Halafu hizi habari zimekaa juu juu tu, hebu mwenye habari iliyokamilika aanike hapa.
Nini sababu ya kifo chake?
Na pia kama kuna historia yake kwa ufupi iwekwe hapa ili wasiomjua wapate kumfahamu vizuri.
MSANII nyota wa miondoko ya Mnanda 'Mchiriku', Omar Omar, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Habari zilizotufikia ni kwamba, Omar Omar aliyetamba na nyimbo mbalimbali ukiwemo ule maarufu wa 'Kupata ni Majaliwa' alifariki nyumbani kwao Temeke, saa chache baada ya kurejeshwa kutoka Hospitali ya Temeke alipokuwa amelazwa kwa siku kadhaa.
Taarifa hizo zinasema kuwa mara baada ya kurejea nyumbani, msanii huyo alizidiwa na hatimaye kufariki na msiba wake upo nyumbani kwao Temeke Mikoroshini.
Akielezea kifo cha msanii huyo Mkubwa Fella ambaye ni jirani yake amesema marehemu Omari Omari alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kifua.
Mwenyezi Mungu Ailaze Roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi. Amen!
Kama sijaelewa kitu hapa,alikuwa amelazwa then akazidiwa muda mfupi baada ya kurudi nyumbani sasa ilikuwaje akaruhusiwa?
Na alikuwa anaumwa tu kifua?mmh
RIP Omar
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.