RAIA MWEMA: CHADEMA kwafukuta

Countrywide

JF-Expert Member
Mar 2, 2015
18,289
27,405
Gazeti la raia mwema limeandika kuwa CHADEMA Kunafukuta. Kuna makundi mawili ya Mbowe na Lissu. Ni mafahali wawili ndani ya zizi moja.

Nimewahi kusema hili suala lakini nikaishia kutukanwa, Leo gazeti la raia mwema wameweka wazi kila kitu.

Huu mgogoro uliopo utaisha kwa mpasuko mkubwa sana ambao utaenda kukipasua kabisa chama. Yote haya inasemekana ni Vita ya uongozi kuelekea 2025.

 
Gazeti la raia mwema limeandika kuwa chadema Kunafukuta. Kuna makundi mawili ya mbowe na Lissu. Ni mafahali wawili ndani ya zizi moja...
Nimekumbuka maneno ya Zitto- mkiniua kwenu hatabaki hata panya, sijui hao walio upande unaopingana na Mwenyekiti aliyetumia mabilioni wana kimzizi kana cha Zitto
 
Mmoja ameshasema anastaafu mwaka huu, mwingine bado yupo kwenye uongozi wa chama, sioni kwa vipi hao jamaa wawili wanaweza kuwa kwenye mgogoro.

Hata kama ni sababu ya makundi/kambi za uchaguzi, bado Lissu hajasema kama atagombea nafasi yoyote, sasa iweje uwepo mgogoro hapo?
 
Nimekumbuka maneno ya Zitto- mkiniua kwenu hatabaki hata panya, sijui hao walio upande unaopingana na Mwenyekiti aliyetumia mabilioni wana kimzizi kana cha Zitto
Sasa hivi mamilioni ya Mbowe hayahitajiki kwa Tundu Lissu, tayari amepata kamradi kake pale Ubeljiji amabacho kinamuingizia pesa ya kutosha. Kumbuka hata ile helikopta aliyotumia kwenye uchaguzi 2020 haikutokana na pesa za CHADEMA.
 
Kuna shinikizo Mbowe asistaafu Uenyekiti ili akamilishe Maridhiano 2025
 
Lissu lazima agombee urais 2025 hata kama CHADEMA wakitangaza kujitoa kwa sababu yoyote ile. Kugombea urais kwa Lissu ni mradi wenye tija sana hata akiwa na uhakika kuwa hatashinda.
 
kwani waasisi wa chama hawafahamiki?
 
La uzalendo linaongozwa na nani?
Hili la kikabila linaongozwa na Asenga,Kileo,Lema na Mbowe mwenyewe huku kamanda mtiifu wa wa Mbowe bwana Mrema akiwa kiranja wa ukabila pale makao makuu ya chama
 

Hakuna kitu kama hicho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…