minda
JF-Expert Member
- Oct 2, 2009
- 1,068
- 65
wakuu, gazeti hili nilipata kulijua zaidi ya miaka 10 iliyopita; likiwa na uadilifu na weledi wa hali ya juu kiasi cha kufanya mmiliki wake kutangazwa kuwa si raia wa nchi hii kisheria.
lakini katika miaka ya hivi karibuni, gazeti hili kwa mtazamo wangu, limekosa dira na limeegemea zaidi kwenye habari za kuchafuana, tuhuma bila uthibitisho na kuandika habari za uchochezi kwa misingi ya udini na ukabila.
mfano mzuri ni gazeti hili kuandika kwenye ishu zake lukuki kuhusu ukabila ndani ya chama fulani cha siasa bila ya uthibitisho; japo chama hicho kilishafafanua kwa ufasaha.
mfano mwingine ni habari za uzushi kuhusu dhehebu fulani hapa tanzania kumuandaa mgombea wa chama fulani ili eti aweze kubalance kura za waislamu na wakristo, bila ya kutoa uthibitisho.
inasikitisha kwamba gazeti hilo lililokuwa likijiuza kwa hoja zake sasa linategemea uchochezi wa kikabila na udini kama mtaji wake; na hivyo kubadili hadhi yake kutoka nguvu ya hoja hadi siasa za maji taka.
hivi mmiliki bado ni yule wa zamani na sasa amelegea kabisa baada ya kutangazwa kuwa persona non grata?
je, kuna kitu kingine cha ziada kilichofanya gazeti hilo libadili na kuandika habari zisizozingatia maadili ya uandishi?
lakini katika miaka ya hivi karibuni, gazeti hili kwa mtazamo wangu, limekosa dira na limeegemea zaidi kwenye habari za kuchafuana, tuhuma bila uthibitisho na kuandika habari za uchochezi kwa misingi ya udini na ukabila.
mfano mzuri ni gazeti hili kuandika kwenye ishu zake lukuki kuhusu ukabila ndani ya chama fulani cha siasa bila ya uthibitisho; japo chama hicho kilishafafanua kwa ufasaha.
mfano mwingine ni habari za uzushi kuhusu dhehebu fulani hapa tanzania kumuandaa mgombea wa chama fulani ili eti aweze kubalance kura za waislamu na wakristo, bila ya kutoa uthibitisho.
inasikitisha kwamba gazeti hilo lililokuwa likijiuza kwa hoja zake sasa linategemea uchochezi wa kikabila na udini kama mtaji wake; na hivyo kubadili hadhi yake kutoka nguvu ya hoja hadi siasa za maji taka.
hivi mmiliki bado ni yule wa zamani na sasa amelegea kabisa baada ya kutangazwa kuwa persona non grata?
je, kuna kitu kingine cha ziada kilichofanya gazeti hilo libadili na kuandika habari zisizozingatia maadili ya uandishi?