Regia Mtema
R I P
- Nov 21, 2009
- 2,970
- 863
Wakuu.Heshima mbele.
Mtakumbuka kuwa Rais amelihutubia Bunge mara kadhaa tangu kuingia kwake madarakani. Katika hotuba zake Bungeni amezungumza mambo mengi na kutoa ahadi na mielekeo kadhaa kuhus Taifa hili.Kati ya ,ambo aliyoahidi na kuahidi kuyatekeleza kabla ya mwaka 2010 ni kuhusu 50/50 representation kati ya Wanawake na Wanaume kwenye vyombo vya maamuzi ikiwemo Bunge.Katika kulitekeleza hilo Chama Cha Mapinduzi(CCM) kilikuwa mstari wa kwanza katika kuhakikisha hili linatekelezeka. Nilikuwa nina imani kubwa na Rais kwamba hili linaenda kutekelezwa.Lakini chakushangaza ahadi hii imeonekana kuwa ni ndoto ya mchana kwani haitaenda kutekelezeka,kama ilivyoelezwa na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Pius Msekwa kama alivyonukuliwa na gazeti la habri leo hapo chini.
Kufikia 50% ya wabunge wanawake kwayeyuka9
MFUMO uliokuwa na lengo la kufikisha asilimia 50 ya wabunge wanawake, umeshindikana kutokana na athari za kutekelezwa kwa mfumo huo nchini.
Akizungumza katika wakati wa kufungua warsha ya siku mbili ya mikakati ya kuongeza idadi ya wagombea wanawake katika Uchaguzi Mkuu 2010, Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa alisema ingawa mfumo huo ungefikisha lengo hilo lakini athari zake ni kuwa zaidi ya malengo hayo.
Kwa mujibu wa Msekwa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), CCM wamekubali kuendelea na mfumo wa sasa wa viti maalumu vya wanawake ambao idadi yao katika Bunge na Baraza la Wawakilishi linapatikana kutokana na wingi wa kura za chama katika uchaguzi wa wabunge na wawakilishi.
Kutokana na hali hiyo, amependekeza vyama vya siasa kuteua wanawake wengi zaidi katika nafasi za kugombea majimboni ili kuongeza idadi ya wabunge bungeni na kwamba mfumo wa viti maalumu ambao utaendelea kuwepo, utasaidia kuongeza idadi yao.
CCM ilifanya uchambuzi wa kina wa njia zipatazo tano zinazoweza kutufikisha kwenye lengo lililomo katika azimio la Umoja wa Afrika (AU). Tumeamua kuendelea na mfumo wa sasa ingawa haupendwi sana na kwamba unafaa kwa kuwa ni utaratibu wa muda na sio wa kudumu,
Msekwa alitaja njia ambazo zilipendekezwa ili kufikia asilimia 50 kwa 50 bungeni kati ya wanawake na wanaume kuwa ni wa kila chama cha siasa kitakachoshiriki kusimamisha wagombea wawili, wanawake na wanaume, mfumo ambao una athari za kuongeza idadi ya wabunge kutoka 232 wa sasa hadi kufikia 480, idadi ambayo ni kubwa mno ukizingatia uwezo mdogo wa uchumi.
Alisema kuwa njia hiyo pia inatoa mwanya kwa chama husika kupoteza viti viwili kwa pamoja kutokana na udhaifu wa mgombea mmoja kati yao na pia ungechochea kuwapo mgogoro na mivutano kati ya wabunge na wawakilishi wa majimbo hususani kwa upande wa Zanzibar ambako jimbo moja la uchaguzi lingekuwa na viongozi wanne.
Msekwa alisema mfumo wa pili ulikuwa kuendelea na majimbo ya uchaguzi yaliyopo sasa na kuanzishwa majimbo mapya ya ziada ambapo kila wilaya ya kiutawala ingekuwa na jimbo la uchaguzi litakalogombewa na wanawake pekee.
Athari za njia hii ni kufanya wilaya ya kiutawala kuwa ni jimbo za ziada la uchaguzi litakalokuwa na mbunge mwanamke, hivyo ingesababisha kupunguzwa kwa idadi ya wilaya za kiutawala kutoka 137 za sasa hadi kufikia 112, jambo ambalo lingeweza kudumaza maendeleo ya nchi hasa wakati huu ambapo kuna maombi ya kuanzishwa wilaya mpya.
Alisema njia hiyo pia ingeathiri mamlaka za dola kwa kuingilia uwezo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano kuanzisha wilaya mpya pale anapoona inafaa, kwani akifanya hivyo inamaanisha kuongeza majimbo ya uchaguzi wa wabunge na kuwapo hatari ya muingiliano wa kikazi baina ya wabunge wanawake wa wilaya na wabunge wa majimbo ya kawaida hususani kwenye wilaya kubwa zenye majimbo mengi.
Msekwa alisema mfumo wa tatu uliojadiliwa ni kuanzisha utaratibu wa kura za uwiano (Party list system of proportional), ambao ungetoa nafasi kwa chama kumuombea kura mgombea badala ya kufanya kampeni.
Alisema njia hiyo ilikuwa na athari za kupunguza hamasa kwa wapiga kura kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi, kwani hawapati fursa ya kumfahamu mgombea watakotaka kumchagua.
Huu ni mfumo mpya ambao unahitaji muda wa kutosha kuwaelimisha wananchi juu ya faida zake hivyo usingeweza kufanyika kwa ufanisi kabla ya uchaguzi wa 2010.
Msekwa alitaja njia ya nne kuwa ni kuendelea na mfumo wa sasa wa viti vya maendeleo vya wanawake kulingana na idadi ya kura ingawa athari zake ni kuendeleza upendeleo kwa wanawake kwa kutengewa viti na hauwezi kupatikana kwa asilimia 50 ya wabunge/ wawakilishi wanawake ambayo imekusudiwa.
Alisema mfumo wa mwisho ulikuwa ni kufuta majimbo yote 232 yaliyopo na kuunda majimbo mapya machache na kila jimbo kuwa na wabunge wawili wanawake na wanaume.
Pia njia hii ina athari za kurudisha nyuma katika maendeleo ya kidemokraisa nchini kwa kufuta majimbo, pia utatoa mwanya kwa chama kupoteza viti vyote viwili na unachochea mazingira ya kuwapo migogoro na mivutano miongoni mwa wabunge hususani kwa Zanzibar.
Msekwa alivitaka vyama vya siasa nchini kuteua idadi kubwa ya wagombea wanawake kugombea majimbo ya uchaguzi mkuu ujao ili kutimiza lengo la kuongeza wabunge wengi wanawake.
Alisema kuwa kuna umuhimu wa kushirikisha wanawake katika vyombo vya maamuzi kutokana na idadi ya wanawake katika jamii, mchango mkubwa wa wanawake katika maendeleo ya jamii na kiuchumi na pia kuimarisha demokrasia. Semina hiyo inaendelea leo ambapo mada mbali mbali zitatolewa na kujadiliwa.
SOURCE: HABARI LEO JUMAPILI 17 JAN 2010
Kwa maelezo hayo basi. Rais alidanganya Bunge na Watanzania kwa ujumla. Hivi hii nchi inalekea wapi kama hata Rais amekuwa akitoa ahdi za uongo?
Mtakumbuka kuwa Rais amelihutubia Bunge mara kadhaa tangu kuingia kwake madarakani. Katika hotuba zake Bungeni amezungumza mambo mengi na kutoa ahadi na mielekeo kadhaa kuhus Taifa hili.Kati ya ,ambo aliyoahidi na kuahidi kuyatekeleza kabla ya mwaka 2010 ni kuhusu 50/50 representation kati ya Wanawake na Wanaume kwenye vyombo vya maamuzi ikiwemo Bunge.Katika kulitekeleza hilo Chama Cha Mapinduzi(CCM) kilikuwa mstari wa kwanza katika kuhakikisha hili linatekelezeka. Nilikuwa nina imani kubwa na Rais kwamba hili linaenda kutekelezwa.Lakini chakushangaza ahadi hii imeonekana kuwa ni ndoto ya mchana kwani haitaenda kutekelezeka,kama ilivyoelezwa na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Pius Msekwa kama alivyonukuliwa na gazeti la habri leo hapo chini.
Kufikia 50% ya wabunge wanawake kwayeyuka9
Imeandikwa na Anastazia Anyimike;
Tarehe: 17th January 2010
Tarehe: 17th January 2010
MFUMO uliokuwa na lengo la kufikisha asilimia 50 ya wabunge wanawake, umeshindikana kutokana na athari za kutekelezwa kwa mfumo huo nchini.
Akizungumza katika wakati wa kufungua warsha ya siku mbili ya mikakati ya kuongeza idadi ya wagombea wanawake katika Uchaguzi Mkuu 2010, Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa alisema ingawa mfumo huo ungefikisha lengo hilo lakini athari zake ni kuwa zaidi ya malengo hayo.
Kwa mujibu wa Msekwa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), CCM wamekubali kuendelea na mfumo wa sasa wa viti maalumu vya wanawake ambao idadi yao katika Bunge na Baraza la Wawakilishi linapatikana kutokana na wingi wa kura za chama katika uchaguzi wa wabunge na wawakilishi.
Kutokana na hali hiyo, amependekeza vyama vya siasa kuteua wanawake wengi zaidi katika nafasi za kugombea majimboni ili kuongeza idadi ya wabunge bungeni na kwamba mfumo wa viti maalumu ambao utaendelea kuwepo, utasaidia kuongeza idadi yao.
CCM ilifanya uchambuzi wa kina wa njia zipatazo tano zinazoweza kutufikisha kwenye lengo lililomo katika azimio la Umoja wa Afrika (AU). Tumeamua kuendelea na mfumo wa sasa ingawa haupendwi sana na kwamba unafaa kwa kuwa ni utaratibu wa muda na sio wa kudumu,
Msekwa alitaja njia ambazo zilipendekezwa ili kufikia asilimia 50 kwa 50 bungeni kati ya wanawake na wanaume kuwa ni wa kila chama cha siasa kitakachoshiriki kusimamisha wagombea wawili, wanawake na wanaume, mfumo ambao una athari za kuongeza idadi ya wabunge kutoka 232 wa sasa hadi kufikia 480, idadi ambayo ni kubwa mno ukizingatia uwezo mdogo wa uchumi.
Alisema kuwa njia hiyo pia inatoa mwanya kwa chama husika kupoteza viti viwili kwa pamoja kutokana na udhaifu wa mgombea mmoja kati yao na pia ungechochea kuwapo mgogoro na mivutano kati ya wabunge na wawakilishi wa majimbo hususani kwa upande wa Zanzibar ambako jimbo moja la uchaguzi lingekuwa na viongozi wanne.
Msekwa alisema mfumo wa pili ulikuwa kuendelea na majimbo ya uchaguzi yaliyopo sasa na kuanzishwa majimbo mapya ya ziada ambapo kila wilaya ya kiutawala ingekuwa na jimbo la uchaguzi litakalogombewa na wanawake pekee.
Athari za njia hii ni kufanya wilaya ya kiutawala kuwa ni jimbo za ziada la uchaguzi litakalokuwa na mbunge mwanamke, hivyo ingesababisha kupunguzwa kwa idadi ya wilaya za kiutawala kutoka 137 za sasa hadi kufikia 112, jambo ambalo lingeweza kudumaza maendeleo ya nchi hasa wakati huu ambapo kuna maombi ya kuanzishwa wilaya mpya.
Alisema njia hiyo pia ingeathiri mamlaka za dola kwa kuingilia uwezo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano kuanzisha wilaya mpya pale anapoona inafaa, kwani akifanya hivyo inamaanisha kuongeza majimbo ya uchaguzi wa wabunge na kuwapo hatari ya muingiliano wa kikazi baina ya wabunge wanawake wa wilaya na wabunge wa majimbo ya kawaida hususani kwenye wilaya kubwa zenye majimbo mengi.
Msekwa alisema mfumo wa tatu uliojadiliwa ni kuanzisha utaratibu wa kura za uwiano (Party list system of proportional), ambao ungetoa nafasi kwa chama kumuombea kura mgombea badala ya kufanya kampeni.
Alisema njia hiyo ilikuwa na athari za kupunguza hamasa kwa wapiga kura kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi, kwani hawapati fursa ya kumfahamu mgombea watakotaka kumchagua.
Huu ni mfumo mpya ambao unahitaji muda wa kutosha kuwaelimisha wananchi juu ya faida zake hivyo usingeweza kufanyika kwa ufanisi kabla ya uchaguzi wa 2010.
Msekwa alitaja njia ya nne kuwa ni kuendelea na mfumo wa sasa wa viti vya maendeleo vya wanawake kulingana na idadi ya kura ingawa athari zake ni kuendeleza upendeleo kwa wanawake kwa kutengewa viti na hauwezi kupatikana kwa asilimia 50 ya wabunge/ wawakilishi wanawake ambayo imekusudiwa.
Alisema mfumo wa mwisho ulikuwa ni kufuta majimbo yote 232 yaliyopo na kuunda majimbo mapya machache na kila jimbo kuwa na wabunge wawili wanawake na wanaume.
Pia njia hii ina athari za kurudisha nyuma katika maendeleo ya kidemokraisa nchini kwa kufuta majimbo, pia utatoa mwanya kwa chama kupoteza viti vyote viwili na unachochea mazingira ya kuwapo migogoro na mivutano miongoni mwa wabunge hususani kwa Zanzibar.
Msekwa alivitaka vyama vya siasa nchini kuteua idadi kubwa ya wagombea wanawake kugombea majimbo ya uchaguzi mkuu ujao ili kutimiza lengo la kuongeza wabunge wengi wanawake.
Alisema kuwa kuna umuhimu wa kushirikisha wanawake katika vyombo vya maamuzi kutokana na idadi ya wanawake katika jamii, mchango mkubwa wa wanawake katika maendeleo ya jamii na kiuchumi na pia kuimarisha demokrasia. Semina hiyo inaendelea leo ambapo mada mbali mbali zitatolewa na kujadiliwa.
SOURCE: HABARI LEO JUMAPILI 17 JAN 2010
Kwa maelezo hayo basi. Rais alidanganya Bunge na Watanzania kwa ujumla. Hivi hii nchi inalekea wapi kama hata Rais amekuwa akitoa ahdi za uongo?