R.I.P Rev Christopher Mtikila, Jebra Kambole ametukumbusha kitu

kajekudya

JF-Expert Member
Sep 24, 2015
2,469
4,904
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 Kama zilivo katiba za nchi nyingi duniani hasa zile zinazoendeshwa katika misingi ya kidemokrasia inatanabaisha wazi uwepo wa mihimili mitatu katika nchi, yaani Serikali, Bunge na mahakama, kati ya hiyo Mahakama ukiwa ndo muhimili uliopewa majukumu ya kutafasri sheria(ikiwemo katiba yenyewe maana nayo ni sheria).

Katika kutafasiri sheria mahakama imekuwa ikifanya mambo kadhaa wa kadhaa Kama vile kuzitamka baadhi ya sheria kuwa zipo kinyume na katiba au vipengele kadhaa vya katiba vinakiuka haki za binadamu na mikataba kadhaa wa kadhaa ya kimataifa N.K. na moja yaya mashuj katika harakati hizi za kupambana na sheria na vipengele vya katiba vilivyoonekana kuwa kandamizi basi ni the late Rev. Mtikila (R.I.P) kwa wale waliosoma sheria basi huyu ni moja ya watu lazima utakutana naye hasa kwenye somo la Katiba(Constitutional Law), hapo alipoenda Kambole mzee Mtikila yeye alishafika kitambo akipinga kipengele kinachozuia mgombea binafsi. Narudia tena R.I.P Reverend.

Naam, Reverend Mtikila!! Kwanini nimemkumbuka huyu jamaa? ni baada ya ya Leo kukutana na thread ikionesha kuwa my learned brother Jebra Kambole amefungua kesi kwenye Mahakama ya Haki za Binadamu ya Africa( African Court of Human Right) kupinga kipengele Cha katiba kinachokataza kupinga matokeo ya urais yakishakutangazwa. Mimi sitaki kuingia kwenye logic ya kwanini kipengele hicho kiwepo au kisiwepo kwenye katiba kwani hii ni more jurispudential au philosophical aspect hivyo kila mtu anaweza kuwa na mtazamo wake.

Kilichonisukuma kuja hapa jamvini ni namna ambavyo Leo tunawaharakati lukuki ambao kila siku Instagram, Twitter na Facebook account zao zimejaa malalamiko juu ya sheria wanazodai ni kandamizi zilizotungwa na Bunge au hata watu waliokamatwa kwa kwakuwa wamekiuka the so said tyranical laws na wengi wa Hawa ni wasomi wazuri na wengine ni wanasheria kabisa ambao wanajua haya mambo kuliko hata the late mzee Mtikila.

Ninachotaka kusema mzee Mtikila alitambua kuwa mahakama ndo chombo pekee kwa mujibu wa katiba chenye mamlaka ya kutafasiri sheria na alikitimia ipasavyo kuzichallenge sheria na vipengele vya katiba alivyoamini kuwa vilikuwa kandamizi na kwa kiasi kikubwa alifanikiwa.

Kinachonishangaza wanaharakati wa Leo wamegeuza Instagram, Twitter na Facebook kuwa ndo mahakama zao, Zitto, Nape, Bashe, Maria Sarungi Julius Mtatiro na wengine wengi wanalamika huko, kibaya zaidi hata Rais wa Chama Cha Wanasheria(TLS) mwanamama Fatuma kalume naye analalamika huko. Hawa ni watu wanaofahamu wazi kuwa njia ya kisasa na ya busara ya kupambana na sheria za bunge zinazoonekana kandamizi ni kutumia Mahakama and nothing more, na hii ndo maana halisi ya ya mihimili ya dola ambayo inakamilisha kile kinachoitwa Check and Balance. ushahidi upo wa kutosha kuwa Jambo hili linawezekana, Reveland aliweza, Hawa kina Fatuma karume, Zitto, Maria Sarungi na wengine wanashindwa Nini hadi wanaishia kulia lia kwenye mitandao? Yes mtandaoni maana huko wanajijengea umaarufu na kwao umaarufu ni kitu Cha mhimu kuliko kile alichokifanya Mtikila ambacho mwisho wa siku kinawanufaisha watu wote.Badala ya kupambana na hizo sheria wanazoziona kandamizi watu wanapambana na matokeo, wanasubiri Abdul Nondo akamatwe wajaze mandishi kwenye account zao za mitandao, wanasubiri Mtatiro akamatwe wajaze mandishi kwenye account zao na sio kwenda kuomba mahakama kuzi declare sheria hizo kuwa kandamizi, yes! Mtandaoni! Hko wanajipatia umaarufu na kujijenga kisiasa.

Ndio maana nasema alichokifanya Jebra ni kutukumbusha namna pekee Bora ya kupambana na hicho tunachokiita unjust laws, na ujumbe huo uwafikie wote wanaoshinda mitandaoni kulalamika na kwa upana wake zimfikie mama/Bibi Fatuma Karume maaana amebeba dhamana kubwa katika hili badala ya kushinda mitandaoni akitoa mipasho atumie mda mwingine kuratibu mambo Kama haya anayoyafanya Jebla Kambole.

"The Court is there for some one who nocks the door" njia pekee ya kupinga sheria tunazodhami kuwa ni kandamizi ni kwa kwenda mahakamani na si mitandaoni!!

Asante Rev, asante brother Jebra kwa kutukumbusha.
 
Hapa kuna ukweli fulani ambao wapinzani inabidi waukubali licha ya ukweli kuwa hata mahakama zetu kwa kiasi fulani sio huru.

Kuna mambo wapinzani huwa wanayapeleka mahakani lakini hili la Tume ya uchaguzi na sheria ya uchaguzi sijui kwanini hawalipi umuhimu katika kulipeke mahakamani.

Ni bora kujaribu mkashindwa au kufanyiwa figisufigusi then mtakuwa na haki ya kulalamika kuliko kutojaribu kabisa tukabaki walalamikaji.

Wakili Fatma Karume kama sikosei yeye amefungua kesi ya kikatiba kudai Tume Huru na kuipinga hii iliyopo tatizo ni muda unakwenda na hiyo keso sijui hata itatajwa lini mahakamani.

Lingine ni ninolijiuluza hivi mchakato wa kupata katiba mpya uliokwama hauwezi kudaiwa kupitia mahakama?

Kura ya maoni si iko kisheria na ni kwanini isidaiwe kisheria?

Katiba inayopendekezwa ikipita licha ya kasoro zake kadhaa,bado inaweza kutupatia Tume Huru na kupelekea mabadiliko ya sheria ya uchaguzi kuwaondoa Wakurugenzi wa Halmashauri kuwa wasimamizi wa uchaguzi katika maeneo yao.
 
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 Kama zilivo katiba za nchi nyingi duniani hasa zile zinazoendeshwa katika misingi ya kidemokrasia inatanabaisha wazi uwepo wa mihimili mitatu katika nchi, yaani Serikali, Bunge na mahakama, kati ya hiyo Mahakama ukiwa ndo muhimili uliopewa majukumu ya kutafasri sheria(ikiwemo katiba yenyewe maana nayo ni sheria).

Katika kutafasiri sheria mahakama imekuwa ikifanya mambo kadhaa wa kadhaa Kama vile kuzitamka baadhi ya sheria kuwa zipo kinyume na katiba au vipengele kadhaa vya katiba vinakiuka haki za binadamu na mikataba kadhaa wa kadhaa ya kimataifa N.K. na moja yaya mashuj katika harakati hizi za kupambana na sheria na vipengele vya katiba vilivyoonekana kuwa kandamizi basi ni the late Rev. Mtikila (R.I.P) kwa wale waliosoma sheria basi huyu ni moja ya watu lazima utakutana naye hasa kwenye somo la Katiba(Constitutional Law), hapo alipoenda Kambole mzee Mtikila yeye alishafika kitambo akipinga kipengele kinachozuia mgombea binafsi. Narudia tena R.I.P Reverend.

Naam, Reverend Mtikila!! Kwanini nimemkumbuka huyu jamaa? ni baada ya ya Leo kukutana na thread ikionesha kuwa my learned brother Jebra Kambole amefungua kesi kwenye Mahakama ya Haki za Binadamu ya Africa( African Court of Human Right) kupinga kipengele Cha katiba kinachokataza kupinga matokeo ya urais yakishakutangazwa. Mimi sitaki kuingia kwenye logic ya kwanini kipengele hicho kiwepo au kisiwepo kwenye katiba kwani hii ni more jurispudential au philosophical aspect hivyo kila mtu anaweza kuwa na mtazamo wake.

Kilichonisukuma kuja hapa jamvini ni namna ambavyo Leo tunawaharakati lukuki ambao kila siku Instagram, Twitter na Facebook account zao zimejaa malalamiko juu ya sheria wanazodai ni kandamizi zilizotungwa na Bunge au hata watu waliokamatwa kwa kwakuwa wamekiuka the so said tyranical laws na wengi wa Hawa ni wasomi wazuri na wengine ni wanasheria kabisa ambao wanajua haya mambo kuliko hata the late mzee Mtikila.

Ninachotaka kusema mzee Mtikila alitambua kuwa mahakama ndo chombo pekee kwa mujibu wa katiba chenye mamlaka ya kutafasiri sheria na alikitimia ipasavyo kuzichallenge sheria na vipengele vya katiba alivyoamini kuwa vilikuwa kandamizi na kwa kiasi kikubwa alifanikiwa.

Kinachonishangaza wanaharakati wa Leo wamegeuza Instagram, Twitter na Facebook kuwa ndo mahakama zao, Zitto, Nape, Bashe, Maria Sarungi Julius Mtatiro na wengine wengi wanalamika huko, kibaya zaidi hata Rais wa Chama Cha Wanasheria(TLS) mwanamama Fatuma kalume naye analalamika huko. Hawa ni watu wanaofahamu wazi kuwa njia ya kisasa na ya busara ya kupambana na sheria za bunge zinazoonekana kandamizi ni kutumia Mahakama and nothing more, na hii ndo maana halisi ya ya mihimili ya dola ambayo inakamilisha kile kinachoitwa Check and Balance. ushahidi upo wa kutosha kuwa Jambo hili linawezekana, Reveland aliweza, Hawa kina Fatuma karume, Zitto, Maria Sarungi na wengine wanashindwa Nini hadi wanaishia kulia lia kwenye mitandao? Yes mtandaoni maana huko wanajijengea umaarufu na kwao umaarufu ni kitu Cha mhimu kuliko kile alichokifanya Mtikila ambacho mwisho wa siku kinawanufaisha watu wote.Badala ya kupambana na hizo sheria wanazoziona kandamizi watu wanapambana na matokeo, wanasubiri Abdul Nondo akamatwe wajaze mandishi kwenye account zao za mitandao, wanasubiri Mtatiro akamatwe wajaze mandishi kwenye account zao na sio kwenda kuomba mahakama kuzi declare sheria hizo kuwa kandamizi, yes! Mtandaoni! Hko wanajipatia umaarufu na kujijenga kisiasa.

Ndio maana nasema alichokifanya Jebra ni kutukumbusha namna pekee Bora ya kupambana na hicho tunachokiita unjust laws, na ujumbe huo uwafikie wote wanaoshinda mitandaoni kulalamika na kwa upana wake zimfikie mama/Bibi Fatuma Karume maaana amebeba dhamana kubwa katika hili badala ya kushinda mitandaoni akitoa mipasho atumie mda mwingine kuratibu mambo Kama haya anayoyafanya Jebla Kambole.

"The Court is there for some one who nocks the door" njia pekee ya kupinga sheria tunazodhami kuwa ni kandamizi ni kwa kwenda mahakamani na si mitandaoni!!

Asante Rev, asante brother Jebra kwa kutukumbusha.
Mwenyewe huwa nawaza,jambo la kisheria Mtu analipeleka tweeter, tweeter inakua mahakama,jaji followers wake baada ya hapo kesi imeisha kwa kutoa hukum ya kuendelea kupiga kelele zisizo na tija.Kuna mda huwa naamini wanachokuwa wanakipinga huwa hawakiamini au huwa wanafanya propaganda so wakienda mahakaman wanaogopa kuumbuka.Kama Rais kavunja katiba kwa kuzuia mikutano,sioni USAHIHI wa kujaza madesa fb,insta au tweeter wakati sehem husika ya kutafsiri hayo mtu unayoyaona ni sahihi ipo.Mwanasheria anaandaa desa lake refu analitupa jf au fb,huku kweli Kuna watu wenye weledi wa kuchambua sheria na kuzitolea maelezo sahihi?
 
Hapa kuna ukweli fulani ambao wapinzani inabidi waukubali licha ya ukweli kuwa hata mahakama zetu kwa kiasi fulani sio huru.

Kuna mambo wapinzani huwa wanayapeleka mahakani lakini hili la Tume ya uchaguzi na sheria ya uchaguzi sijui kwanini hawalipi umuhimu katika kulipeke mahakamani.

Ni bora kujaribu mkashindwa au kufanyiwa figisufigusi then mtakuwa na haki ya kulalamika kuliko kutojaribu kabisa tukabaki walalamikaji.

Wakili Fatma Karume kama sikosei yeye amefungua kesi ya kikatiba kudai Tume Huru na kuipinga hii iliyopo tatizo ni muda unakwenda na hiyo keso sijui hata itatajwa lini mahakamani.

Lingine ni ninolijiuluza hivi mchakato wa kupata katiba mpya uliokwama hauwezi kudaiwa kupitia mahakama?

Kura ya maoni si iko kisheria na ni kwanini isidaiwe kisheria?

Katiba inayopendekezwa ikipita licha ya kasoro zake kadhaa,bado inaweza kutupatia Tume Huru na kupelekea mabadiliko ya sheria ya uchaguzi kuwaondoa Wakurugenzi wa Halmashauri kuwa wasimamizi wa uchaguzi katika maeneo yao.
Mda wa kudai hayo mtapata wapi wakati SIASA zenu mnaendesha kwa matukio?saiz mko kwenye dreamliner, mkitoka huko mnasubir ccm waje na tukio jipya mwisho 2020 hii hapa mnaanza kulialis ooh tume huru mara cjui nn.
 
Mwenyewe huwa nawaza,jambo la kisheria Mtu analipeleka tweeter, tweeter inakua mahakama,jaji followers wake baada ya hapo kesi imeisha kwa kutoa hukum ya kuendelea kupiga kelele zisizo na tija.Kuna mda huwa naamini wanachokuwa wanakipinga huwa hawakiamini au huwa wanafanya propaganda so wakienda mahakaman wanaogopa kuumbuka.Kama Rais kavunja katiba kwa kuzuia mikutano,sioni USAHIHI wa kujaza madesa fb,insta au tweeter wakati sehem husika ya kutafsiri hayo mtu unayoyaona ni sahihi ipo.Mwanasheria anaandaa desa lake refu analitupa jf au fb,huku kweli Kuna watu wenye weledi wa kuchambua sheria na kuzitolea maelezo sahihi?
Kwenda mitandaoni sio tatizo, tatizo ni kwenda mitandaoni pasipo kwenda na mahakamini.

Mwanasiasa anachokifanya ni lazima aujulishe umma maana umma ndio mwajiri wake hivyo wako sahihi kabisa.
 
Mda wa kudai hayo mtapata wapi wakati SIASA zenu mnaendesha kwa matukio?saiz mko kwenye dreamliner, mkitoka huko mnasubir ccm waje na tukio jipya mwisho 2020 hii hapa mnaanza kulialis ooh tume huru mara cjui nn.
Nyie mnaoenda kujazana Airport kupokea ndege moja kisha kupiga picha ndio mnajiona mko sahihi?

Hivi gharama ya kukusanyika pale mnaweza kuitolea justification wakati kuna wananchi tunasikia wana-share vyanzo vya maji na mifugo?

Wacha nisisema sana nisije kutafutwa na watu wasiojulikana.
 
Mwenyewe huwa nawaza,jambo la kisheria Mtu analipeleka tweeter, tweeter inakua mahakama,jaji followers wake baada ya hapo kesi imeisha kwa kutoa hukum ya kuendelea kupiga kelele zisizo na tija.Kuna mda huwa naamini wanachokuwa wanakipinga huwa hawakiamini au huwa wanafanya propaganda so wakienda mahakaman wanaogopa kuumbuka.Kama Rais kavunja katiba kwa kuzuia mikutano,sioni USAHIHI wa kujaza madesa fb,insta au tweeter wakati sehem husika ya kutafsiri hayo mtu unayoyaona ni sahihi ipo.Mwanasheria anaandaa desa lake refu analitupa jf au fb,huku kweli Kuna watu wenye weledi wa kuchambua sheria na kuzitolea maelezo sahihi?
You nailed it mkuu, nadhani mahakama ingetumika, zipo sheria kibao ambazo mahakama imeshawi kuzideclare kuwa hazifai, na Judges hasa wa High Court to be honest kwenye kesi za Constitutional wanajitahidi Sana, serikali Kuna kesi nyingi sana imepigwa.Tatzo ninaloliona wanaharati na wanasiasa wanaangalia Sana vitu vitakavyowapa umaarufu wao kuliko vile vyenye manufaa kwa jamii nzima, ndo maana wameanzisha mahakama zao huko!
 
Nyie mnaoenda kujazana Airport kupokea ndege moja kisha kupiga picha ndio mnajiona mko sahihi?
Hao ni chama tawala na kwa mujibu wao tume ya uchaguzi na mengind ambayo nyie mnaona hayako sawa wao kwao hayana mattz.So kama upinzani sioni usahihi wa kukimbizana na matukio ya ccm tena ambayo hayana msaada wwt kwa upinzani kushika dola.Chama makini kinaongozwa na agenda kuu sio matukio.Hivi la dreamliner linapita na siku zijazo wanazndua flyover,najua tena mmejipanga kupinga hahahahaha
 
Hao ni chama tawala na kwa mujibu wao tume ya uchaguzi na mengind ambayo nyie mnaona hayako sawa wao kwao hayana mattz.So kama upinzani sioni usahihi wa kukimbizana na matukio ya ccm tena ambayo hayana msaada wwt kwa upinzani kushika dola.Chama makini kinaongozwa na agenda kuu sio matukio.Hivi la dreamliner linapita na siku zijazo wanazndua flyover,najua tena mmejipanga kupinga hahahahaha
Agenga kuu zipi? Hizi za kurudia uchaguzi kutokana na watu kujiuzulu kiutatanishi?

Hizi za kutafuta sifa kila kukicha?

Agenda za kukopa kila kukicha?

Agenda za kuzindua vilivyowahi kuzinduliwa?

Hebu kaa kimya usitutibue hapa.
 
Agenga kuu zipi? Hizi za kurudia uchaguzi kutokana na watu kujiuzulu kiutatanishi?

Hizi za kutafuta sifa kila kukicha?

Agenda za kukopa kila kukicha?

Agenda za kuzindua vilivyowahi kuzinduliwa?

Hebu kaa kimya usitutibue hapa.
Mwezi wa saba huu,lieleze jukwaa nini Agenda kuu za Chadema na kwa nusu ya mwaka huu mmekamilisha ngapi?
 
Mwezi wa saba huu,lieleze jukwaa nini Agenda kuu za Chadema na kwa nusu ya mwaka huu mmekamilisha ngapi?
Hao CHADEMA mnaowadhibiti utadhani uwepo wao hauko kisheria unataka wafanye nini?

Watu kila siku kushinda mahakamani mradi tu muwavuruge.

Ovyo kabisa!!
 
Hao CHADEMA mnaowadhibiti utadhani uwepo wao hauko kisheria unataka wafanye nini?

Watu kila siku kushinda mahakamani mradi tu muwavuruge.

Ovyo kabisa!!
Mkuu haya maelezo ndio majibu ya swali langu?Ka huna cha kujibu lala,nkutakie usiku mwema
 
Hapa kuna ukweli fulani ambao wapinzani inabidi waukubali licha ya ukweli kuwa hata mahakama zetu kwa kiasi fulani sio huru.

Kuna mambo wapinzani huwa wanayapeleka mahakani lakini hili la Tume ya uchaguzi na sheria ya uchaguzi sijui kwanini hawalipi umuhimu katika kulipeke mahakamani.

Ni bora kujaribu mkashindwa au kufanyiwa figisufigusi then mtakuwa na haki ya kulalamika kuliko kutojaribu kabisa tukabaki walalamikaji.

Wakili Fatma Karume kama sikosei yeye amefungua kesi ya kikatiba kudai Tume Huru na kuipinga hii iliyopo tatizo ni muda unakwenda na hiyo keso sijui hata itatajwa lini mahakamani.

Lingine ni ninolijiuluza hivi mchakato wa kupata katiba mpya uliokwama hauwezi kudaiwa kupitia mahakama?

Kura ya maoni si iko kisheria na ni kwanini isidaiwe kisheria?

Katiba inayopendekezwa ikipita licha ya kasoro zake kadhaa,bado inaweza kutupatia Tume Huru na kupelekea mabadiliko ya sheria ya uchaguzi kuwaondoa Wakurugenzi wa Halmashauri kuwa wasimamizi wa uchaguzi katika maeneo yao.
Mwambie dead law lawyer apeleke maana ameshapigwa PO tayari yeye na mtoto wa Wangwe.
 
Mwenyewe huwa nawaza,jambo la kisheria Mtu analipeleka tweeter, tweeter inakua mahakama,jaji followers wake baada ya hapo kesi imeisha kwa kutoa hukum ya kuendelea kupiga kelele zisizo na tija.Kuna mda huwa naamini wanachokuwa wanakipinga huwa hawakiamini au huwa wanafanya propaganda so wakienda mahakaman wanaogopa kuumbuka.Kama Rais kavunja katiba kwa kuzuia mikutano,sioni USAHIHI wa kujaza madesa fb,insta au tweeter wakati sehem husika ya kutafsiri hayo mtu unayoyaona ni sahihi ipo.Mwanasheria anaandaa desa lake refu analitupa jf au fb,huku kweli Kuna watu wenye weledi wa kuchambua sheria na kuzitolea maelezo sahihi?
Hawa ndio barua ya taasisi kwa taasisi( kiofisi) wamepeleka social media kupata sympathy za wananchi.

Kuna uzi mpya rais wa TLS a.k.a dead law lawyer kapigwa knock out, baada ya kuwa wanajisomea maana sheria zinabadilika kila wakati wao wanashinda kwenye social media kukebehi serikali ya awamu ya tano.
 
Back
Top Bottom