Rai Muhimu kwa Wanasiasa kuelekea 2020

Rai Muhimu kwa Wanasiasa kuelekea 2020

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2010
Posts
17,026
Reaction score
20,511
Wataalamu wa siasa na madaraka wanakubaliana kuwa mamlaka huzaa nguvu, mtu anatafuta mamlaka ili awe na nguvu, na kwa vyovyote vile, madaraka ni mapambano ya kimadaraka (Power Struggle). Madaraka, Cheo au Nguvu ni falsafa ya tafsiri moja tu kuwa ni nguvu apatazo mtu kwajili ya kuongoza jamii ama kundi la watu katika jamii.

Tofauti ni moja tu, Madaraka, Cheo au Nguvu yanaweza kupatikana kwa njia mbili, ama kwakuteuliwa na watu wachache au mtu mmoja mwenye madaraka juu yako, ama kwa kuchaguliwa na wengi wenye uamuzi wa jumla. Katika ulimwengu mpya, mamlaka yote ya kisiasa apatayo mtu hutoka kwa watu, yaani huchaguliwa na watu kwa kura. Ili uchaguliwe na watu, unatakiwa utengeneze ushawishi kwa watu hao ili wakuone wewe ni bora kuliko mtu mwingine.

Jambo muhimu linaloumiza na kufifisha nduto za vijana wengi ni njia zipi za kutumia ili kuwashawishi watu? Hili ndio limekuwa mtihani mgumu kwa wanasiasa wengi dunia, na katika kukusaidia hilo, ulimwengu umebuni taaluma halisi ya watu wenye kufunzwa na kusaidia kuandaa njia bora kwa mwamasiasa ama mtu yeyote anayetaka madaraka, njia bora za kushawishi wapiga kura nk, watu hawa huitwa wataalamu wa mikakati ya ushindi kisiasa.

Katika kujaribu kusaidia wanasiasa hawa, mimi nimefanya utafiti wa njia bora kwa mwanasiasa na ama chama kuweza kushinda uchaguzi ndani ya chama chake cha Siasa (kura za maoni) na nje ya chama cha siasa. Mbinu za kushinda kura za maono zinaweza kutofautiana sehemu moja ya eneo la kiuchaguzi, na eneo lingine lakini yapo mambo kimsingi ambayo hayabadiliki iwe ulaya au afrika, iwe Mbeya au Bukoba.

Katika kusaidia hilo, nimekusanya "utafiti" wa kitaalamu na mifano ya chaguzi nyingi duniani na katika vyama toautitofauti duniani, namna wagombea walivyoshinda na namna vyama vyao vilivyoingia madarakani. Mifamo ya uchaguzi wa Nigeria uliomwingiza madarakani Buhari, Uchaguzi wa Panama, Uchaguzi wa Kenya, Uchaguzi wa Marekani, Uchaguzi wa Zambia, Uchaguzi wa Malawi nk.. Utafiti huu kwapamoja nimeuita ni mkakati wa ushindi.

Nimeuweka katika muundo wa kitabu chenye kurasa 250, na hivyo yeyote anayetaka kugombea udiwani, Ubunge na Urais anaweza kuutumia kama muongozo wake muhimu. Ushindi wa kisiasa hutokea kwa maandalizi ya muda mrefu, ni watu wachache sana wanaoweza kushinda madaraka bila kujiandaa yaani anaamka asubuhi anajaribu tu kugombea kisha anashinda, huyu hushindwa kuongoza na huanguka.

Nikusihi mwanasiasa unayetarajia kuwania udiwani, ubunge nk, mikakati uianze sasa kwa kupata kitabu hiki kikuongoze, utaepuka kuingia gharama kubwa za kuandaa mikakati na mwisho wa siku ukashindwa.

Mkakati huu utaupata kwa shilingi laki saba tu.(700,000/=)

0715865544
0755865544

IMG_20180125_163304_384.jpg
 
Yericko bana!

Wewe uligombea ujumbe tu katika wilaya yako na ukapigwa chini achilia mbali kitaifa.

Kama ungekuwa unajua mikakati mpaka unashauri wanasiasa wakitaka kushinda wanahitaji tu kusoma kitabu chako basi wewe leo hii ungekuwa na cheo kikubwa ndani ya CHADEMA labda kama hakuna demokrasia ndani ya CHADEMA.

Promotion at its worst!

Tujikumbushe yaliyokupata kwenye uchaguzi kupitia thread hii;

LINK>>>Yericko ashindwa uchaguzi CHADEMA
 
Yericko bana!

Wewe uligombea ujumbe tu katika wilaya yako na ukapigwa chini achilia mbali kitaifa.

Kama ungekuwa unajua mikakati mpaka unashauri wanasiasa wakitaka kushinda wanahitaji tu kusoma kitabu chako basi wewe leo hii ungekuwa na cheo kikubwa ndani ya CHADEMA labda kama hakuna demokrasia ndani ya CHADEMA.

Promotion at its worst!

Tujikumbushe yaliyokupata kwenye uchaguzi kupitia thread hii;

LINK>>>Yericko ashindwa uchaguzi CHADEMA
Hoja yako ni dhaifu sana ndugu.... 1995 JK alianguka, 2000 akaanguka, na kisha 2005 ndio akashinda....

Angekuwa na akili yako hiyo angekata tamaa
 
Hizo bahati i mean dodo kwemye mkorosho, unazosema ndio watu wanavyozitumia, kumbuka kwenye uongozi kuna kuchaguliwa na kuteuliwa, wenye bahati zao tu ndio huwa wanapata fursa!
 
Hoja yako ni dhaifu sana ndugu.... 1995 JK alianguka, 2000 akaanguka, na kisha 2005 ndio akashinda....

Angekuwa na akili yako hiyo angekata tamaa
Mkuu;
Kumbuka JK alipoanguka hakuibuka na kudai ana uwezo wa mikakati ya kisiasa na yoyote anayetaka kupata madaraka inabidi amuone yeye.

Inawezekana JK baada ya kuanguka ilibidi aende darasani kupata elimu ya mikakati!

Wewe baada ya kuanguka kwenye uchaguzi unataka wanaotaka madaraka wanunue kitabu chako ili wapate mikakati ya ushindi.

Tanzania tuna vituko!
 
Hakika kama kila mtunzi wa kitabu lazima awe na mafanikio katika alichoandika basi vitabu visingeuzwa kabisa.Lakini wengi ya watunzi hawana mafanikio kama msomaji wa kitabu husika hii ni kutokana na fursa anazokuwa nazo msomaji, la sivyo watu wasingekubali kufungishwa ndoa na mapadre ambao hawana ndoa!
 
Hizo bahati i mean dodo kwemye mkorosho, unazosema ndio watu wanavyozitumia, kumbuka kwenye uongozi kuna kuchaguliwa na kuteuliwa, wenye bahati zao tu ndio huwa wanapata fursa!
Kwa miaka miamoja hutokea mara moja tu...
 
Hakika kama kila mtunzi wa kitabu lazima awe na mafanikio katika alichoandika basi vitabu visingeuzwa kabisa.Lakini wengi ya watunzi hawana mafanikio kama msomaji wa kitabu husika hii ni kutokana na fursa anazokuwa nazo msomaji, la sivyo watu wasingekubali kufungishwa ndoa na mapadre ambao hawana ndoa!
Shukrani sana mkuu
 
Mbona kina mishale mishale ya CHADEMA sasa! Ungeacha kuweka alama yoyote ya chama chochote.
 
kitabu tsh 700,000 ???......hahaha you are not serious labda buku saba watu wangekifikiria
 
kitabu tsh 700,000 ???......hahaha you are not serious labda buku saba watu wangekifikiria
Ukishangaa mimi nakushangaa, kama hujui mgombea urais, ubunge na udiwani humia mamilioni katika kutafuta wataalamu wa kumuandalia mikakati, basi wewe utakuwa mchanga wa siasa
 
Mpe Lowasa asome ili ashinde 2020.
Au kisome mwenyewe ili upate ubunge 2020.
 
Yericko bana!

Wewe uligombea ujumbe tu katika wilaya yako na ukapigwa chini achilia mbali kitaifa.

Kama ungekuwa unajua mikakati mpaka unashauri wanasiasa wakitaka kushinda wanahitaji tu kusoma kitabu chako basi wewe leo hii ungekuwa na cheo kikubwa ndani ya CHADEMA labda kama hakuna demokrasia ndani ya CHADEMA.

Promotion at its worst!

Tujikumbushe yaliyokupata kwenye uchaguzi kupitia thread hii;

LINK>>>Yericko ashindwa uchaguzi CHADEMA
Hata Yesu alikuwa fundi Seremala hakupata wateja wengi kwenye kazi hio. Lakini alipata wafuasi wengi alipotangaza dini. Hivi unajua gari kabla haijaingia barabarani hujaribiwa kwanza, na huweza ikafeli na kurejeshwa kiwandani na kurudi barabarani tena.
 
Mpiga filimbi wa Hamelin,alikusanya watoto [emoji124][emoji124][emoji124]ngoja tutafute laki saba tutakuja.
 
Back
Top Bottom