BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 654
- 1,598
Hayo ameyabainisha Agosti 24, 2025 mara baada ya kuchukua fomu katika Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Kinondoni, mgombea huyo alieleza kuwa ajenda yake kuu ni kusimamia miundombinu ya barabara, kuhakikisha elimu ya bure inakuwa na hadhi kubwa zaidi pamoja na kuboresha huduma za afya kwa Mama na mtoto ili ziwe bora na bure kwa wote.
Aidha, Bi, Rahma alisisitiza kuwa changamoto za mazingira zitatiliwa mkazo, akiahidi kusimamia usafi na uhifadhi wa mazingira ili Kinondoni ibaki kuwa sehemu salama na rafiki kwa maisha ya wakazi wake.
Mchakato wa wagombea kuchukua fomu unaendelea katika wilaya mbalimbali za Jiji la Dar es Salaam, ambapo vyama vya siasa vipo katika hatua za awali za maandalizi kuelekea uchaguzi mkuu.