Rais Buhari atangaza utajiri wake

Rais Buhari atangaza utajiri wake

RUCCI

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2011
Posts
1,702
Reaction score
1,716
150807165728_buhari_nigeria_512x288_bbc_nocredit.jpg


Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ametangaza kuwa ana $150,000 (£100,000) kwenye akaunti zake za benki, katika hatua inayolenga kuendeleza uwazi na kupiga vita ufisadi serikalini.

Kiasi hicho kinaonyesha kuwa amekuwa akiishi "maisha ya kujinyima", msemaji wake Garba Shehu amesema.

Bw Buhari anamiliki makao matano na nyumba mbili za matope, pamoja na mashamba kadha, akaongeza.

Kiongozi huyo wa zamani wa kijeshi alichaguliwa kuwa rais mwezi Machi ahadi zake kuu zikiwa kukabiliana na ufisadi na ukosefu wa usalama.

Ufisadi ni tatizo sugu katika taifa hilo lenye uchumi mkubwa barani Afrika na mwezi uliopita, Bw Buhari alisema $150bn (£100bn) zimeporwa kutoka kwa hazina ya serikali.

Bw Shehu alisema kupitia taarifa kuwa Bw Buhari ana shamba la matunda na renchi yenye ng'ombe 270, kondoo 25, farasi watano na ndege wengi.

Pia anamiliki hisa katika kampuni tatu - Berger Paints, Union Bank na Skye Bank, taarifa hiyo iliongeza.

Hata hivyo, makamu wa rais wa Nigeria Yemi Osinbajo ni tajiri kumshinda mdosi wake.

Taarifa hiyo ilisema Bw Osinbajo ana $900,000 (£600,000) kwenye akaunti zake za benki.

Kwenye fomu ya kutangaza utajiri wake, Bw Osinbajo pia alifichua anamiliki nyumba nne, moja ikiwa ya vyumba viwili vya kulala ambayo analipia mkopo mjini Bedford, Uingereza.

Taarifa hiyo haikusema thamani halisi ya mali yote ya rais na makamu wake, ikieleza kuwa stakabadhi zilizokabidhiwa Afisi ya Maadili zitafanywa wazi kwa umma karibuni baada ya ukaguzi wake kukamilika.

Chanzo: BBC
 
Mmmh !! imposibo huyo labda siyo mNigeria... "vijisenti" hawa watu ni mBilioneaz!!
 
Nimeshangaa sana aisee...kuwa kiongozi mkubwa Wa jeshi miaka mingi.,..na menhine ambayo siyajui..eti ana Nyumba mbili, ana 150,000$, kondoo 25??? Teh teh teh...ingawa sijui ni vigumu kuamini.
 
Kama kawa karibu viongozi wote wa Africa wanafanana kwa usanii wao,huyu alipokuwa mtawala wa kijeshi alipiga sana hela. Unaambiwa pamoja Sani Abacha kufisadi hela nyingi lakini maendeleo na hali za wananchi zilikuwa nzuri kuliko viongozi wengine wote wawe wa Kiraia au wa Kijeshi.
 
Wasalaaam alleikum!!

Duru zenye kujuza zinasema kuwa Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria anawezekana ndiye Rais lofa kuliko marais wote wa Africa. Nyaraka za kuorodhesha mali zake ambazo alizirejesha katika kukidhi matakwa ya kisheria; na baadaye kuwekwa wazi zinaonyesha kuwa ana US $ 150,000 tu katika akaunti yake binafsi. Anamiliki nyumba tano za tofali za sement na nyumba mbili za tofali za matope, ana ngombe 250, kondoo 25, farasi watano na ndege wa kienyeji (chiriku, njiwa etc) kadhaa. Ameandikisha kuwa ana gari mbili alizonunua kutokana na akiba zake, na hana akaunti nje ya nchi, hana kiwanda, hana kampuni na wala hana kisima cha mafuta.

Huyu Rais amenifurahisha sana kwa uwazi alioonyesha kulinganisha na marais wengine katika Africa, mfano Jose Eduardo dos Santos wa Angola: $20 Billion, Uhuru Kenyatta wa Kenya: $500 Million, Paul Biya wa Cameroon: $200 Million, na King Mswati III wa Swaziland: $100 Million. Rais aliyemtangulia Goodluck Jonathan anazo: $100 Million.

====================================
imrs.php


Nigerian President Muhammadu Buhari salutes his supporters during his inauguration in Abuja, Nigeria, on May 29. An official in Nigeria says the new president's wealth declaration shows that he has been living "an austere and Spartan lifestyle" compared to his predecessors and other senior government officials, with $150,000 in his personal account. (Sunday Alamba/AP)

By the standards of sub-Saharan African leaders, Nigeria's President Muhammadu Buhari is dirt-poor.

According to a statement released by his government, he has $150,000 in his savings account. He owns five homes and two mud houses, an orchard and ranch with 270 head of cattle, 25 sheep, five horses and a variety of birds. He has bought two cars from his savings

"President Buhari had no foreign account, no factory and no enterprises. He also had no registered company and no oil wells," reads the statement released by the spokesman, Garba Shehu, describing the president's assets as "Spartan."

The question on many minds is this: Is Buhari, Nigeria's former military ruler and ex-head of the oil ministry, telling the truth?

Corruption, after all, is a major problem in Africa's largest economy. Buhari himself has publicly said that more than $150 billion is missing from the government's coffers. Still, the public declaration appears to be an attempt to show some much-needed transparency. Buhari was elected in March largely by promising that he wouldn't tolerate corruption.

What's clear is that Buhari has done what his predecessors - and most other African leaders - have never done.

Consider these five other African leaders. They have been labeled by Forbes Magazine as the "five worst leaders in Africa."

1. Teodoro Obiang Nguema Mbasogo, president of Equatorial Guinea

He's Africa's longest-serving ruler, an autocrat who leads the tiny, oil-rich West African nation of Equatorial Guinea. Despite its vast natural wealth, the majority of its people live in deep poverty with no access to clean drinking water, proper educational or health facilities. One fifth of children die before age 5. The money has gone into the pockets of Mbasogo and his family. They own luxury

Source: https://www.washingtonpost.com/news...as-leader-may-be-the-least-corrupt-in-africa/
 
Back
Top Bottom