Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,552
Rais Kikwete.
Wafadhili wameamua kupunguza fungu lao la pesa linalokuja kwenye bajeti yetu. Wameteoa masharti na vitisho ambavyo vyaonekeana wazi kuwa wanachotaka kutoka kwa Tanzania pamoja na kuonekana kuwa ni nia nzuri kama vile kupiga vita ufisadi, lakini wanataka mazingira mazuri ya uwekezaji ambayo tafsiri yake rahisi sana ni kuwa Tanzania iruhusu Wawekezaji waendeleze unyonyaji na kuivuna Tanzania kwa utashi na manufaa yao na si kwa manufaa ya Watanzania na Tafa letu.
Je unajiandaa vipi kukabiliana na upungufu huo? Je utakimbilia kutafuta Wafadhili wengine, utalegeza masharti yetu kwa ajili ya manufaa na maslahi ya Taifa letu ili kukidhi masharti ya Wafadhili ili watuongezee huko tujisenti au utasimama kidete na kuing'oa Tanzania kutoka mfumo tegemezi?
Bajeti ya Serikali yetu inategemea asilimia 40 ya fedha za Matumizi na Maendeleo kutoka kwa misaada ya Wafadhili na mashirika ya fedha ya kimataifa.
Tafsiri nyepesi sana ni kuwa sisi ni nchi huru kwa asilimia 60, asilimia 40 iliyobakia bado iko mikononi mwa wakoloni.
Ningependa sana ulisome tena Azimio la Arusha na ujiulize ni kipi wewe binafsi an CCM mmeendelea kukosea na hivyo kupoteza asilimia 40 ya Uhuru wetu?
Labda nikupe dokezo la kukupa faraja ili ufanye maamuzi kwa manufaa na maslahi ya Watanzania na si kukimbilia matakwa ya Mkoloni na vyombo vyake vya fedha.
Serikali ya Australia, ambayo ni nchi mmoja inayotupa misaada sana, imeongeza viwango vya mapato kwa makampuni yanayofanya uchimbaji wa madini na nishati na kuweka kiwango cha mapato na kodi kwa ni asilimia 40 ya mapato ya uchimbaji wa Madini, Mafuta, Gesi na aina zote za nishati.
Hugo Chavez, Lous Lula na hata Kabila na Kagame na viongozi wengi wa Dunia ya Pili na ya Tatu, wameamua kulinda maslahi ya nchi zao kwa kuongeza viwango vya kodi na mapato kwa Wawekezaji wa nje ili nchi hizi iachane na tabia ya mazoea ya kutegemea misaada na mikopo kujiendesha.
Kinachonishangaza mimi ni kuwa huu ni mwaka 2010, Tanzania hatujawa na ulazima wa kutumia Rasilimali zetu kwa lengo mmoja la kukamua Hazina yetu kama tulivyofanya mwaka 1978 tulipoingia vita na Uganda.
Ni mwaka 2010, Afrika Kusini iko huru na kila nchi inayotuzunguka iko huru pamoja na kuwa kuna chokochoko za ndani lakini ukweli ni kuwa ndoto za Tanzania kuvamiwa ni ndogo mno.
Sasa kama kwa miaka 25 tumeishi kwa Amani, Utulivu na Mshikamano, iweje tushindwe kujijenga kikamilifu na kuachana na Utegemezi wa misaada na hata kuendelea kuunadi uhuru wetu kwa hiyo asilimia 40 tunayowapa Benki ya Dunia, Nchi wafadhili na Wawekezaji?
Kwa nini chama chako CCM na Serikali yake vina kigugumizi cha kuleta mapinduzi ya uzalishaji mali ambao utalenga kumnufaisha Mtanzania na si mwekezaji?
Je ushajiuliza kama tungefuata mkondo na mfano wa Australia na kuongeza pato la Taifa kutoka wka Wawekezaji kutoka asilimia 4 hadi asilimia 40 ni mapato ya kiasi gani tungepata na ni miradi mingapi ya maendeleo tungeweza kuigharamia wenyewe?
Ikiwa ulikiri kuwa Asilimia 30 ya Bajeti yetu inapotea katika Rushwa, je huoni kama ukiziba kabisa mianya ya Rushwa na Ufisadi na hata kuongeza pato la Taifa kwa asilimia hata 25, Tanzania inaweza kuwa nchi inayojitegemea kabisa miaka 10 kutoka leo?
Ulipochaguliwa 2005, wengi walitegemea ungekuwa Gorbachev wetu ambye utaleta mapinduzi ya fikra na uzalishaji mali, mapinduzi ambayo yangeiondoa Tanzania kutoka utegemezi.
Lakini kinachoonekana ni kuwa umeendeleza demokrasia ya kujieleza kwa watu, lakini wanachokuambia, wanacholalamikia hata kukutukana kinaingia sikio moja na kutokea lingine na kasi yako ni kuiingiza Tanzania katika uchumi tegemezi na si ajabu kuongeza wigo wa utegemezi kwa kuuza asilimia zaidi za uhuru wetu kwa kisingizio chako cha kutuingiza katika soko huria au kama aliyekutangulia Rais Mkapa aliyekuwa akituhubiria Utandawazi na kutupumbaza na vijideni tulivyofutiwa huku akiruhusu misahama ya kodi na mapato na kuuza kila rasilimali kwa bei chee!
Uamuzi wa Wafadhili kupunguza misaada kwenye bajeti yetu isikupe kizunguzungu au shinikizo. Ningekuwa mimi wewe, ningeita timu ifanye kazi ya kuziba mwanya huo wa mapato kwa kuongeza pato la Taifa na kuiga walichofanya Australia!
Mara nyingine Ukarimu wako unafadhaisha, majuzi kwenye mkutano wa WEF ulikaririwa ukiwaita WB, IMF na nchi wafadhili eti wao ni Wakubwa, je unyonge wako na kujisalimisha kwa wanaotunyonya utakoma lini?
Tunajua wazi kuwa Takrima, Rushwa na Ufisadi ni vitu vigumu sana kwako kuvishinda, wewe CCM na Serikali yako mmenogewa sana na Takrima na Rushwa. Basi tunakupa Ruksa, kaa na hiyo Takrima yako, ipunguze kutoka asilimia 30 hadi 15, lakini ongeza pato la Taifa kwa kila sekta ambayo mwekezaji kaweka mguu kutoka asilimia 3 hadi asilimia 40. Zaidi ya hilo toa sharti la kutaka Wawekezaji watumie malighafi, nguvukazi na kila aina ya nyenzo kwa kutumia kinachopatikana Tanzania. Ama futa misamaha yote kwa Wawekezaji wote kutoka nje ya nchi na hata wa ndani ya nchi walio na ubia.
Uamuzi ni wako Mheshimiwa Rais, kusuka au kunyoa!
Wafadhili wameamua kupunguza fungu lao la pesa linalokuja kwenye bajeti yetu. Wameteoa masharti na vitisho ambavyo vyaonekeana wazi kuwa wanachotaka kutoka kwa Tanzania pamoja na kuonekana kuwa ni nia nzuri kama vile kupiga vita ufisadi, lakini wanataka mazingira mazuri ya uwekezaji ambayo tafsiri yake rahisi sana ni kuwa Tanzania iruhusu Wawekezaji waendeleze unyonyaji na kuivuna Tanzania kwa utashi na manufaa yao na si kwa manufaa ya Watanzania na Tafa letu.
Je unajiandaa vipi kukabiliana na upungufu huo? Je utakimbilia kutafuta Wafadhili wengine, utalegeza masharti yetu kwa ajili ya manufaa na maslahi ya Taifa letu ili kukidhi masharti ya Wafadhili ili watuongezee huko tujisenti au utasimama kidete na kuing'oa Tanzania kutoka mfumo tegemezi?
Bajeti ya Serikali yetu inategemea asilimia 40 ya fedha za Matumizi na Maendeleo kutoka kwa misaada ya Wafadhili na mashirika ya fedha ya kimataifa.
Tafsiri nyepesi sana ni kuwa sisi ni nchi huru kwa asilimia 60, asilimia 40 iliyobakia bado iko mikononi mwa wakoloni.
Ningependa sana ulisome tena Azimio la Arusha na ujiulize ni kipi wewe binafsi an CCM mmeendelea kukosea na hivyo kupoteza asilimia 40 ya Uhuru wetu?
Labda nikupe dokezo la kukupa faraja ili ufanye maamuzi kwa manufaa na maslahi ya Watanzania na si kukimbilia matakwa ya Mkoloni na vyombo vyake vya fedha.
Serikali ya Australia, ambayo ni nchi mmoja inayotupa misaada sana, imeongeza viwango vya mapato kwa makampuni yanayofanya uchimbaji wa madini na nishati na kuweka kiwango cha mapato na kodi kwa ni asilimia 40 ya mapato ya uchimbaji wa Madini, Mafuta, Gesi na aina zote za nishati.
Hugo Chavez, Lous Lula na hata Kabila na Kagame na viongozi wengi wa Dunia ya Pili na ya Tatu, wameamua kulinda maslahi ya nchi zao kwa kuongeza viwango vya kodi na mapato kwa Wawekezaji wa nje ili nchi hizi iachane na tabia ya mazoea ya kutegemea misaada na mikopo kujiendesha.
Kinachonishangaza mimi ni kuwa huu ni mwaka 2010, Tanzania hatujawa na ulazima wa kutumia Rasilimali zetu kwa lengo mmoja la kukamua Hazina yetu kama tulivyofanya mwaka 1978 tulipoingia vita na Uganda.
Ni mwaka 2010, Afrika Kusini iko huru na kila nchi inayotuzunguka iko huru pamoja na kuwa kuna chokochoko za ndani lakini ukweli ni kuwa ndoto za Tanzania kuvamiwa ni ndogo mno.
Sasa kama kwa miaka 25 tumeishi kwa Amani, Utulivu na Mshikamano, iweje tushindwe kujijenga kikamilifu na kuachana na Utegemezi wa misaada na hata kuendelea kuunadi uhuru wetu kwa hiyo asilimia 40 tunayowapa Benki ya Dunia, Nchi wafadhili na Wawekezaji?
Kwa nini chama chako CCM na Serikali yake vina kigugumizi cha kuleta mapinduzi ya uzalishaji mali ambao utalenga kumnufaisha Mtanzania na si mwekezaji?
Je ushajiuliza kama tungefuata mkondo na mfano wa Australia na kuongeza pato la Taifa kutoka wka Wawekezaji kutoka asilimia 4 hadi asilimia 40 ni mapato ya kiasi gani tungepata na ni miradi mingapi ya maendeleo tungeweza kuigharamia wenyewe?
Ikiwa ulikiri kuwa Asilimia 30 ya Bajeti yetu inapotea katika Rushwa, je huoni kama ukiziba kabisa mianya ya Rushwa na Ufisadi na hata kuongeza pato la Taifa kwa asilimia hata 25, Tanzania inaweza kuwa nchi inayojitegemea kabisa miaka 10 kutoka leo?
Ulipochaguliwa 2005, wengi walitegemea ungekuwa Gorbachev wetu ambye utaleta mapinduzi ya fikra na uzalishaji mali, mapinduzi ambayo yangeiondoa Tanzania kutoka utegemezi.
Lakini kinachoonekana ni kuwa umeendeleza demokrasia ya kujieleza kwa watu, lakini wanachokuambia, wanacholalamikia hata kukutukana kinaingia sikio moja na kutokea lingine na kasi yako ni kuiingiza Tanzania katika uchumi tegemezi na si ajabu kuongeza wigo wa utegemezi kwa kuuza asilimia zaidi za uhuru wetu kwa kisingizio chako cha kutuingiza katika soko huria au kama aliyekutangulia Rais Mkapa aliyekuwa akituhubiria Utandawazi na kutupumbaza na vijideni tulivyofutiwa huku akiruhusu misahama ya kodi na mapato na kuuza kila rasilimali kwa bei chee!
Uamuzi wa Wafadhili kupunguza misaada kwenye bajeti yetu isikupe kizunguzungu au shinikizo. Ningekuwa mimi wewe, ningeita timu ifanye kazi ya kuziba mwanya huo wa mapato kwa kuongeza pato la Taifa na kuiga walichofanya Australia!
Mara nyingine Ukarimu wako unafadhaisha, majuzi kwenye mkutano wa WEF ulikaririwa ukiwaita WB, IMF na nchi wafadhili eti wao ni Wakubwa, je unyonge wako na kujisalimisha kwa wanaotunyonya utakoma lini?
Tunajua wazi kuwa Takrima, Rushwa na Ufisadi ni vitu vigumu sana kwako kuvishinda, wewe CCM na Serikali yako mmenogewa sana na Takrima na Rushwa. Basi tunakupa Ruksa, kaa na hiyo Takrima yako, ipunguze kutoka asilimia 30 hadi 15, lakini ongeza pato la Taifa kwa kila sekta ambayo mwekezaji kaweka mguu kutoka asilimia 3 hadi asilimia 40. Zaidi ya hilo toa sharti la kutaka Wawekezaji watumie malighafi, nguvukazi na kila aina ya nyenzo kwa kutumia kinachopatikana Tanzania. Ama futa misamaha yote kwa Wawekezaji wote kutoka nje ya nchi na hata wa ndani ya nchi walio na ubia.
Uamuzi ni wako Mheshimiwa Rais, kusuka au kunyoa!