lina walakini tangu mwanzo". Lakini Dowans hiyohiyo ilipojibadili jina kuwa Symbion, ni Kikwete huyohuyo aliyemualika Rais Obama na kwenda kuzindua mitambo. Akazindua mitambo ya watu walewale aliosema ameona wana "walakini" tangu mwanzo.

Tunashindwa tumueleweje Rais wetu. Si moto, si baridi. Si mweupe si mweusi. Hakubali wala hakatai. Rais asiye na msimamo.

Mwanafalsafa Plato aliwahi kusema "nothing can be and not be, at the same time in the same context"... Yani kitu hakiwezi kuwepo halafu tena kisiwepo kwa wakati huohuo na kwa namna hiyohiyo.

Yani huwezi kuwa mnene halafu tena ukawa mwembamba kwa wakati huohuo. Huwezi kuwa mweupe halafu tena ukawa mweusi kwa wakati huohuo...Mtu pekee duniani aliyeweza kuwa mnene na mwembamba kwa wakati mmoja... akawa mweusi na mweupe kwa wakati huohuo ni Rais wetu mtukufu Jakaya Kikwete. Our President is Extra Ordinary.!!

JIPU LIMEPASUKA, SIWEZI KUWA ADUI KWA KUSEMA UKWELI.!

Malisa GJ || Your Partner In Critical Thinking.!
Ni moja ya majanga makubwa yaliyowahi kulikumba taifa hili kaka.
 
Mimi kweli sipendi siasa za tanzania. Nilitarajia kingekuwa ni kitu kidogo kabisa.

1. Kupokea mapendekezo

2. Kuwashukuru wana kamati

3. Kuwasisitiza wananchi kuipokea na kuisoma kwa MAKINI kuona kama kila hitaji lao limeguswa bila kujali wajumbe wanavyoinadi. Wasiwasikilize wajumbe waisome tena wao wenyewe wananchi. Kila kipengele wanachodhan kinagusa maisha yao..je kipo? Kipo wanavyokitaka kiwepo?

4. Wajitokeze kwa wingi kupiga kura. Haijalishi ni ndiyo ama hapana. Wapige kutokana na upeo wao wa rasimu hiyo na chochote kitakachoamuliwa nao kitakuwa final maana si katiba ya wajumbe ni katiba ya wananchi.

5. Mungu ibariki Afrika. Mungu ibariki Tanzania. Asanteni kwa kunisikiliza.

Duration: 30 minutes
 
Kuna watu wanaweweseka sana. Ukweli ni kwamba, whether kura ya maoni itabigwa kabla au baada ya uchaguzi, bunge maalum limetimiza wajibu wake na hatua hiyo haitarudiwa
 
Mimi kweli sipendi siasa za tanzania. Nilitarajia kingekuwa ni kitu kidogo kabisa.

1. Kupokea mapendekezo

2. Kuwashukuru wana kamati

3. Kuwasisitiza wananchi kuipokea na kuisoma kwa MAKINI kuona kama kila hitaji lao limeguswa bila kujali wajumbe wanavyoinadi. Wasiwasikilize wajumbe waisome tena wao wenyewe wananchi. Kila kipengele wanachodhan kinagusa maisha yao..je kipo? Kipo wanavyokitaka kiwepo?

4. Wajitokeze kwa wingi kupiga kura. Haijalishi ni ndiyo ama hapana. Wapige kutokana na upeo wao wa rasimu hiyo na chochote kitakachoamuliwa nao kitakuwa final maana si katiba ya wajumbe ni katiba ya wananchi.

5. Mungu ibariki Afrika. Mungu ibariki Tanzania. Asanteni kwa kunisikiliza.

Duration: 30 minutes
Mkuu, kwani speech ya JK imetumia dakika ngapi?
 
Kuna mahali alisema, "...kama kuna mtu atakaye ona mapungufu kwenye hii katiba basi ana matatizo..."

Alitaka kumaanisha wale watakao/waliopiga kura za hapana ni punguani au?

I mean siungi mkono siasa za CCM wala siungi mkono siasa za CHADEMA (in my view ziko immature sana) ..so siko ki ccm wala kichadema hapa.

Ila kama raia tu wa Tanzania nahisi ameutukana umma wa Watanzania wenye haki kikatiba ya kupiga kura na kusema Hapana.

It sounded like alikuwa anahutubia wajumbe wa NEC.

anyway...I have a dream aiku moja Tanzania tutajifunza siasa inayoangalia maslahi ya umma badala ya mambo binafsi na kufahamika.

I have a dream siku moja mtu atasimama na kuitetea nchi yake kabla ya chama chake.

I have a dream siku moja tutampima mtu kwa akisemacho na akitendacho bila kuangalia ametokea chama gani.

I have a dream...and one day yes!

It has started with me...

Mungu ibariki Afrika. Mungu ibariki Tanzania
 
Mchakato ni mwaka huu huu,yale mazungumzo ya kusitisha mpaka mwakani,yaliexpire baada ya ukawa kuendelea na harakati za kuandamanisha watu licha ya kuwa walikubaliana bunge lisite tarehe 4 october.
jiandaeni kwa kura ya maoni mwezi dicember.
 
Kuna mahali alisema, "...kama kuna mtu atakaye ona mapungufu kwenye hii katiba basi ana matatizo..."

Alitaka kumaanisha wale watakao/waliopiga kura za hapana ni punguani au?

I mean siungi mkono siasa za CCM wala siungi mkono siasa za CHADEMA (in my view ziko immature sana) ..so siko ki ccm wala kichadema hapa.

Ila kama raia tu wa Tanzania nahisi ameutukana umma wa Watanzania wenye haki kikatiba ya kupiga kura na kusema Hapana.

It sounded like alikuwa anahutubia wajumbe wa NEC.

anyway...I have a dream aiku moja Tanzania tutajifunza siasa inayoangalia maslahi ya umma badala ya mambo binafsi na kufahamika.

I have a dream siku moja mtu atasimama na kuitetea nchi yake kabla ya chama chake.

I have a dream siku moja tutampima mtu kwa akisemacho na akitendacho bila kuangalia ametokea chama gani.

I have a dream...and one day yes!

It has started with me...

Mungu ibariki Afrika. Mungu ibariki Tanzania
Mkuu hiyo signature yako umeandika kwa kichagga cha ndani ndani sana
 
Hata ile chembe ya imani niliyokuwa nimeibakiza kwa JK imeondoka kabisa, nimeanza kuwaamini wale waliosema Rais wetu ni 'msanii'.

Kwa sasa hainishangazi tena, CCM ipo jinsi ilivyo kwa sababu yake-kuna OMBWE LA UONGOZI. Hata Tanzania yetu iko hivi kwa sababu hiyo hiyo-Ujanjaujanja, Usanii na Ombwe la Uongozi.

CCM ilianza kuparanganyika baada ya wafanyabiashara kuingia,kununua na kuwaweka watu wao, wale viongozi wachache walibaki kuwa viongozi wenye miiko ya Uongozi ndani ya CCM kama kina Mzee Mangula wamezidiwa na wamechoka.

Vv
 
Malisa Godlisten, asante kwa uchambuzi makini umejitahidi na umeweza.

Ila kubwa ambalo umezunguka sana katika kulibainisha ni kwamba Rais wetu kwa hakika kabisa anasumbuliwa na kikubwa ambacho kwa kweli hawezi kukiepuka kwasababu ni asili tangu kuzaliwa kwake hivyo hata aende shule gani ya kujifunza ujasiri hawezi kufaulu tatizo hili linalomkabili. Tatizo kubwa kwa Presidentt wetu ni UDHAIFU,DHAIFU na UDHAIFU, hakuna kingine

Mtu ambaye haelewi anahitaji nini kwa wakati gani na kuhitaji kila kitu kwa wakati wote!! Huyo kwa asili ni Mdhaifu kwasababu anatamani kila kitu asichokuwa nacho na kutaka kufanya kila kitu asichokuwa na uwezo wa kukifanya sawia na hata wale wanaotaka kukifanya sawia hataki wakifanye. Anaishia kuvulunda kila mahali anakopita na kwasababu ya UDHAIFU wake haoni ajabu KUVURUGA hata lile alilokwisha VURUGA kwakuwa kila kitu yeye kinawezekana

BACK TANGANYIKA
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom