Rafiki yangu Prof. Kai Krisse Mjerumani Mswahili

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,918
30,259
RAFIKI YANGU PROF. KAI KRESSE WA ZENTRUM MODERNER (ZMO) ORIENT, BERLIN, UJERUMANI

Vipi nilifika Ujermani kwenye taasisi kubwa ya utafiti iitwayo Zentrum Moderner Orient ni kisa kirefu na kinaanza na Prof. Ibrahim Noor Shariff.

Sauti ya Ujermani ilikuwa inataka kufanya kipindi katika Meza ya Duara kuzungumza kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar ya 1964 na walikuwa wamepanga jopo la Ahmed Rajab kutoka London, Dr. Harith Ghassany kutoka Washington DC, Prof. Ibrahim Noor Shariff kutoka Muscat na Saleh Feruzi Makamu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar akiwa visiwani.

Mwenyekiti ni Othman Miraji akiwa DW Bonn.

Prof. Ibrahim Noor Shariff akasema yeye hawezi kushiriki na akapendekeza jina langu.

Hawa washiriki wote mimi tukifahamiana ila Saleh Feruzi.

Mimi nilikuwa Tanga.

Hivi ndivyo nilivyoshiriki katika kipindi kile na kipindi hiki kikasababisha mimi kualikwa ZMO na Prof. Kai Kresse nifanye mhadhara mmoja na niandike mada moja.

Hii ilikuwa mwaka wa 2011 na ndiyo kwanza tumetoka katika uchaguzi wa 2010 uchaguzi ambao Zanzibar kama ilivyo kawaida uligubikwa na matatizo makubwa.

Katika kipindi kile kufupisha mambo mimi na Saleh Feruzi tulipambana sana.

Nadhani kule kwa Saleh Feruzi kutonifahamu ndiko labda kulikofanya kipindi hiki kipendeze sana kwani yeye hakuwa anategemea kutoka kwangu yale ambayo mimi nilikuwa nasema nikimkabili yeye.

Saleh Feruzi hakuwa amepata kukutana na mtu wa aina yangu na hakujua anikabili vipi ninapoeleza katika hsitoria ya CCM Zanzibar yale ambayo wengine wangeyakwepa.

Kipindi kilipokwenda hewani wasikilizaji wengi walivutiwa na jinsi nilivyokuwa naieleza CCM Zanzibar katika chaguzi zote walizoshiriki na kupata shida ya kupata ushindi unaoeleweka.

Wasikilizaji wengi wa DW Idhaa wa Kiswahili walioko nje ya Tanzania wakawa wanampigia simu Othman Miraj kutaka kunifahamu.

Katika hao walikuwa ZMO na Othman Miraji akawaunganisha ni mimi na hivi ndivyo nilivyoalikwa Ujerumani na Kai Kresse ambae akaja kuwa rafiki yangu.

Nilipanda Egypt Air ndege ya usiku hadi Cairo kisha kutoka Cairo ndege ya mchana hadi Berlin.

Kai Kresse alikuja uwanja wa ndege kunipokea.

Nakumbuka ilikuwa inanyesha mvua.

Bahati mbaya sana begi langu likawa halionekani.

Haikunishughulisha sana kwani nilichokuwa nakithamini ni laptop yangu nayo nilikuwanayo ndani ya ndege.

Huu ni moyo wangu siku zote safari zote nakuwanao mkononi ndani ya ndege.

Wakati tunatoka nje ya uwanja likatoka tangazo kuwa natafutwa Customs nikachukue mzigo wangu umeonekana.

Nakumbuka wakati tuko katika gari Kai ananipeleka waliponipangia nyumba sehemu inaitwa Wedding katika mazungumzo akaniuliza kama mimi ni mpenzi wa mpira.

Nikamwambia naipenda Liverpool.

Hapo akaniahadithia Berlin ilikuwaje Fainali ya Kombe la Vilabu Vya Ulaya Bayern Munich walipofungwa na Manchester United wakati Bayern walikuwa wakiongoza kwa magoli mawili.

Magoli yote yalirudi na wakaongezwa goli moja.
Kazi ya Ferguson Boys, Paul Scholes na wenzake.

Anasema siku ile mji mzima wa Berlin ulikuwa kimya umejiinamia.

Mazungumzo yetu yote tunazungumza Kiswahili na hakimpi shida hata kidogo.

Nilishangaa kidogo.

Akanishangaza aliponiambia kuwa mhadhara wangu wenye jina ''Baraza'' utakuwa kwa Kiswahili.

Mada yangu ilikuwa nimeiandika kwa Kiingereza.

Nimekaa ZMO kwa mwezi mzima na Kai Kresse alikuwa kila siku ananikagua ofisini kwangu kuangalia naendeleaje.

Alikuwa kanipangia siku mbili tu za kuja kazini Jumatatu na Alkhamisi.

Mimi nikawa nakuja siku zote isipokuwa Jumamosi na Jumapili.

Berlin ni katika miji migumu niliyopata kufika Ulaya.

Wajerumani si watu wenye kubeba sana tabasamu kwenye nyuso zao na hali ya mji ni hivyo tofauti na miji mingi ya Ulaya niliyopata kufika kama London, Paris, Amsterdam ambako kuna sehemu nyingi tu ambazo mtu anaweza kwenda na kuchanganyika na wenyeji.

Siku moja katika mazungumzo nilimuuliza Kai kuhusu historia ya Ujerumani.

Akaniambia inasomeshwa kama funzo watu wajifunze kutokana na yale yaliyopita hata kama ni machungu.

Kai anakuja sana Tanzania na kila akija atanitaarifu nami nitamfuata hotelini kwake.

Kila akija huwa hakosi kuja na zawadi ya kitabu kwangu.

Kai ni mwenyeji wa Dar es Salaam kiasi kuwa kuna wakati alipanga hoteli Sinza na wakati mwingine New Africa Hotel katikati ya Jiji.

Kote huko nilimfuata kumkagua na kufanya mazungumzo na yeye.

Nimefurahi kuwa Kai kaja kuhudhuria Kongamano la Kimataifa la Shaaban Robert na Kumbukizi zake MUM na nikapata bahati ya kuwaleta yeye na Prof. Ibrahim Noor Shariff Maktaba.

Kai Kresse alichukua muda mwingi sana kupitia kitabu baada ya kitabu katika Maktaba.

Picha ya kwanza Kai Kresse akiwa New Africa Hotel na picha ya Pili akiwa kwenye hoteli moja Sinza.

Picha ya tatu nikiwa Maktaba na wageni wangu na picha ya nne nikiwa na Kai Kresse ZMO, Berlin.

1704397870720.jpeg

1704397916154.jpeg

1704397950042.jpeg

1704397986865.jpeg
 
Innalillah ' yan bindiga sunkashe makiyaya jahar a taraba.
Nusra ya Allah ipo karibu, na wote tuseme INSHAALAH.
Maalim huyu mzungu kuna uzi umempa jina la kiislam, hapa umemtaja kwa jina jingine tofauti kabisa na ule uzi mwingine.. Nataka kujua ikiwa huyu bwana ana dual names.
 
Innalillah ' yan bindiga sunkashe makiyaya jahar a taraba.
Nusra ya Allah ipo karibu, na wote tuseme INSHAALAH.
Maalim huyu mzungu kuna uzi umempa jina la kiislam, hapa umemtaja kwa jina jingine tofauti kabisa na ule uzi mwingine.. Nataka kujua ikiwa huyu bwana ana dual names.
Let...
Nadhani unamchanganya na Ridha yeye ni Mholanzi na ni Muislam na ni rafiki yangu akisomesha University of Humburg.

1704402610609.png

Kushoto ni Ridha Simpson na anefuatia ni Kai Kresse
Zentrum Moderner Oriente



 
RAFIKI YANGU PROF. KAI KRESSE WA ZENTRUM MODERNER (ZMO) ORIENT, BERLIN, UJERUMANI

Vipi nilifika Ujermani kwenye taasisi kubwa ya utafiti iitwayo Zentrum Moderner Orient ni kisa kirefu na kinaanza na Prof. Ibrahim Noor Shariff.

Sauti ya Ujermani ilikuwa inataka kufanya kipindi katika Meza ya Duara kuzungumza kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar ya 1964 na walikuwa wamepanga jopo la Ahmed Rajab kutoka London, Dr. Harith Ghassany kutoka Washington DC, Prof. Ibrahim Noor Shariff kutoka Muscat na Saleh Feruzi Makamu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar akiwa visiwani.

Mwenyekiti ni Othman Miraji akiwa DW Bonn.

Prof. Ibrahim Noor Shariff akasema yeye hawezi kushiriki na akapendekeza jina langu.

Hawa washiriki wote mimi tukifahamiana ila Saleh Feruzi.

Mimi nilikuwa Tanga.

Hivi ndivyo nilivyoshiriki katika kipindi kile na kipindi hiki kikasababisha mimi kualikwa ZMO na Prof. Kai Kresse nifanye mhadhara mmoja na niandike mada moja.

Hii ilikuwa mwaka wa 2011 na ndiyo kwanza tumetoka katika uchaguzi wa 2010 uchaguzi ambao Zanzibar kama ilivyo kawaida uligubikwa na matatizo makubwa.

Katika kipindi kile kufupisha mambo mimi na Saleh Feruzi tulipambana sana.

Nadhani kule kwa Saleh Feruzi kutonifahamu ndiko labda kulikofanya kipindi hiki kipendeze sana kwani yeye hakuwa anategemea kutoka kwangu yale ambayo mimi nilikuwa nasema nikimkabili yeye.

Saleh Feruzi hakuwa amepata kukutana na mtu wa aina yangu na hakujua anikabili vipi ninapoeleza katika hsitoria ya CCM Zanzibar yale ambayo wengine wangeyakwepa.

Kipindi kilipokwenda hewani wasikilizaji wengi walivutiwa na jinsi nilivyokuwa naieleza CCM Zanzibar katika chaguzi zote walizoshiriki na kupata shida ya kupata ushindi unaoeleweka.

Wasikilizaji wengi wa DW Idhaa wa Kiswahili walioko nje ya Tanzania wakawa wanampigia simu Othman Miraj kutaka kunifahamu.

Katika hao walikuwa ZMO na Othman Miraji akawaunganisha ni mimi na hivi ndivyo nilivyoalikwa Ujerumani na Kai Kresse ambae akaja kuwa rafiki yangu.

Nilipanda Egypt Air ndege ya usiku hadi Cairo kisha kutoka Cairo ndege ya mchana hadi Berlin.

Kai Kresse alikuja uwanja wa ndege kunipokea.

Nakumbuka ilikuwa inanyesha mvua.

Bahati mbaya sana begi langu likawa halionekani.

Haikunishughulisha sana kwani nilichokuwa nakithamini ni laptop yangu nayo nilikuwanayo ndani ya ndege.

Huu ni moyo wangu siku zote safari zote nakuwanao mkononi ndani ya ndege.

Wakati tunatoka nje ya uwanja likatoka tangazo kuwa natafutwa Customs nikachukue mzigo wangu umeonekana.

Nakumbuka wakati tuko katika gari Kai ananipeleka waliponipangia nyumba sehemu inaitwa Wedding katika mazungumzo akaniuliza kama mimi ni mpenzi wa mpira.

Nikamwambia naipenda Liverpool.

Hapo akaniahadithia Berlin ilikuwaje Fainali ya Kombe la Vilabu Vya Ulaya Bayern Munich walipofungwa na Manchester United wakati Bayern walikuwa wakiongoza kwa magoli mawili.

Magoli yote yalirudi na wakaongezwa goli moja.
Kazi ya Ferguson Boys, Paul Scholes na wenzake.

Anasema siku ile mji mzima wa Berlin ulikuwa kimya umejiinamia.

Mazungumzo yetu yote tunazungumza Kiswahili na hakimpi shida hata kidogo.

Nilishangaa kidogo.

Akanishangaza aliponiambia kuwa mhadhara wangu wenye jina ''Baraza'' utakuwa kwa Kiswahili.

Mada yangu ilikuwa nimeiandika kwa Kiingereza.

Nimekaa ZMO kwa mwezi mzima na Kai Kresse alikuwa kila siku ananikagua ofisini kwangu kuangalia naendeleaje.

Alikuwa kanipangia siku mbili tu za kuja kazini Jumatatu na Alkhamisi.

Mimi nikawa nakuja siku zote isipokuwa Jumamosi na Jumapili.

Berlin ni katika miji migumu niliyopata kufika Ulaya.

Wajerumani si watu wenye kubeba sana tabasamu kwenye nyuso zao na hali ya mji ni hivyo tofauti na miji mingi ya Ulaya niliyopata kufika kama London, Paris, Amsterdam ambako kuna sehemu nyingi tu ambazo mtu anaweza kwenda na kuchanganyika na wenyeji.

Siku moja katika mazungumzo nilimuuliza Kai kuhusu historia ya Ujerumani.

Akaniambia inasomeshwa kama funzo watu wajifunze kutokana na yale yaliyopita hata kama ni machungu.

Kai anakuja sana Tanzania na kila akija atanitaarifu nami nitamfuata hotelini kwake.

Kila akija huwa hakosi kuja na zawadi ya kitabu kwangu.

Kai ni mwenyeji wa Dar es Salaam kiasi kuwa kuna wakati alipanga hoteli Sinza na wakati mwingine New Africa Hotel katikati ya Jiji.

Kote huko nilimfuata kumkagua na kufanya mazungumzo na yeye.

Nimefurahi kuwa Kai kaja kuhudhuria Kongamano la Kimataifa la Shaaban Robert na Kumbukizi zake MUM na nikapata bahati ya kuwaleta yeye na Prof. Ibrahim Noor Shariff Maktaba.

Kai Kresse alichukua muda mwingi sana kupitia kitabu baada ya kitabu katika Maktaba.

Picha ya kwanza Kai Kresse akiwa New Africa Hotel na picha ya Pili akiwa kwenye hoteli moja Sinza.

Picha ya tatu nikiwa Maktaba na wageni wangu na picha ya nne nikiwa na Kai Kresse ZMO, Berlin.

Mzee wewe ni msomi mzuri na uwezo mkubwa na vitabu vyako nimevisoma ,ila tu mara nyingi ume base kwenye imani yako sana .Naamini una madini mengi sana zaidi ya imani yako. Lakini nakukubali sana kwa uvumilivu na ustaarabu kutokana kupata mashambulizi makali hapa jukwaani.
 
Mzee wewe ni msomi mzuri na uwezo mkubwa na vitabu vyako nimevisoma ,ila tu mara nyingi ume base kwenye imani yako sana .Naamini una madini mengi sana zaidi ya imani yako. Lakini nakukubali sana kwa uvumilivu na ustaarabu kutokana kupata mashambulizi makali hapa jukwaani.
Nyio...
Niliamua kufanya utafiti wa mchango wa Waislam nilipogundua kuwa mtafiti yeyote kutoka nje alikuwa akiomba kibali cha utafiti kuhusu Uislam alikuwa anakataliwa kimya kimya.

Nikatambua pia Idara ya Historia Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam haikuwa na chochote katika historia ya Uislam na Waislam lau kulikuwa na mengi ya kutafiti na kuandika.

Mimi sihitaji visa ya kuingia nchini wala kibali cha kufanya utafiti hivyo nikaanza kwa kutafiti historia ya uhuru wa Tanganyika na mchango wa Waislam.

Ndiyo historia hii mnayosoma hapa JF Jukwaa la Historia.

Sina utafiti mwingine nje ya utafiti huu.

Vitabu vyote na research papers nilizoandika ni kuhusu Uislam na Waislam ukitoa Autobiography ya Sal Davis (2023).
 
Mzee wewe ni msomi mzuri na uwezo mkubwa na vitabu vyako nimevisoma ,ila tu mara nyingi ume base kwenye imani yako sana .Naamini una madini mengi sana zaidi ya imani yako. Lakini nakukubali sana kwa uvumilivu na ustaarabu kutokana kupata mashambulizi makali hapa jukwaani.
Nyio...
Niliamua kufanya utafiti wa mchango wa Waislam nilipogundua kuwa mtafiti yeyote kutoka nje alikuwa akiomba kibali cha utafiti kuhusu Uislam alikuwa anakataliwa kimya kimya.

Nikatambua pia Idara ya Historia Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam haikuwa na chochote katika historia ya Uislam na Waislam lau kulikuwa na mengi ya kutafiti na kuandika.

Mimi sihitaji visa ya kuingia nchini wala kibali cha kufanya utafiti hivyo nikaanza kwa kutafiti historia ya uhuru wa Tanganyika na mchango wa Waislam.

Ndiyo historia hii mnayosoma hapa JF Jukwaa la Historia.

Sina utafiti mwingine nje ya utafiti huu.

Vitabu vyote na research papers nilizoandika ni kuhusu Uislam na Waislam ukitoa Autobiography ya Sal Davis (2023) kilichochapwa na Amazon.

1704510133182.png
 
Maalim tupia link ya mahojiano tusikilize ulivyomchana saleh feruzi wa ccm
 
Maalim tupia link ya mahojiano tusikilize ulivyomchana saleh feruzi wa ccm
Jabulani,
Si kama nilimchana ila nilimuuliza ikiwa anajua kuwa Wazanzibari hawana haja na mapinduzi na ndiyo sababu CCM Zanzibar inashindwa kila uchaguzi.

Yeye akajibu kuwa CCM imeshinda.
Nami nikamwambia, "Inaelekea hujui hali ya Zanzibar ikoje."

Mahojiano ya namna hii.

Sina ile audio ni miaka 13 sasa ishapita.
 
Innalillah ' yan bindiga sunkashe makiyaya jahar a taraba.
Nusra ya Allah ipo karibu, na wote tuseme INSHAALAH.
Maalim huyu mzungu kuna uzi umempa jina la kiislam, hapa umemtaja kwa jina jingine tofauti kabisa na ule uzi mwingine.. Nataka kujua ikiwa huyu bwana ana dual names.
Ona umeumbuka
 
Anakuwaje rafiki yako wakati huyo sio muislamu?
Mna...
Kitu gani kinakufanya wewe udhani kuwa siwezi kuwa na marafiki ambao si Waislam?

Huyo hapo chini ni katika mabingwa wa African History ni rafiki ndugu.

Nilimjua wakati akiwa kijana mdogo mwanafunzi alikuja Tanga kunihoji wakati anafanya Ph D akitokea Northwestern University, Chicago.

Tumekuwa marafiki kuanzia miaka hiyo ya mwanzoni 2000 hadi leo na anakuja sana Tanzania.

1704624570294.png

James Brennan University of Iowa
1704624690631.png

James Brennan Kisutu Dar es Salaam
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom