Rafiki wa mchepuko wangu anataka kunioa

Rafiki wa mchepuko wangu anataka kunioa

exceptional lady

JF-Expert Member
Joined
Oct 16, 2015
Posts
332
Reaction score
248
Habari zenu humu ndani,

Mimi mwenzenu ninatoka na mume wa mtu ndo mbaba wangu na ananiweka mjini mwaka sasa, kuna kipindi cha nyuma tulienda zetu huko sehemu ya mbali kidogo kubadilisha hali ya hewa.

Sasa akanitambulisha kwa rafiki zake ambao walikuwa wakifanya kazi pamoja, ila baadae wakatenganishwa. Kijana mmoja akaonyesha kama kanizimia mana alivyokuja akanisalimia akanishika mkono kama shemeji yake.

Sasa tukakutana ghafla siku nyingine tukapeana namba. Sasa kijana akanipenda tangu ile siku kiukweli nilipomuona pia nilijikuta navutiwa nae. Basi tumewasiliana na nampenda na tumepanga mikakati mingi na soon tunataka tukatambulishane ili mwakani Mungu akipenda tuoane.

MTIHANI UNAKUJA HAPA. Mchepuko ananipenda mpaka basi na hii ni kutokana tunaheshimiana na naiheshimu familia yake. Je naanzaje kumwambia huyu mtu? Na mi najua hatoweza kunioa kwa mara ya pili, na mi kijana tumeelewana vyema.

Ebu wenye upeo wanipe mawazo na ushauri jinsi ya kumwambia huyu baba pia nahitaji maneno ya busara maana asije akafa kwa presha.

Wale mliozoea kutukana sihitaji comments zenu za matusi, muwe wastaarabu kwani hakuna asiejua kwamba kuna kuchepuka au kutembea na mke au mume wa mtu huwezi kushauri pita tu kwa ustaarabu.

Karibuni kwa msaada
 
With all due respect, huyo kijana sio muoaji bali ni muonjaji tu.
Anajua unatoka na mfanyakazi mwenzake na yeye anatangaza kukupenda tena anataka mpaka uwe mke?!
Fanya maamuzi taratibu kabla ya kumpa babu mkono wa kwaheri.
 
Anza taaratiibu
Muulize kuwa yeye anajisikiaje kuwa hivyo siku zote
Na je ikitokea wwe unataka kuolewa atajisikiaje au atalichukuliaje? Hapo utakuwa umemwandaa ki psychologia kuwa unaweza olewa
At the end mwambie nilikuwa nataka kujua tu utajisikiaje....na ww kuanzia hapo utakuwa ushajua atakuaje and then mambo yakishakamilika mwambie..
 
{Kama wewe ni muumini mzuri wa dini}

Kabla hujafunga ndoa na huyo kijana nenda katubu dhambi ya uzinzi na mume wa mtu na kupima afya yako .

Then Kaa uongee nae huyo mume wa mtu ana malengo gani na wewe {kama si muislam}, na nini hatma yako katika mahusiano, kisha muweke wazi kuwa unahitaji ndoa halali ili maisha yako yaende salama.
 
Hongera kwa kupata mume... Maadam mwenyezi Mungu keshakupatia wako, achana na mume wa mtu. Muujiza kama huo haujagi mara mbili... You need to move on and build your own family... Cha muhimu usimuoneshee dharau. Muite umshukuru kwa kukulea na kukuweka mjini kwa zaidi ya mwaka, pia mshukuru kwa kuwa kama daraja la kukutanisha na mumeo mtarajiwa... Mwambie kama atahitaji mchepuko mwingine unaweza kumtafutia mtu wa kuku replace lakini kuanzia sasa inabidi muheshimiane kama mashemeji. Ukitumia lugha nzuri kumueleza atakuelewa tu coz mtoto mzuri kama wewe huwezi kuwa mchepuko for life...
 
Kuwa Mchepuko ni kipindi cha mpito na kuolewa ni ahadi ya milele so kuolewa ni muhimu ila mweleze mchepuko wako umepata kijana wa kukuoa
 
Habari zenu humu ndani... mi mwenzenu ninatoka Na mme wa mtu ndo mbaba WANGU Na ananiweka mjini mwaka sasa.. kuna kipindi cha nyuma tulienda zetu huko sehem ya mbali kidogo kubadilisha hali ya hewa. Sasa akanitambulisha kwa rafiki zake ambao walikua wakifanya kazi pamoja ila baadae wakatenganishwa.
Kijana mmoja akaonesha kama kanizimia mana alivokuja akanisalimia akanishika mkono kama shemeji ake .
Sasa tukakutana gafla siku nyingine tukapeana namba. Sasa kijana akanipenda tangu ile siku kiukwel nilipomuona pia nilijikuta navutiwa nae. Basi tumewasiliana Na nampenda Na tumepanga mikakati mingi Na soon tunataka tukatambulishane ili mwakani mungu akipenda tuoane.. MTIHANI UNAKUJA HAPA. mchepuko ananipenda mpaka basi Na hii ni kutokana tunaheshimiana Na naiheshimu familia yake.Je naanzaje kumwambia huyu mtu??? Na mi najua hatoweza nioa kwa mara ya pili,Na mi kijana tumeelewana vema.
Ebu wenye upeo wanipe mawazo Na ushauri jinsi ya kumwambia huyu baba pia nahitaji maneno ya busara maana asije akafa kwa presha.
Wale mliozoea kutukana sihitaji comments zenu Za matusi... muwe wastaarabu kwani hakuna asiejua kwamba kuna kuchepuka au kutembea Na mke au mme wa mtu.. huwezi kushauri pita tuu kwa ustaarabu.
Karibuni kwa msaada
Kama yeye mpaka sasa anakuruhusu uende kuonana na mpaka sasa hakuna muoaji hapo endelea na babu mpaka utakapo pata mmeo wa ukweli
 
Kama yeye mpaka sasa anakuruhusu uende kuonana na mpaka sasa hakuna muoaji hapo endelea na babu mpaka utakapo pata mmeo wa ukweli
Hapana kanizuia kuonana Na babu Na hajui kama naonana nae coz tumetofautiana maeneo ya kuishi mi Na huyu baba tupo mkoa mmoja yeye yupo nje kidooogo
 
Anaweza akawa mmeo wa ukweli ila jaribu tena kumsoma si unajua vijana cc na tamaa za kimwili naweza nikakutamani kumbe nataka nimwalibie tu huyo babu kisa kazi tulivyo tofautiana
 
Huyo kijana ni muoaji wa kweli? Asijekua anataka kumkomoa rafiki yake kupitia wewe.

Mzee anafamilia yake na hatokaa aiache, ataumia sana ukimweleza habari za kuolewa kwako uzuri binadamu tumeumbiwa kusahau, atasahau. Nnachokuhakikishia haitakua rahisi kusitisha mahusiano yenu na msipokua makini utaolewa na bado utaendelea na huyo baba. Fanya maamuzi yatakayokusaidia wewe sasa na baadae.
 
Kuna maswali ya kujiuliza..
1. Ndoto zako ni zipi kuolewa au kuendelea kuwa mchepuko?
2. Shida yako ni kuhudumiwa au kuishi na mwanaume mtakaosaidiana kihisia, kimali..n.k.??

Ukipata majibu kwa kuangalia kila upande wa hao wanaume utajua cha kufanya
 
Babu Hana shida jiulize wewe kwanza utaiweza ndoa? Kama wewe moyo wako upo tayari kuolewa na utavumilia kwa kila hali basi safari njema, lkn Kama unataka kuolewa na ww uonekane una mume basi jipange usijekumkumbuka babu tena.
 
Back
Top Bottom