Rais Kikwete, kutimua Mawaziri wezi si uamuzi mgumu

Mjomba wa taifa

JF-Expert Member
Apr 20, 2012
231
161
Kumekuwa na taarifa mbalimbali toka pembe zote nchini Tanzania kuwa Rais Jakaya Kikwete anatarajia kuchukua "MAAMUZI MAGUMU" ya kuwafukuza kazi Mawaziri walitaojatwa katika sakata la ESCROW pia kuwapumzisha kazi Mawaziri wote ambao wametajwa kuwa ni Mizigo kama vile Christopher Chiza.

Sidhani kama wanaosema maneno haya wametafakari zaidi kuhusu Raisi Kuchukua Maamuzi Magumu. Hivi kweli ndugu zangu, wabadhilifu waliotajwa mpaka leo bado wapo Ofisini wengine wanasafiri nje za nchi bado wanakula posho za nchi, Rais mpaka leo anajivuta kuchukua uamuzi?

Kwa mujibu wa sheria za kazi za nchi, mfanyakazi anapotuhumiwa kwa ubadhilifu ama wizi wowote kazini, husimamishwa kazi (SUSPENSION) huku akiendelea kulipwa mshahara wake kama kawaida ili kupisha uchunguzi ufanyike kubaini ukweli wa tuhuma. Na ndivyo imekuwa ikifanyika kwa watumishi wote Sekta binafsi na za Umma. Sasa mpaka leo mabwana hawa bado wapo ofisini licha ya tuhuma zinazowakabili ili waendelee kupiga dili zingine kumalizia miezi 9 ya JK kuwa madarakani.

Kinachosaidia hapa ni mashinikizo mbalimbali toka mataifa ya Magharibi ya kuinyima Tanzania misaada ya kifedha ndo maana matamko toka Ikulu chini kwa chini tunasikia Rais anatarajia kufanya MAAMUZI MAGUMU. Sitampinga Mbunge wa Ubungo John Mnyika aliposema tumefika hapa kwa kuwa RAIS ni dhaifu iwapo CCM na Ikulu bado itaamini kuwafukuza mafisadi uwaziri ni "MAAMUZI MAGUMU".

Kama hatujui UAMUZI MGUMU ni bora tukae kimya au tusome historia ya baadhi ya MAAMUZI MAGUMU ikiwemo kutaifisha taasisi zote za watu binafsi uamuzi uliofanyika baada ya Uhuru. Maamuzi mengine Magumu ni yale ya Wazi, ri Mkuu Marehemu Sokoine ya kukamata Wahujumu uchumi, hali iliyopelekea wahujumu uchumi kukimbia mali zao.

Kwa hili la kuwafukuza mawaziri wezi si MAAMUZI MAGUMU hata kidogo, na hata kama itatokea Raisi akawafukuza wezi hawa wala hatoingia katika orodha ya viongozi waliowahi kufanya MAAMUZI MAGUMU TANZANIA. Labda afanye kwa kujiburudiasha tu. Alikuwa na Uwezo wa kufanya MAAMUZI MAGUMU toka alipochaguliwa mwaka 2005 ambapo wananchi wengi nikiwemo mimi tuliingia mkenge kwa kuhadaika na mwonekano wake tukadhani atakuja kufanya MAAMUZI MAGUMU kumbe anakuja kutafuta udaktari na uprofessor wa kutembelea nchi nyingi duniani kama Vasco Dagama.
 
Kama anataka kuingia kwenye record ya ma-rais waliowahi kufanya maamuzi magumu, basi waliohusika wote wakamatwe na mali zao kutaifishwa ikiwa ni pamoja na ku-seize account zao. Hapo atatoa fundisho kwa wengine wanaofikiria kufanya hivyo. Hii ni pamoja na kumkamata Singa Singa na kutaifisha mitambo. Hii haihitaji kuiachia mahakama kutoa hukumu bali yawe ni maamuzi ya baraza la mawaziri
 
Mimi ninavyoona maamuzi magumu ni kuwaacha watuhumiwa madarakani kuliko kuwatoa maana kama katiba ingeruhusu wangekuwa washawajibika wenyewe ila kuwatoa ni kawaida kama bosi kumfukuza mfanyakazi wake.

Kumbuka kuwaacha waendelee na kazi ndio maamuzi magumu kuliko kuwatimua ni kama kumtetea kibaka aliyekamatwa na kidhibiti
 
Rais anaweza kikatiba kumteua au kumwondoa waziri wakati wowote kadri avyoona inafaa.Wala halazimiki kutoa sababu.Ukiacha mambo ya ufisadi anaweza kumwondoa au kuwaondoa mawaziri ili kuongeza ufanisi katika serikali.
Pamoja na uwezo huo kikatiba,ni vigumu kumwondoa waziri kwa ufisadi kama yeye ni sehemu ya ufisadi huo.Ndio maana hakuwahi kuwa ngumu kwa Nyerere kumtema waziri yeyote.
Katiba yetu mbovu inampa uhuru wa kuamua idadi ya wizara. Kwa wenzetu Rais hana madaraka hayo kwani idadi ipo kwenye katiba ya nchi. Kunakuwa na kikomo .
Haitaji ujasiri kumtema waziri kama Rais ni msafi.
 
Maamuzi magumu waachiwe kina Kagame ndiyo maana nchi kama Rwanda inapiga hatua
 
Kama anataka kuingia kwenye record ya ma-rais waliowahi kufanya maamuzi magumu, basi waliohusika wote wakamatwe na mali zao kutaifishwa ikiwa ni pamoja na ku-seize account zao. Hapo atatoa fundisho kwa wengine wanaofikiria kufanya hivyo. Hii ni pamoja na kumkamata Singa Singa na kutaifisha mitambo. Hii haihitaji kuiachia mahakama kutoa hukumu bali yawe ni maamuzi ya baraza la mawaziri

Kwa Rais makini na asiye fisadi kumteua au kumtosa waziri ni uamuzi wa kawaida na si uamuzi mgumu.
 
Namshauri Rais wangu msikivu amteue Mh Tundu Lissu kwenye Baraza lake jipya la Mawaziri......itamsaidia sana......
 
Tatizo akivunja baraza hana watu tena Maskini ambao anaweza kuwaingiza just take a minute ku study wabunge waCCM waliopo sasa nani ambae anaweza kua waziri? Yani anajuuuuuuuuuuta kua Rais ndo maana ktk rasim ya katiba waTz walipendekeza mawaziri wasitokane na Wabunge
 
Richmond rais alihusika ,escrow rais anahusika ,bado mnategemea atafanya nini ,mawaziri wasasa hivi wamemshtukia, hana lolote ndio maana hawajiuzulu kila mtu anamchek, na wamejifunza kutoka kwa lowasa kule kujiuzulu kwake ilikua ni kosa la kiufundi, aondoke na yeye anahusika ,hii mambo ya kumbeba rais mpaka lini, halafu rais mwenyewe anaebebwa sasa habebeki aaah
 
Richmond rais alihusika ,escrow rais anahusika ,bado mnategemea atafanya nini ,mawaziri wasasa hivi wamemshtukia, hana lolote ndio maana hawajiuzulu kila mtu anamchek, na wamejifunza kutoka kwa lowasa kule kujiuzulu kwake ilikua ni kosa la kiufundi, aondoke na yeye anahusika ,hii mambo ya kumbeba rais mpaka lini, halafu rais mwenyewe anaebebwa sasa habebeki aaah

Ila kwa hili jamaa kabanwa na nchi wahisani lazima atachukua hatua tu, anachofanya ni just delay of time......M C C juzi walianza kupigwa mikwara na jana World Bank wakakazia kabisa
 
TANZANIA BWANA INANIBURUDISHA SANA KAMA MOVIE HIVI NAJARIBU KUFIKIRI KAMA HILI SWALA LINGEMKUTA RAISI KAGAME , ENZI HIZO INGEMKUTA SOKOINE INHEKUWA BADO TUNAJADILI AU TUNGEKUWA TUMESHAZIKA TUNAENDELEA NA MAMBO YA MSINGO NA HAO WANAOTETE uozo wangekuwa kimyaaaaa lakini Leo wanajua wakitetea wezi wanaonekana Mashujaa shame to all of you.
 
Kama anataka kuingia kwenye record ya ma-rais waliowahi kufanya maamuzi magumu, basi waliohusika wote wakamatwe na mali zao kutaifishwa ikiwa ni pamoja na ku-seize account zao. Hapo atatoa fundisho kwa wengine wanaofikiria kufanya hivyo. Hii ni pamoja na kumkamata Singa Singa na kutaifisha mitambo. Hii haihitaji kuiachia mahakama kutoa hukumu bali yawe ni maamuzi ya baraza la mawaziri
Unafikiri ni rahisi kumkamata huyo singasinga na kuitaifisha kiwanda yake kwa maamuzi ya baraza la mawaziriwewe upo dunia gani, hii karne nyengine hatupo Somalia. Nchi yetu inaendeshwa kisheria, Chombo ambacho kinaweza toa amri ya kukamatwa kiwanda au kutaifisha na kukamatwa kwa huyo singasinga ni mahakama.
 
Richmond rais alihusika ,escrow rais anahusika ,bado mnategemea atafanya nini ,mawaziri wasasa hivi wamemshtukia, hana lolote ndio maana hawajiuzulu kila mtu anamchek, na wamejifunza kutoka kwa lowasa kule kujiuzulu kwake ilikua ni kosa la kiufundi, aondoke na yeye anahusika ,hii mambo ya kumbeba rais mpaka lini, halafu rais mwenyewe anaebebwa sasa habebeki aaah

229073_10150178384733316_6446847_n.jpg

Kipanya aliiona zamani hii..
 
Kama hatujui UAMUZI MGUMU ni bora tukae kimya au tusome historia ya [COLOR=#ff0000 said:
baadhi ya MAAMUZI MAGUMU ikiwemo kutaifisha taasisi zote za watu binafsi[/COLOR] uamuzi uliofanyika baada ya Uhuru. Maamuzi mengine Magumu ni yale ya Wazi, ri Mkuu Marehemu Sokoine ya kukamata Wahujumu uchumi, hali iliyopelekea wahujumu uchumi kukimbia mali zao.

Hapo huyajuwi vizur na ni siri kwa wengi lakini ukweli ni kwamba, raia wote wa Uropa na US "waliotaifishwa" walilipwa thamani ya mali zao, waliodhulumiwa "taifishwa" kiukweli ni Waasia, ambao kama si wote basi wengi wao hawakulipwa.

Kuna kisa cha kutaifishwa Tiny Rowlands aka LONRHO ambapo Nyerere alidhani kuwa huyo ni Mkaburu kumbe ni Mwingereza mwenye influence kubwa sana, akamtaifisha kibabe, sakata alilokumbana nalo Nyerere mwenyewe akarudisha mali za Tiny.

Usidanganyike na usidanganye kwa usiyoyajuwa.

Tiny in name not in nature - BBC


Hata iweje, kudhulumu haijawahi kuwa maamuzi magumu.
 
Unafikiri ni rahisi kumkamata huyo singasinga na kuitaifisha kiwanda yake kwa maamuzi ya baraza la mawaziriwewe upo dunia gani, hii karne nyengine hatupo Somalia. Nchi yetu inaendeshwa kisheria, Chombo ambacho kinaweza toa amri ya kukamatwa kiwanda au kutaifisha na kukamatwa kwa huyo singasinga ni mahakama.
Mahakama gani! Hii inayotumiwa na ccm kama toilet pepa? Kikwete akiamua kutaifisha mitambo ya IPTL na kumkamata Singasinga ananyanyua simu tu na kumpigia chande kwisha habari. Kwa mfumo mbovu uliopo kuna mteuliwa wa raisi anaweza kwenda kinyume na rais? Ndio maana ccm wameikanyaga ovyo rasimu katiba kwasababu wanajua katiba iliyopo ndio inawaweka madarakani kwa sasa, mwenyekiti wao anapiga simu tu kwa wateuliwa wahakikishe ccm iko salama. Somalia inaheshimu zaidi katiba na sheria zake kuliko TZ, kinachowashinda ni kuwa na taasisi za ulinzi zenye nguvu.
 
Hapana hayo ni maamuzi magumu kwani unawezaje kumfukuza mtu kazi kwa wizi uliomtuma kuiba. Mama anawezaje kumkemea mtoto kwa mimba asiyoitarajia iwapo mama mwenyewe alikuwa akimkuwadia?? Vivyo hivyo uamuzi wa JK kuwatosa mafisadi ni mgumu sana mana kwa mujibu taarifa zisizo rasmi ni kwamba naye ni mbia mkubwa kama si mmiliki wa IPTL.
 
Too much jamani,, uwiiii "cjui kama huyu raisi anawashauri,, ndo maana inaniingia kwamba" ilulu ilihusika na ufisadi " aondoke tuu madarakani katutia hasara za kutosha,,, bado hyo mikataba ya gesi nayo itakua kiliooo
 
Back
Top Bottom