Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
Makamo Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar, Rais Amani Abeid Karume leo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mkutano mkubwa ulionadaliwa na chama hicho kwa lengo kuelezea mazungumzo ya kisiasa yaliyofikiwa kati yake na Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad.
Mkutano huo ambao utakuwa ni wa mwanzo wa chama hicho kuzungumzia mazungumzo ya viongozi hao yaliobatizwa jina la Maridhiano unatarajiwa kuwa wa aina yake katika viwanja vya Demokrasia Kibanda Maiti ambapo imeelezwa kwamba utapambwa kwa vikundi mbali mbali vya burudani kabla ya kuanza kwa mkutano huo.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Umoja wa Wazazi wa Jumuiya ya CCM na kusainiwa na Naibu Katibu Mkuu wake, Yasmin Aloo na kusambazwa kwa vyombo vya habari imewataka wanachama na wafuasi pamoja na wakereketwa wa chama hicho wa mikoa yote mitatu ya Unguja kujitokeza kwa wingi kuhudhuria mkutano huo.
Wakati Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikitarajiwa kuwatangazia wanachama wake suala la mazungumzo ya Rais Karume na Malim Seif tayari Chama Cha Wananchi (CUF) kimeshawaelezwa wanachama wake suala hilo na kuwaomba wanachama wote wa CUF na wazanzibari kuunga mkono mazungumzo hayo ambayo yana azma ya kuleta umoja na maridhiano kwa wazanzibari wote bila ya kujali itikadi za kisiasa walizonazo wanachama hao.
Mkutano wa CCM wa leo utakuwa ni mkutano wa kwanza kwa wafuasi wa chama hicho kupokea tamko la Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume tokea alipokutana Ikulu Unguja na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad Novemba 5 mwaka huu mazungumzo ambayo yameelezwa kuwa na nia ya kumaliza uhasama na chuki za kisiasa kati ya pande mbili hizo.
Ni siku moja tu baada ya viongozi hao kukutana Ikulu na kufanya mazungumzo ya faragha yaliochukua takriban masaa mawili mazungumzo ambayo hatima yake yamesababisha Chama Cha Wananchi (CUF) kuregeza msimamo wake wa kutomtambua Rais Karume kuwa ndiye Rais halali wa Zanzibar.
Akiutangazia umati mkubwa katika viwanja vya Demokrasia Novemba 7 mwaka huu Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad alisema uongozi wa baraza kuu umeamua kumtambua Rais Karume kuwa ndiye Rais halali wa Zanzibar kauli ambayo ilipingwa vikali na wafuasi wa chama hicho kwa upande wa Unguja na kumshutumu kiongozi wao kuwa amewasaliti wanachama wake.
Kufuatia kauli hiyo wafuasi hao walipiga kelele za kutotaka kutambuliwa Rais Karume huku wengine wakiangua vilio hadharani na kusema hawakubaliani na tamko hilo jambo ambalo lilisababisha Mwenyekiti wa chama hicho Professa Ibrahim Lipumba kupanda jukwaani na kuwaomba wafuasi hao wakubaliane na maamuzi hayo kwa kuwa hayo sio maamuzi ya Maalim Seif bali ni uamuzi wa baraza kuu la uongozi wa CUF.
Hata hivyo Professa Lipumba aliwaambia wafuasi hao kwamba Maalim Seif hajawahi kuwa msaliti katika historia ya maisha yake katika siasa, hivyo sio sawa kumuona kama amekisaliti chama na wafuasi wake na kuwataka wote wakubaliane na tamko hilo kwa lengo la kujenga umoja na mshikamano kwa maslahi ya wazanzibari wote.
Wakati hayo yakifanyika Unguja wafuasi wa chama hicho Kisiwani Pemba walilipokea tamko hilo kwa furaha na kuwapongeza viongozi hao kwa ujasiri mkubwa waliounesha kwa kukutana na kuweza kuzungumzia maslahi ya zanzibari na watu wake.
Wiki moja baada ya wafuasi wa CUF kumkatalia hadharani Maalim Seif kumtambua Rais Karume Umoja wa Wanawake wa CUF walitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuunga mkono mazungumzo hayo pamoja na kuitisha maandamano makubwa yaliofuatiwa na mkutano ambayo ulimuomba radhi Katibu Mkuu wao kwa kitendo walichokionesha Novemba 7 cha kujiliza hadaharani wakisema wamekijutia kwa kuwa walikuwa hawajaelewa azma na lengo la mazungumzo ya viongozi hao wawili.
Tayari Chama Cha CUF kimeshafanya mikutano miwili ya hadhara kwa ajili ya kuwajulisha wafuasi wao kuhusu nia ya kumtambuwa Rais Karume kama kiongozi halali wa Zanzibar aliyeshinda katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005.
Chimbuko la kutotambuliwa Rais Karume na Chama Cha Wananchi CUF ni mara baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 ambapo CUF kilikataa matokeo ya uchaguzi huo na kusema hakitamtambua kuwa ndie Rais halali kwa madai kuwa hajashinda katika uchaguzi huo kwa kuwa uchaguzi ulikuwa na hila na udanganyifu katika mchakato mzima wa uchaguzi wenyewe.
Kwa mujibu wa taarifa ya CCM imesema kwamba viongozi wote wakuu wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar pamoja na viongozi wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar watahudhuria mkutano huo na kuhutubiwa na Rais Amani Karume.
Awali kulikuwa na fununu kwamba Kamati ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM kukutana Zanzibar siku moja kabla ya mkutano huo wa hadhara kuelezwa juu ya suala zima la mazungumzo na kutoa baraka zake kama ilivyofanywa kwa upande wa CUF kuwaita barza kuu la uongozi kuwaeleza suala hilo.
Akizungumza kwa njia ya simu Katibu wa Idara ya Uenezi wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai alisema hakuna kikao cha halmashauri kuu ya CCM Zanzibar kitakachofanyika zaidi ya mkutano ambao umeandalwia na chama hicho kufanyika leo Unguja.
Mkutano wa leo unatazamiwa kuhudhuriwa na wanachama na wafuasi wa wa CCM na wafuasi wengine wasiokuwa wa CCM wa mikoa mitatu ya Kusini, Kaskazini na Mjini Magharibi Unguja ambapo hadi haijaelezwa kama kwa upande wa Pemba mkutano kama huo utapangwa lini.
Nchi mbali mbali za Umoja wa Ulaya wakiwemo washiriki wa maendeleo wamepongeza mazungumzo yaliofikiwa Novemba 5 Ikulu Unguja kati ya Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume na Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad yenye lengo la kumaliza mivutano ya kisiasa na kujenga Zanzibar mpya yenye mashirikiano na umoja.
Hii itakuwa ni mara ya nne kuafikiwa kwa mazungumzo ya kutafuta mwafaka wa kisiasa ambapo awali mazungumzo hayo yalifanyika mwaka 1999 wakati wa utawala wa Dkt Salmin Amour Juma mazungumzo ambayo hayajatekelezwa.
Mwafaka wa pili uliafikiwa mwaka 2001 baada ya watu kadhaa kufariki dunia kufuatia maandamano yaliopangwa na Chama Cha CUF mara baada ya kukataa kuyatambua matokeo ya uchaguzi wa mwaka 2000.
Mwafaka wa tatu ulitangazwa na Rais Kikwete mara baada ya kuingia madarakani na kutangaza kuwa atamaliza mpasuko wa kisiasa Zanzibar mazungumzo ambayo yalidumu kwa miezi 14 ambapo pande mbili hizo kuvutana na mazungumzo hayo kusimamishwa ghafla.
source: zanzibar yetu web blog
Mkutano huo ambao utakuwa ni wa mwanzo wa chama hicho kuzungumzia mazungumzo ya viongozi hao yaliobatizwa jina la Maridhiano unatarajiwa kuwa wa aina yake katika viwanja vya Demokrasia Kibanda Maiti ambapo imeelezwa kwamba utapambwa kwa vikundi mbali mbali vya burudani kabla ya kuanza kwa mkutano huo.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Umoja wa Wazazi wa Jumuiya ya CCM na kusainiwa na Naibu Katibu Mkuu wake, Yasmin Aloo na kusambazwa kwa vyombo vya habari imewataka wanachama na wafuasi pamoja na wakereketwa wa chama hicho wa mikoa yote mitatu ya Unguja kujitokeza kwa wingi kuhudhuria mkutano huo.
Wakati Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikitarajiwa kuwatangazia wanachama wake suala la mazungumzo ya Rais Karume na Malim Seif tayari Chama Cha Wananchi (CUF) kimeshawaelezwa wanachama wake suala hilo na kuwaomba wanachama wote wa CUF na wazanzibari kuunga mkono mazungumzo hayo ambayo yana azma ya kuleta umoja na maridhiano kwa wazanzibari wote bila ya kujali itikadi za kisiasa walizonazo wanachama hao.
Mkutano wa CCM wa leo utakuwa ni mkutano wa kwanza kwa wafuasi wa chama hicho kupokea tamko la Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume tokea alipokutana Ikulu Unguja na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad Novemba 5 mwaka huu mazungumzo ambayo yameelezwa kuwa na nia ya kumaliza uhasama na chuki za kisiasa kati ya pande mbili hizo.
Ni siku moja tu baada ya viongozi hao kukutana Ikulu na kufanya mazungumzo ya faragha yaliochukua takriban masaa mawili mazungumzo ambayo hatima yake yamesababisha Chama Cha Wananchi (CUF) kuregeza msimamo wake wa kutomtambua Rais Karume kuwa ndiye Rais halali wa Zanzibar.
Akiutangazia umati mkubwa katika viwanja vya Demokrasia Novemba 7 mwaka huu Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad alisema uongozi wa baraza kuu umeamua kumtambua Rais Karume kuwa ndiye Rais halali wa Zanzibar kauli ambayo ilipingwa vikali na wafuasi wa chama hicho kwa upande wa Unguja na kumshutumu kiongozi wao kuwa amewasaliti wanachama wake.
Kufuatia kauli hiyo wafuasi hao walipiga kelele za kutotaka kutambuliwa Rais Karume huku wengine wakiangua vilio hadharani na kusema hawakubaliani na tamko hilo jambo ambalo lilisababisha Mwenyekiti wa chama hicho Professa Ibrahim Lipumba kupanda jukwaani na kuwaomba wafuasi hao wakubaliane na maamuzi hayo kwa kuwa hayo sio maamuzi ya Maalim Seif bali ni uamuzi wa baraza kuu la uongozi wa CUF.
Hata hivyo Professa Lipumba aliwaambia wafuasi hao kwamba Maalim Seif hajawahi kuwa msaliti katika historia ya maisha yake katika siasa, hivyo sio sawa kumuona kama amekisaliti chama na wafuasi wake na kuwataka wote wakubaliane na tamko hilo kwa lengo la kujenga umoja na mshikamano kwa maslahi ya wazanzibari wote.
Wakati hayo yakifanyika Unguja wafuasi wa chama hicho Kisiwani Pemba walilipokea tamko hilo kwa furaha na kuwapongeza viongozi hao kwa ujasiri mkubwa waliounesha kwa kukutana na kuweza kuzungumzia maslahi ya zanzibari na watu wake.
Wiki moja baada ya wafuasi wa CUF kumkatalia hadharani Maalim Seif kumtambua Rais Karume Umoja wa Wanawake wa CUF walitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuunga mkono mazungumzo hayo pamoja na kuitisha maandamano makubwa yaliofuatiwa na mkutano ambayo ulimuomba radhi Katibu Mkuu wao kwa kitendo walichokionesha Novemba 7 cha kujiliza hadaharani wakisema wamekijutia kwa kuwa walikuwa hawajaelewa azma na lengo la mazungumzo ya viongozi hao wawili.
Tayari Chama Cha CUF kimeshafanya mikutano miwili ya hadhara kwa ajili ya kuwajulisha wafuasi wao kuhusu nia ya kumtambuwa Rais Karume kama kiongozi halali wa Zanzibar aliyeshinda katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005.
Chimbuko la kutotambuliwa Rais Karume na Chama Cha Wananchi CUF ni mara baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 ambapo CUF kilikataa matokeo ya uchaguzi huo na kusema hakitamtambua kuwa ndie Rais halali kwa madai kuwa hajashinda katika uchaguzi huo kwa kuwa uchaguzi ulikuwa na hila na udanganyifu katika mchakato mzima wa uchaguzi wenyewe.
Kwa mujibu wa taarifa ya CCM imesema kwamba viongozi wote wakuu wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar pamoja na viongozi wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar watahudhuria mkutano huo na kuhutubiwa na Rais Amani Karume.
Awali kulikuwa na fununu kwamba Kamati ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM kukutana Zanzibar siku moja kabla ya mkutano huo wa hadhara kuelezwa juu ya suala zima la mazungumzo na kutoa baraka zake kama ilivyofanywa kwa upande wa CUF kuwaita barza kuu la uongozi kuwaeleza suala hilo.
Akizungumza kwa njia ya simu Katibu wa Idara ya Uenezi wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai alisema hakuna kikao cha halmashauri kuu ya CCM Zanzibar kitakachofanyika zaidi ya mkutano ambao umeandalwia na chama hicho kufanyika leo Unguja.
Mkutano wa leo unatazamiwa kuhudhuriwa na wanachama na wafuasi wa wa CCM na wafuasi wengine wasiokuwa wa CCM wa mikoa mitatu ya Kusini, Kaskazini na Mjini Magharibi Unguja ambapo hadi haijaelezwa kama kwa upande wa Pemba mkutano kama huo utapangwa lini.
Nchi mbali mbali za Umoja wa Ulaya wakiwemo washiriki wa maendeleo wamepongeza mazungumzo yaliofikiwa Novemba 5 Ikulu Unguja kati ya Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume na Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad yenye lengo la kumaliza mivutano ya kisiasa na kujenga Zanzibar mpya yenye mashirikiano na umoja.
Hii itakuwa ni mara ya nne kuafikiwa kwa mazungumzo ya kutafuta mwafaka wa kisiasa ambapo awali mazungumzo hayo yalifanyika mwaka 1999 wakati wa utawala wa Dkt Salmin Amour Juma mazungumzo ambayo hayajatekelezwa.
Mwafaka wa pili uliafikiwa mwaka 2001 baada ya watu kadhaa kufariki dunia kufuatia maandamano yaliopangwa na Chama Cha CUF mara baada ya kukataa kuyatambua matokeo ya uchaguzi wa mwaka 2000.
Mwafaka wa tatu ulitangazwa na Rais Kikwete mara baada ya kuingia madarakani na kutangaza kuwa atamaliza mpasuko wa kisiasa Zanzibar mazungumzo ambayo yalidumu kwa miezi 14 ambapo pande mbili hizo kuvutana na mazungumzo hayo kusimamishwa ghafla.
source: zanzibar yetu web blog