888I
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 445
- 554
NITATUMIA ALIYOYASEMA GWAJIMA PIA..
Kwa takwimu zao wenyewe, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinasema kimefanikiwa kuwasajili wanachama zaidi ya milioni 10 kote nchini. Hii si idadi ndogo. Hii ni jeshi la maana kweli kweli wameshashinda Uchaguzi kabla ya kupiga kampeni hapa.
Tukigeuka upande wa maendeleo ndiyo balaa madaraja yamejengwa, barabara zimefunguliwa, mikopo ya elimu ya juu imetolewa kwa wingi, madarasa yameongezeka, vituo vya afya vimepanuka, na mapato ya taifa yameimarika.
Ni wazi Rais Samia Suluhu Hassan anafanya kazi. Hakika, mama anaupiga mwingi.
Lakini basi, tukiwa tumefika hapa – kwanini sasa tusifanye reform ya uchaguzi?
Kwa nini tusirekebishe sheria na mfumo wa Tume ya Uchaguzi ili kuonesha dunia na wananchi kuwa:
✅ Tuna ushindi wa haki,
✅ Tuna uwanja wa ushindani ulio sawa,
✅ Tuna imani hata kwa wanaotofautiana nasi.
Tumejenga vituo vya afya, shule, na reli. Kwani tunaogopa Nini ?
Wapo wanaosema Chadema HAWANA hoja wananchi hawawaelewi.
Basi kama ni hivyo, kwa nini tuogope reforms?
Si bora tufungue milango, kila mtu ashindane kwa uwanja sawa, halafu tuwashinde kishujaa kama tulivyozoea?
CCM ina nguvu.
CCM ina mtandao.
CCM ina historia.
Lakini historia ya kweli haijengwi kwa woga wa mabadiliko — inajengwa kwa uthubutu wa kukubali kwamba hata wenye nguvu, wanahitaji kanuni za haki.
Kwa takwimu zao wenyewe, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinasema kimefanikiwa kuwasajili wanachama zaidi ya milioni 10 kote nchini. Hii si idadi ndogo. Hii ni jeshi la maana kweli kweli wameshashinda Uchaguzi kabla ya kupiga kampeni hapa.
Tukigeuka upande wa maendeleo ndiyo balaa madaraja yamejengwa, barabara zimefunguliwa, mikopo ya elimu ya juu imetolewa kwa wingi, madarasa yameongezeka, vituo vya afya vimepanuka, na mapato ya taifa yameimarika.
Ni wazi Rais Samia Suluhu Hassan anafanya kazi. Hakika, mama anaupiga mwingi.
Lakini basi, tukiwa tumefika hapa – kwanini sasa tusifanye reform ya uchaguzi?
Kwa nini tusirekebishe sheria na mfumo wa Tume ya Uchaguzi ili kuonesha dunia na wananchi kuwa:
✅ Tuna ushindi wa haki,
✅ Tuna uwanja wa ushindani ulio sawa,
✅ Tuna imani hata kwa wanaotofautiana nasi.
Tumejenga vituo vya afya, shule, na reli. Kwani tunaogopa Nini ?
Wapo wanaosema Chadema HAWANA hoja wananchi hawawaelewi.
Basi kama ni hivyo, kwa nini tuogope reforms?
Si bora tufungue milango, kila mtu ashindane kwa uwanja sawa, halafu tuwashinde kishujaa kama tulivyozoea?
CCM ina nguvu.
CCM ina mtandao.
CCM ina historia.
Lakini historia ya kweli haijengwi kwa woga wa mabadiliko — inajengwa kwa uthubutu wa kukubali kwamba hata wenye nguvu, wanahitaji kanuni za haki.